Basi la Taifa Stars lashambuliwa kwa mawe, lapasuliwa kioo

Basi la Taifa Stars lashambuliwa kwa mawe, lapasuliwa kioo

Freeland

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2012
Posts
14,481
Reaction score
10,227
WATU wasiojulikana jana walilishambulia kwa mawe basi la timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars maeneo ya Kariakoo, Dar es Salaam.

Basi hilo lililokuwa limebeba baadhi ya wachezaji wa timu hiyo waliokuwa wakitoka mazoezini Uwanja wa Karume, Dar es Salaam lilishambuliwa kwa mawe na watu wanaosadikiwa kuwa mashabiki wenye hasira.

Taifa Stars juzi ilifungwa mabao 3-0 na Misri katika mechi yake ya kwanza ya Kundi G kufuzu Fainali za Mataifa ya Afrika 2017 mjini Alexandria.


basiii.jpg

Chanzo: Bin Zubeiry
 
Basi lina kosa gani hadi walishambulie?

Umekosana na jirani, unamvizia mtoto wake akitoka shule anachezea kichapa wakati hata ugomvi wenu haufahamu?

Huo ni uhuni tu kama uhuni mwingine. Hao waliofanya hivyo hawana tofauti na "panya-road".
 
Kama bus lenyewe kila kona kumejaa matangazo ya pombe tu,Hao wachezaji wako salama na hizo pombe? Naona wakiingia tu seat ya konda wanagawiwa beer, mpira na ulevi wapi na wapi!! Bora wangevunja vioo vyote choma moto kabisa halina faida, wangewashusha wachezaji wote bakora kila mmoja kuanzia kocha wao, tumbafuuu kabisa hovyoooo, watu tunakatisha usingizi wetu mijitu inacheza ubishoo tu
 
Basi lina kosa gani hadi walishambulie?

Umekosana na jirani, unamvizia mtoto wake akitoka shule anachezea kichapa wakati hata ugomvi wenu haufahamu?

Huo ni uhuni tu kama uhuni mwingine. Hao waliofanya hivyo hawana tofauti na "panya-road".

We unaona basi limeandikwa 'bonge la kiburudisho kwa watanzania', yaani nani anaburudika kwa kufungwa?
 
Naona wangesubiri kwanza wachezaji wote pamoja na wazee wao wa kamati ya ufundi waingie ndani then walichome moto tu basi, tuanze upya na wachezaji wengine si hawa wachawi wasiofundishika.
 
Jamal Malinzi aunde Tume kuchunguza kwa nini uongozi wake na Taifa Starz ni gozigozi
 
kilicho baki niku wavamiaa kwnye uwanja wa mazoezi nakuwapga viboko....
 
Cha msingi hii timu ifungiwe maana taifa stars kufuzu tu shida sasa si wanatumia kodi za walala hoi bure hawana faida zaidi ya hasara tu kwa taifa
 
Wangelisimamisha tu walitoe upepo pumbavuu!
 
Back
Top Bottom