Mpita Njia
JF-Expert Member
- Mar 3, 2008
- 6,997
- 1,172
Hii ni sehemu ya tangazo lililotolewa na Ewura leo
Bei za jumla na rejareja kwa aina zote za mafuta zimebadilika ikilinganishwa
na toleo lililopita la tarehe 01 Februari 2012. Katika toleo hili, bei ya
rejareja kwa mafuta aina zote zimepanda kama ifuatavyo: Petroli
imeongezeka kwa Sh 153/lita sawa na asilimia 7.67; Dizeli imeongezeka kwa Sh
119/lita sawa na asilimia 6.01; na Mafuta ya taa yameongezeka kwa Sh
104/lita, sawa na asilimia 5.35. Mabadiliko haya ya bei za mafuta hapa
nchini yametokana na mabadiliko ya bei katika soko la dunia na kushuka
kidogo kwa thamani ya shilingi ya Tanzania dhidi ya dola ya Marekani.
Thamani ya shilingi imeshuka kwa asilimia 0.13 ikilinganishwa na thamani ya
shilingi katika toleo lililopita. Bei za jumla kwa kulinganisha matoleo haya
mawili zimebadilika kama ifuatavyo: Petroli imeongezeka kwa Sh 152.70/lita
sawa na asilimia 7.97; Dizeli imeongezeka kwa Sh 118.77/lita sawa na
asilimia 6.24; na Mafuta ya taa yameongezeka kwa Sh 104.49/lita, sawa na
asilimia 5.57.
Bei za jumla na rejareja kwa aina zote za mafuta zimebadilika ikilinganishwa
na toleo lililopita la tarehe 01 Februari 2012. Katika toleo hili, bei ya
rejareja kwa mafuta aina zote zimepanda kama ifuatavyo: Petroli
imeongezeka kwa Sh 153/lita sawa na asilimia 7.67; Dizeli imeongezeka kwa Sh
119/lita sawa na asilimia 6.01; na Mafuta ya taa yameongezeka kwa Sh
104/lita, sawa na asilimia 5.35. Mabadiliko haya ya bei za mafuta hapa
nchini yametokana na mabadiliko ya bei katika soko la dunia na kushuka
kidogo kwa thamani ya shilingi ya Tanzania dhidi ya dola ya Marekani.
Thamani ya shilingi imeshuka kwa asilimia 0.13 ikilinganishwa na thamani ya
shilingi katika toleo lililopita. Bei za jumla kwa kulinganisha matoleo haya
mawili zimebadilika kama ifuatavyo: Petroli imeongezeka kwa Sh 152.70/lita
sawa na asilimia 7.97; Dizeli imeongezeka kwa Sh 118.77/lita sawa na
asilimia 6.24; na Mafuta ya taa yameongezeka kwa Sh 104.49/lita, sawa na
asilimia 5.57.