Batuli: Sitaki kumsikia Mtunisy

Batuli: Sitaki kumsikia Mtunisy

warumi

R I P
Joined
May 6, 2013
Posts
16,218
Reaction score
18,440
attachment.php

Mtunisi

YOBNESH Yusuph ' Batuli' anayekimbiza kunako soko la Bongo Movies , amefunguka kuwa hataki kusikia habari za aliyekuwa mpenzi wake aliye pia msanii mwenzake, Mtunisi kwani mapenzi yalishaisha.

Akistorisha na paparazi wetu, Batuli alisema hataki kumsikia wala kujua habari za Mtunisi kwani mapenzi yalikuwa zamani lakini kwa sasa kila mtu ana maisha yake yaani yeye Mtunisi ana mke na yeye ana mpenzi wake.

"Mimi kwa sasa nina maisha yangu na Mtunisi ana maisha yake nawashangaa wanaoniandama kwa maneno kwamba bado niko naye , jamani Mtunisi ana mke na mimi nina mpenzi hivyo sitaki kusikia habari hizo kabisa , " alisema Batuli.
 

Attachments

  • index.jpeg
    index.jpeg
    7.3 KB · Views: 358
mmmmmnh hataki kusikia habari zake wakati wako sector moja kwenye mambo ya kazi je
 
mmmmmnh hataki kusikia habari zake wakati wako sector moja kwenye mambo ya kazi je

Anajishaua tu wakati kutwa alikuwa anapost picha za mtunisy instagram , jamaa akam mind akamchana live yeye yupo na mkewe na hana mwanamke mwingine yeyote, sasa ivi na yeye ndo anajifanya eti hataki kumsikia
 
Anajishaua tu wakati kutwa alikuwa anapost picha za mtunisy instagram , jamaa akam mind akamchana live yeye yupo na mkewe na hana mwanamke mwingine yeyote, sasa ivi na yeye ndo anajifanya eti hataki kumsikia

hahaha mapenzi ya kibongo movie ni shiiida hayana happy ending
 
Kwani nani kawazushia tena sema hawa wazee wa bongo movie ni shidaaah?Wanachosema sio wanachotenda usaaniii mpk nje ya industry.
 
Sasa mbona sie wambea hatujasikia kua anaandamwaa au alitaka tujue tuu
 
Batuli ingekuwa vizuri kama angejiweka mbali na media. Alikuwa anaheshimika sana before, but tangu aanze kuropoka. kwenye udaku, naona heshima yake inashuka tu (in Joti's voice). Muda si mrefu sana aliropoka eti hatokaa ampende mwanaume kama alivyompenda mtunisy, akawa anamuweka na insta. Afu leo kanajishaua tena eti simtaki mtunisy. Mmh ama kweli sizitaki mbichi hizi
 
Bongo movies ni chama kisicho rasmi cha wauza mbunye Tanzania...
 
Batuli ingekuwa vizuri kama angejiweka mbali na medias. Alikuwa anaheshimika sana before, but tangu aanze kuropoka. kwenye udaku, naona heshima yake inashuka tu (in Joti's voice). Muda si mrefu sana aliropoka eti hatokaa ampende mwanaume kama alivyompenda mtunisy, akawa anamuweka na insta. Afu leo kanajishaua tena eti simtaki mtunisy. Mmh ama kweli sizitaki mbichi hizi

Si ndo apo kutwa ana post waume za watu, jamaa kampondo ndo anjifanya hatak kumsikia, wakosaji bhaba na atakoma
 
Back
Top Bottom