Basi la Kandahar Investment (Arusha-Dodoma) linaishia njiani kama abiria hawajajaa ndani ya basi, Trafiki wanajua na hawachukui hatua

Basi la Kandahar Investment (Arusha-Dodoma) linaishia njiani kama abiria hawajajaa ndani ya basi, Trafiki wanajua na hawachukui hatua

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
WhatsApp Image 2024-07-01 at 16.24.39_06d707b2.jpg
Muda huu (Julai 1, 2024) nipo safarini natoka Arusha naelekea Dodoma, nilikata tiketi na kupanda katika Basi la Kandahar Investment.

Tumefika Manyoni Stendi, wenye basi wakaanza kutulazimisha abiria tushuke wote ndani ya basi wakidai kwamba gari limeharibika.

Tulipohoji kipi kilichoharibika wakati kila kitu kinaonekana kipo sawa, hawasemi, abiria tukagoma kushuka.

Baadhi ya abiria wakaenda kuwafuata Trafiki kuja kusuluhisha, alipofika hapo huyo Trafiki naye anatuambia hilo basi huwa ndio kawaida yao wakifika maeneo hayo kama hawan abiria wengi ndani wanawashusha na kuwafaulisha.
WhatsApp Image 2024-07-01 at 16.24.38_f0e741a3.jpg
Yaani hata Mamlaka husika ambazo Wananchi wanazitegemea kutatua matatizo ya abiria nao wanakuwa upande wa madereva kwa kukubali kero hii, eti kisa abiriwa hawajajaza basi, hii ni sawa kweli?

Kama hii ni tabia yao na Askari wanawachekea, hii ni hatari! Jeshi la Polisi na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) wanatakiwa kuchukua hatua la sivyo ipo siku abiria watagoma kabisa kushuka na mambo yatakuwa magumu.

Baada ya mzozo wa muda mrefu wametuhamishia kwenye gari lingine la Al _ Jabry Safaris ambalo ni dogo na abiria tumebanana, kwa ufupi ni kero kubwa.


WhatsApp Image 2024-07-01 at 16.31.52_a79599ab.jpg

Abiria tulivyobanana baada ya kufaulishwa
 
Hiyo kampuni niliwahi jisemea sitokuja kuitumia baada ya kugawanyika na moja mmiliki ndiye huyo huyo dereva, hivyo anafanya anavyotaka njiami.

Na kuna mwaka fulani huko walitufanyia karaha sana njiani, walitukalisha Singida masaa kenda kisa hamna abilia.

Ni wana tabia za ajabu sana, nakumbuka askali wa usalama pale singida hawakutusaidia na kilichobaki ni kuwa wapole hadi tunafika, hao (Sumatra) wkt huo ndo hata simu hawajibu.
 
Mimi kabla kupanda basi huwa naangalia jina la basi

Kandahar ni eneo.la Afghanistan ambako Osama Bin Laden yalikuwa makazi yake ya kigaidi

Hilo basi ni la mjahidina mshabiki wa Gaidi Osama bin Laden

Acheni kulipanda
 
Hv na akili zako TIMAMU unapanda bus tofauti na shabiby line kwenye hiyo route? Bro siku zote usafiri wa uhakika arusha dodoma ni shabiby line.
Shabiby ana gari nzuri na customer care ,afu ata wahudumu sio wengi ni kawaida sana kupanda bus la Shabiby mkawa na driver na mhudumu mmoja tu na amna kukaguliwa ticket kama wavamizi ..
 
Muda huu (Julai 1, 2024) nipo safarini natoka Arusha naelekea Dodoma, nilikata tiketi na kupanda katika Basi la Khandahar Investment.

Tumefika Manyoni Stendi, wenye basi wakaanza kutulazimisha abiria tushuke wote ndani ya basi wakidai kwamba gari limeharibika.

Tulipohoji kipi kilichoharibika wakati kila kitu kinaonekana kipo sawa, hawasemi, abiria tukagoma kushuka.

Baadhi ya abiria wakaenda kuwafuata Trafiki kuja kusuluhisha, alipofika hapo huyo Trafiki naye anatuambia hilo basi huwa ndio kawaida yao wakifika maeneo hayo kama hawan abiria wengi ndani wanawashusha na kuwafaulisha.
Yaani hata Mamlaka husika ambazo Wananchi wanazitegemea kutatua matatizo ya abiria nao wanakuwa upande wa madereva kwa kukubali kero hii, eti kisa abiriwa hawajajaza basi, hii ni sawa kweli?

