Bei ya kunganisha umeme mjadala Bungeni, Wabunge wahoji kwanini haibadiliki?

Bei ya kunganisha umeme mjadala Bungeni, Wabunge wahoji kwanini haibadiliki?

Mzee wa Code

Member
Joined
Sep 23, 2024
Posts
61
Reaction score
91
Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania siku ya jana Oktoba 29, 2024 katika kipindi cha maswali na majibu wameibana Serikali kuhusu bei ya kuunganisha umeme maeneo ya mijini, ambapo bei hiyo ni shilingi 320,000.

Akijibu swali la Mbunge wa Korogwe, Timotheo Mzava, Naibu Waziri Judith Kapinga alisisitiza kuwa bei ya umeme kwa mijini kuunganishwa ni shilingi 320,000 na vijijini kupitia miradi ya REA ni shilingi 27,000.

Pamoja na majibu hayo, jambo hili liliendelea kuwa mjadala wakati wa uchangiaji jioni ambapo Mbunge wa Iramba Mashariki, Francis Isack Mtinga, alitoa mfano wa kijiji kilichopo jimboni kwake alichokitajia kwa jina la Iguguno, akisema kuwa kinachajiwa gharama za kuunganisha umeme shilingi laki tatu na ishirini. Mtinga alihoji kwanini bei hii inaendelea kuchajiwa na Tanesco katika maeneo ambayo sio sahihi kama Iguguno, maana ni kijijini.

“Jambo hili tumeshasema hapa mara nyingi, lakini Tanesco wamekuwa wagumu sana kutekeleza jambo hili. Kila wakati ukiwafuata wanasema michakato inaendelea nchini nzima,” alisisitiza Mtinga.

Aliongeza kuwa bei ya kuunganisha umeme kuendelea kuwa hiyo inafubaza maendeleo ya Watanzania, na akapendekeza bei ya umeme iwe shilingi ishirini na saba hata mijini, kwa sababu miundombinu ya mjini ni rahisi.
 

Attachments

  • MBUNGEmtinga .mp4
    28 MB
Nachukia watu wanaoutukuza umasikini
 
Tatizo kizimkazi alipoingia tu madaraka akalazimisha wananchi wakamulikwa Kwa laki tatu na ishirini ndani ya mita 20 haijalishi mjini au vijijini wakati huohuo yeye Kila siku anasafiri Kwa Kodi zetu na halipi Kodi hata ya kununua sukari.kilakitu anapewa Bure na wanaolipishwa ni wananchi.Muda mwingine unatamani kuhama Nchi kabisa Kwa haya ma mbo yake ya hovyo
 
Back
Top Bottom