Bata wa nyama na mayai

CHASHA FARMING

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2011
Posts
7,872
Reaction score
9,263
Usha sikia bata wa nyama ba mayai? Hapa nazungumzia aina mbili za Bata.
1. Pekin au American Duck
2. Khaki Campbell

Hawa pekin ni Broiler bata yaani ni sawa na kuku brouler kwa sababu wana mature mapema.

Ukiwalisha chakula cha kuku wa nyama basi hawa bata utawatoa wakiwa na wiki 6. Hapo watakuwa na kilo 2+.

Khaki Campbell
Hawa ni bata wa mayai, hawa ukizungumzia top 5 ya ndege watagai mayai mengi basi hawa wanaweza shika namba 1 au 2.

Khaki hutaga mayai hadi 300+ kwa mwaka, ukiwapa matunzo vyema watatha kila siku kitu ambacho hata kuku wa kisasa wa mayai hawezi fikia kamwe.

SOKO SASA
Bata kwanza kumbuka hili kwamba mayai yake ndo hutumika kwa Backing Duniani, yaani watu wenye beckar wakipata mayai ya bata basi kamwe hawawezi tumia mayai ya kuku.

Mayai ya bata yana kiini cheipe kingi sana hivyo kiwafanya wawe bora zaidi kwa bekar. Haya tumika kwa sababu hayapo.
Wengi wanao fuga bata wana bata wawili hadi 20 na wanauzaga tu.

Ila mayai yake ni dili mno kwa viwanda vya ku back. Shida hawapati haya mayai ndo maana.

Hawa wa nyama nao wana nyama bora kabisa, bata wa kisasa nyama yao ni tofauti na ya bata wa Kienyeji na haina ile shombo kama bata wa kienyeji hata mayai yake pia.

Hii nyama watu kama Wazungu wana consume sana nyama ya bata, watu wa Asia kama Wachina na pia Wahindi.

Shida Bongo haipatikanai au inapatikana kwa kuunga uunga sana hakuna mtu anaye weza supply nyama wiki nzima.

KUMBUKA HII

Mchaga anapenda sana Mbege, Je mchaga akienda kuishi London atakuwa anaulizia Mbege kwenge mabaa? Jibu ni big Nooo, kwa sababu anajua fika London hawezi pata mbege so hana haja ya kuiulizia.

Ila siku akitokea mtu akawa anatengeneza basi atainunua na atakuwa anainunua sana make ndo kinywajipendwa chake.

Sasa basi, Watu kama Wazungu au Wachina wakifika huku kuna vitu hawawezi ulizia madukani kwa sababu wanajua havipo make hawajawahi viona kwenye maduka ila siki vikiwepo basi watanunua tu.

Usiwe mtu wa kuuliza tu SOKO LIPO? SOKO LIKOJE?

Weupe ndo Pekin na wa kaki na Khaki Campbell wa mayai



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nisha sema hapo juu, kupata bata Quality ni ngumu sana kwa sasa, ila binafisi isingekuwa korona ningeisha ingiza mayai kutoka India.

Hivyo kukuunganisha kwa watu wa bongo utapara bata ila aisee sio wale wanao takiwa hapana na usichezee pesa bure na nyakati hizi ngumu.

Subilia mambo yakisha kuwa vyema baada ya korona ninaweza pata mayai kutoka kwenye Makampuni yenye Parents stock
Niuzie mayai niangulishe

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu shamba lako la bata lipo sehemu gani? Nataka nije nikutembelee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…