Kama hii ni tabia yao na Askari wanawachekea, hii ni hatari! Jeshi la Polisi na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) wanatakiwa kuchukua hatua la sivyo ipo siku abiria watagoma kabisa kushuka na mambo yatakuwa magumu.

Baada ya mzozo wa muda mrefu wametuhamishia kwenye gari lingine la Al _ Jabry Safaris ambalo ni dogo na abiria tumebanana, kwa ufupi ni kero kubwa.


View attachment 3030708
Abiria tulivyobanana baada ya kufaulishwa
Wewe faulishwa tu.., unataka mtu achome mafuta na gari tupu?
 
Muda huu (Julai 1, 2024) nipo safarini natoka Arusha naelekea Dodoma, nilikata tiketi na kupanda katika Basi la Khandahar Investment.

Tumefika Manyoni Stendi, wenye basi wakaanza kutulazimisha abiria tushuke wote ndani ya basi wakidai kwamba gari limeharibika.

Tulipohoji kipi kilichoharibika wakati kila kitu kinaonekana kipo sawa, hawasemi, abiria tukagoma kushuka.

Baadhi ya abiria wakaenda kuwafuata Trafiki kuja kusuluhisha, alipofika hapo huyo Trafiki naye anatuambia hilo basi huwa ndio kawaida yao wakifika maeneo hayo kama hawan abiria wengi ndani wanawashusha na kuwafaulisha.
Yaani hata Mamlaka husika ambazo Wananchi wanazitegemea kutatua matatizo ya abiria nao wanakuwa upande wa madereva kwa kukubali kero hii, eti kisa abiriwa hawajajaza basi, hii ni sawa kweli?

Kama hii ni tabia yao na Askari wanawachekea, hii ni hatari! Jeshi la Polisi na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) wanatakiwa kuchukua hatua la sivyo ipo siku abiria watagoma kabisa kushuka na mambo yatakuwa magumu.

Baada ya mzozo wa muda mrefu wametuhamishia kwenye gari lingine la Al _ Jabry Safaris ambalo ni dogo na abiria tumebanana, kwa ufupi ni kero kubwa.


View attachment 3030708
Abiria tulivyobanana baada ya kufaulishwa
Sasa unapandaje kandahari kampuni iliyochoka hivyo?? Kata ticket Yako kwenye mtandao upande shabiby au machame
 
Muda huu (Julai 1, 2024) nipo safarini natoka Arusha naelekea Dodoma, nilikata tiketi na kupanda katika Basi la Kandahar Investment.

Tumefika Manyoni Stendi, wenye basi wakaanza kutulazimisha abiria tushuke wote ndani ya basi wakidai kwamba gari limeharibika.

Tulipohoji kipi kilichoharibika wakati kila kitu kinaonekana kipo sawa, hawasemi, abiria tukagoma kushuka.

Baadhi ya abiria wakaenda kuwafuata Trafiki kuja kusuluhisha, alipofika hapo huyo Trafiki naye anatuambia hilo basi huwa ndio kawaida yao wakifika maeneo hayo kama hawan abiria wengi ndani wanawashusha na kuwafaulisha.
Yaani hata Mamlaka husika ambazo Wananchi wanazitegemea kutatua matatizo ya abiria nao wanakuwa upande wa madereva kwa kukubali kero hii, eti kisa abiriwa hawajajaza basi, hii ni sawa kweli?

Kama hii ni tabia yao na Askari wanawachekea, hii ni hatari! Jeshi la Polisi na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) wanatakiwa kuchukua hatua la sivyo ipo siku abiria watagoma kabisa kushuka na mambo yatakuwa magumu.

Baada ya mzozo wa muda mrefu wametuhamishia kwenye gari lingine la Al _ Jabry Safaris ambalo ni dogo na abiria tumebanana, kwa ufupi ni kero kubwa.


View attachment 3030708
Abiria tulivyobanana baada ya kufaulishwa
"Thed weld " dwellers mnatesekeka sana. Mimi nikishatoka kwenye masion yangu Malibu ndani ya limo napelekwa moja kwa moja kwa gulfstream yangu.
 
Back
Top Bottom