Basi la kanisa lapatikana likisafirisha bangi

Basi la kanisa lapatikana likisafirisha bangi

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Polisi waliokuwa wakishika doria kwenye barabara kuu ya Nairobi-Mombasa Jumanne, Oktoba 15, walipatwa na mshangao baada ya kunasa basi la kanisa likiwa linasafirsha bangi.

Kulingana na ripoti za polisi, basi hilo lilikuwa limesafirisha waombolezaji kutoka Kilifi kwenda Homa Bay na wakati wa kurudi likapakiwa na bangi hiyo.

Basi la kanisa lilipatikana likisafirisha bangi kwenye barabara ya Nairobi-Mombasa. Tayari dereva wa basi hilo pamoja na watu wengine wawili walitiwa mbaroni ili kusaidia polisi kwenye uchunguzi wa kisa hicho.

OCPD wa Voi Bernastein Shali alisema basi hilo ni la kanisa la PEFA na lilikuwa limebeba mamia ya misokoto ya bangi.

"Lilipatikana na misokoto 230 ya bangi ambayo inakisiwa kuwa ya takriban shilingi elfu 46. Dereva wake na watu wengine wawili wamekamatwa," Shali alisema.
 
Banana Republic of Kenya, Hadi kanisa linan'gan'ga kuchukua chake mapema kabla mchina hajachukua ikulu
 
Kwani bangi Kenya si imeruhusiwa? Hapo hakuna cha kushangaa Labda tushangae basi la Kanisa kubeba bangi
 
Wako bize kumshangilia kipchoge mabeberu weusi.wanakimbia mbio za kuvunja rekodi ya dunia,wanashindwa kuwakamata alshabab[emoji2][emoji2][emoji2]
 
Sina Hakika Lakini Kuna nchi moja ya afrika hapa karibu karibu na sie imeruhusu bangi sema tu nimesahau kidogo
Sasa kama huna uhakika kwanini uthibitishe moja kwa moja.

Zimbabwe ndiyo imehalalisha bangi ila siyo kwenye uvutaji bali utafiti wa kisayansi.
 
Back
Top Bottom