Bei ya mafuta kupanda kiasi hiki inasababishwa na nini, na kwanini mamlaka zipo kimya?

Bei ya mafuta kupanda kiasi hiki inasababishwa na nini, na kwanini mamlaka zipo kimya?

KITEKSORO

JF-Expert Member
Joined
Sep 25, 2012
Posts
346
Reaction score
425
Wapendwa humu JF bila shaka mtakubaliana nami kwamba kwa miezi kadhaa bei ya mafuta ya petroli na dizel imeendelea kupaa tu hapa Tanzania. Kwa baadhi ya maeneo bei imefika hadi 2,700-2,800 kwa lita moja.

Natamani kujua sababu ya bei kwenda juu kiasi hicho, na upandaji huo kuendelea bila kubadilika kwa kushuka.

Kwa kuzingatia umuhimu wa bidhaa hiyo, pia serikali kupitia mamlaka husika ingeliangalia hili suala, kulitolea ufafanuzi na pia kuangalia namna ya kudhibiti bei isiendelee kupaa.

Maisha yamekuwa magumu sana yaani sana, kwani mafuta yanagusa kila mahali na yanagusa maisha ya kila mtu😭😭😭😭😭
 
Watakwambia soko la dunia huko pipa moja limepanda bei,sometimes naonaga bora tu mwisho wa dunia ufike ijulikane moja
Yaani hususan kipindi hiki cha lizabeta ni balaa Unaweza kweli kutamani mwisho wa dunia ufike
 
Back
Top Bottom