Bei ya kahawa Kagera yafikia Tsh. 4,100, shangwe kila kona ya mkoa

Bei ya kahawa Kagera yafikia Tsh. 4,100, shangwe kila kona ya mkoa

BWANKU M BWANKU

JF-Expert Member
Joined
Jan 12, 2019
Posts
377
Reaction score
435
Na Bwanku M Bwanku

Kagera ni moja ya mkoa wa kilimo na mazao mbalimbali yanalimwa. Kwasasa ni msimu wa zao la kahawa ambalo ni moja ya zao linalolimwa.

Toka Tanzania ianze, bei ya zao la kahawa ilikua inagotea kuishia 1,100 kuzunguka hapo lakini leo chini ya Rais Samia Suluhu Hassan bei ya kahawa imepanda kwa karibu mara 4 kwa mpigo. Wakulima walioanza kuuza kahawa katika Vyama vya Msingi (AMCOS) kwenye Wilaya ya Karagwe wameuza Tsh 4,100 kwa kilo kwenye mnada uliofanyika Juni 5.

Moja ya Mkulima wa kahawa ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Karagwe na Waziri wa Ujenzi Mhe. Innocent Bashungwa amekiri kupanda maradufu kwa bei ya kahawa.

Waziri Bashungwa anasema Juni 5, 2024 amepeleka kahawa yake kwenye Chama cha msingi Bweranyange wilayani Karagwe kuuza ambapo anatoa ushuhuda kwamba kilo ya kahawa aina ya Arabika kwa mnada wa leo Juni 5 ameuza kwa Tsh. 4,100 kwa kilo ya maganda ya Arabika.

Mhe. Bashungwa anasema wakulima wa Kagera hii ni shangwe tupu na haijapata kutokea. Kwa miaka mingi kahawa iligota kwenye Tsh. 1,100 kwa kilo hadi Mhe. Rais Samia alipoingia madarakani na kuingilia kati kuhusu kuzorota kwa bei ya kahawa kwa muda mrefu.

Waziri amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa sera nzuri za kuinua zao la kahawa pamoja na Wizara ya Kilimo chini ya Waziri wake Hussein Bashe na timu yao kwa kusimamia vyema bei na sasa wakulima mkoani Kagera wananufaika zaidi.

Na Bwanku M Bwanku.

IMG-20240607-WA0000.jpg
 
Mama anapiga kila kona na kila raia wa nchi hii ataguswa,naimani hata lissu atafikiwa muda sio mrefu
 
Na Bwanku M Bwanku

Kagera ni moja ya mkoa wa kilimo na mazao mbalimbali yanalimwa. Kwasasa ni msimu wa zao la kahawa ambalo ni moja ya zao linalolimwa.

Toka Tanzania ianze, bei ya zao la kahawa ilikua inagotea kuishia 1,100 kuzunguka hapo lakini leo chini ya Rais Samia Suluhu Hassan bei ya kahawa imepanda kwa karibu mara 4 kwa mpigo. Wakulima walioanza kuuza kahawa katika Vyama vya Msingi (AMCOS) kwenye Wilaya ya Karagwe wameuza Tsh 4,100 kwa kilo kwenye mnada uliofanyika Juni 5.

Moja ya Mkulima wa kahawa ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Karagwe na Waziri wa Ujenzi Mhe. Innocent Bashungwa amekiri kupanda maradufu kwa bei ya kahawa.

Waziri Bashungwa anasema Juni 5, 2024 amepeleka kahawa yake kwenye Chama cha msingi Bweranyange wilayani Karagwe kuuza ambapo anatoa ushuhuda kwamba kilo ya kahawa aina ya Arabika kwa mnada wa leo Juni 5 ameuza kwa Tsh. 4,100 kwa kilo ya maganda ya Arabika.

Mhe. Bashungwa anasema wakulima wa Kagera hii ni shangwe tupu na haijapata kutokea. Kwa miaka mingi kahawa iligota kwenye Tsh. 1,100 kwa kilo hadi Mhe. Rais Samia alipoingia madarakani na kuingilia kati kuhusu kuzorota kwa bei ya kahawa kwa muda mrefu.

Waziri amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa sera nzuri za kuinua zao la kahawa pamoja na Wizara ya Kilimo chini ya Waziri wake Hussein Bashe na timu yao kwa kusimamia vyema bei na sasa wakulima mkoani Kagera wananufaika zaidi.

Na Bwanku M Bwanku.

View attachment 3011395
Hii nayo ni takataka, kwa hiyo samia ndo kapandisha bei ya kahawa??
 
Mitano tena na ziada ya muhula mmoja kwa mama, hao wapingaji acha waendelee na wivu wao ikulu watapasikia na wajukuu zao
 
Bei ikipanda sana si hatari kwenye uchumi? Shida watanzania wengi hawana uelewa
 
Huku Moshi since 2019
Kahawa bei kilo 5000
Ila ndio hivyo tulishatoka huko na tunafanya mambo mengine kilimo sio sehemu ya kutujengea uchumi imara hasa Kwa huku Kilimanjaro
 
Back
Top Bottom