yote uko sahihi ila kuongezewa muda Magu hapana mkuu pliz acha mawazo ya kichawi kama hayo! acha kuwaza kibinafsi
Ha haha yaani kusema aongezewe muda nimekuwa MLOZI mweka watu VIZUU....
Sasa huo ubinafsi unatoka wapi komredi wangu?!! Waliofikiria kuweka kipengele cha miaka 5 ili uchaguzi ufanyike walipatia ila wale waliofikiri iwe miaka 4 walikosea?!!
Kwangu Mimi hao wote wako sahihi Kama ilivyo sahihi kwa baadhi ya sisi walalahoi ambao tuna mtazamo tofauti....
UPI HUO?
Nilisuuzika Sana na mh.Ally Kessy mbunge wa Nkasi pale alipoonesha kiu yake ya kutaka ifike siku akiwaona WABUNGE wanajadili uwezekano wa kumuongezea muda mh.Magufuli.
SI UBINAFSI WALA SI UCHAWI
Kama si magufuli Kuna mtu alijua watanzania tutajiamini tena na kutembea kifua mbele kizalendo?!!
Taifa hili halikuwa likielekea kuwa km Kenya?!!
SI siri kuwa vijana wengi wa vyuo vikuu na waliomaliza huko walishakuwa na mentalities za SHORTCUTS katika maisha,wengi walishaiga ama kutaka kuiga kuwa km vijana wa NIGERIA...hv ungewaambia nn wakuelewe na maneno yako mepesi ya UZALENDO Koko huku kila kona ya upeo wa macho yao wanaona shuhuda za MAZONGE yafuatayo;
1.EPA
2.IPTL-ESCROW
3.KAGODA
4.DEEP GREEN
5.MEREMETA
6.TANGOLD
7.TWIGA WATOROSHWAO
8.HUJUMA KTK MABWAWA YA KUZALISHA UMEME
9.UPIGAJI BANDARINI
10.TRA MAPATO HAFIFU
11.MADINI YATOROSHWAYO
BILA SERIKALI KUINGIZA KITU
12.MISHAHARA HEWA
13.WAFANYAKAZI HEWA
14.KUSUASUA KWA BODI YA MIKOPO ELIMU YA JUU HESLB
15.VYETI BANDIA VYA ELIMU KILA KONA
16.RUSHWA KUBWAKUBWA NA NDOGONDOGO KUWA km SALA MAISHANI MWETU et cetera
Katika NAKAMA hiyo KIMIUJIZA anatokea "MWAMUZI"..
MWAMUZI wa kutung'oa kutoka MSAMBWENI...wa kutubadilisha mentalities zetu zenye UPOGO atutayarishe kwenda KANAANI....
Wallahi namng'ang'ania....bora aendelee tu kitu gani bwana kwani mi nautaka URAIS niseme ananichelewesha kupigiwa saluti na CDF?!!
All and all watanzania tunajijua kwa ufundi wetu wa maneno mengi kuliko vitendo..
Wa vitendo kapatikana.
Wa vitendo tunaye.
Twendeni na magufuli kiunzi cha 2020.
Tafakari ukiwa RELAXED.