Pre GE2025 BAWACHA: Usaliti wa Mch. Msigwa ni kukosa fadhila kwa CHADEMA, Tulimuokota akiuza Mitumba Iringa

Pre GE2025 BAWACHA: Usaliti wa Mch. Msigwa ni kukosa fadhila kwa CHADEMA, Tulimuokota akiuza Mitumba Iringa

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Baraza la Wanawake wa CHADEMA (BAWACHA) limetoa tamko la kukerwa na matendo ya Mchungaji Peter Msigwa, aliyekuwa Mwenyekiti wa Kanda ya Nyasa kupitia chama hicho kabla ya kuhamia CCM.

BAWACHA wanasema kuwa Msigwa amekuwa akiwakandamiza viongozi wa CHADEMA katika majukwaa mbalimbali ya kisiasa, hatua wanayoona kama ya kukosa heshima. Mwenyekiti wa BAWACHA mstaafu wa Mkoa wa Geita, Husna Said, amesisitiza hili katika mkutano wa hadhara uliofanyika Kata ya Nyarugusu, Wilayani Geita.

Said ameonya kuwa matendo ya Msigwa yanadhihirisha usaliti kwa chama kilichompa nafasi ya uongozi na akasema kuwa BAWACHA haitakubali tabia hiyo endapo itaendelea. Kwa upande mwingine, Mwenyekiti wa Jimbo la Geita Mjini, Pasquina Ferdinand Lucas, aliwataka wakazi wa Nyarugusu kujitokeza kwa wingi kujiandikisha ili waweze kushiriki kikamilifu katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Vijiji, na Vitongoji, kwa lengo la kuleta mabadiliko.
Pia, Soma:

 
Pumbavu zao,
Kuna aliyekuwa na Hali ngumu kumzidi lissu?!!! Basi aliokolewa na mama Samia, The Mother of Modern Tanzania, na Sasa ni huyo lissu anayeongoza matusi na Kila aina ya uzushi dhidi yake Huku akiungwa mkono kwa Kila Hali na hawa wanaojifanya kulalamika.
 
Nimeamini CHADEMA ndiyo tumani tosha la watz. Mungu ibariki CHADEMA
 
Baraza la Wanawake wa CHADEMA (BAWACHA) limetoa tamko la kukerwa na matendo ya Mchungaji Peter Msigwa, aliyekuwa Mwenyekiti wa Kanda ya Nyasa kupitia chama hicho kabla ya kuhamia CCM.

BAWACHA wanasema kuwa Msigwa amekuwa akiwakandamiza viongozi wa CHADEMA katika majukwaa mbalimbali ya kisiasa, hatua wanayoona kama ya kukosa heshima. Mwenyekiti wa BAWACHA mstaafu wa Mkoa wa Geita, Husna Said, amesisitiza hili katika mkutano wa hadhara uliofanyika Kata ya Nyarugusu, Wilayani Geita.

Said ameonya kuwa matendo ya Msigwa yanadhihirisha usaliti kwa chama kilichompa nafasi ya uongozi na akasema kuwa BAWACHA haitakubali tabia hiyo endapo itaendelea. Kwa upande mwingine, Mwenyekiti wa Jimbo la Geita Mjini, Pasquina Ferdinand Lucas, aliwataka wakazi wa Nyarugusu kujitokeza kwa wingi kujiandikisha ili waweze kushiriki kikamilifu katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Vijiji, na Vitongoji, kwa lengo la kuleta mabadiliko.
Pia, Soma:

MLIMUOKOTA??? YAAANI WANAWAKE WA SIKUHIZI HAWANA ADABU KABISA UNASEMA KABISA MBELE YA WANAUME KUWA KUNA MTU UMEMUOKOTA WEWE MWANAMKEEEEE WE WE KEEEE SHIT WANAWAKE KAMA HWA HAWAWEZI HATA KUOLEWA HAWANQA ADABU MWANAUME HUWEZI KWAMBIA UMEMUOKOTA ILE NI KAZI KAMA KAZI ZINGINE MUWE NA ADABU SHENZI NYIE
 
Ndivyo wanasiasa wa tz walivyo, wanaingia kwenye siasa wakitegemea kupata maslahi zaidi au kuukata.
Kuna mwanasiasa mmoja ni Prof. yeye alikiri mwenyewe kwamba aliokotwa jalalani.
 
Msigwa ndio aliiokota Chadema iringa akaipa na mbunge wa kwanza
Wewe Simbilisi Mchungaji Msigwa alikuwa muuzaji maarufu wa Suluari za Cadet Kwa Wanafunzi wa Shule Bora kabisa ya Bakwata enzi hizo The Highlands sec school

Mimi na Salim ASAS tulikuwa wateja wake wakubwa na Kwenye Siasa Mchungaji Msigwa aliingizwa na mkemia Dr Kibassa Mbunge wa kwanza wa Upinzani 1995 aliyemshinda DG Tiss mstaafu Dr Kitine Kwa sharti kwamba akasome MEMKWA Lakini Msigwa alikataa Kwa madai kuwa wao Wakinga Elimu siyo Kipaumbele

Halafu huyu Husna kama namkumbuka hivi 😂😂😂
 
Chadema hadi mamna ya kuongea wamebuni staili yao ukimsikiliza huyo mama anavyoonge na Lema akiongea staili ni moja moja
 
Back
Top Bottom