Bei za mafuta zinaendelea kupanda, ruzuku haijasaidia sana, hatua zinazochukuliwa haziwiani na ukali wa tatizo

Bei za mafuta zinaendelea kupanda, ruzuku haijasaidia sana, hatua zinazochukuliwa haziwiani na ukali wa tatizo

Dr Eli Isaac

Member
Joined
Jul 23, 2022
Posts
11
Reaction score
12
Kwenu Rais Samia, VP Mpango, Mwigulu, Mafuru, Benki Kuu, Makamba na Mulamula.

Kwa Ufupi,
Serikali Mlishauriwa na Wabunge kuhusu namna ya kukabiliana na suala la bei za Mafuta kupanda.

Mkaambiwa:-
1. Wekeni Utaratibu wa Kununua Oil Futures Options kama Hedging Mechanisms za ku-lock in Bei za Mafuta pale zinapokuwa nafuu. Mkaambiwa pia kuhusu namna bora ya kuendesha Hifadhi ya Kimkakati ya Mafuta.
Kimya, Bei zinapanda [emoji1745]

2. Changanyeni utaratibu wa PBPA na Mfumo wa Ununuzi wa Mafuta kwa Njia za Ushindani(huku Ubora ukihakikiwa). Hii ni ili kuwezesha upatikanaji wa Mafuta ya Bei Nafuu. Kimya, Bei zinapanda [emoji1745]

3. Tumieni marafiki zetu wenye urafiki na Upande wa Marekani na Upande wa Urusi: mfano China na India, ili wanaponunua mafuta Urusi, wanunue zaidi ili hiyo ziada tulipie sisi tupewe tuitumie. Wao wanasifika kama HARD BARGAINERS huko sokoni Ueusi na wananunua Mafuta mengi kwa bei nafuu sana. Na hii ni mpaka hivi leo. Imewafanya hata Marekani na wenzake kwenye G7 waanze kufikiria KUONDOA BAADHI YA VIKWAZO kwa Urusi kwa sharti jipya kwamba sasa nchi za G7 au Ulaya zitazonunua Mafuta ya Urusis basi Urusi ikubali kuziuzia kwa bei nafuu.Na wanataka kuhakikisha hili kwa kuweka Price Caps. La msingi hapo ni kwamba Urusi ina mafuta mengi na iko katika nafasi ambayo haipati hasara kuyauza kwa Bargain au Hard Bargain. Ref: How Russian Oil Is Making Its Way From Europe To Asia | OilPrice.com
Kimya, Bei zinapanda[emoji1745]

Na mimi nawaambia:

1. Hizo Macroeconometric Models na Structural Equations mnazotumia zimepigwa na Supply Shocks, zimepoteza Forecasting Accuracy na nyie wenyewe mnahaha kurudisha Integrity yake. Linaeleweka.

2. Tumekumbwa na Complex Problem. Kuna Simple Problems, Complicated Problems na Complex Problems. Kanuni ya kutatua Simple Problem ni rahisi: Panga halafu Tekeleza. Kanuni ya kutatua Complicated Problem nayo ipo hivyohivyo japo utekelezaji inabidi ufuatiliwe na kurudi kupanga tena. LAKINI Complex Problem inatatuliwa hivi: TEKELEZA halafu PANGA. Anza kutekeleza mambo au suluhu zinazoelekea kufanya kazi.

Tunasema ,kwenye Complex Problem, PLAUSIBLE solutions zinapokuwepo, zitekeleze, pima matokeo, hasa pale matokeo yanapotegemewa kutoleta madhara zaidi ya yale yaliyopo, halafu lichukue kama darasa na ndipo ulitumie kama Mpango unaoweza kuutumia tatizo kama hilo likitokea. Hivyo kwenye kutatua Complex Problem : TEKELEZA halafu PANGA.

Nyie Mpo, Bei za Mafuta zinapaa, Vituo vya Kampuni fulani hivi vinaishiwa mafuta na vinakaa wiki nzima havina mafuta, Balozi zetu India na China zipo, Balozi wa India na China wapo hapa kwetu, Waziri wa Mambo ya Nje yupo, Mfano wa kuiga kwa habari ya kununuliwa mafuta au gesi kutoka Urusi upo, Wataalam wapo. LAKINI pamoja na yote haya mnaingia baridi na kigugumizi at the expense ya sisi wananchi tunaofuatilia yote yanayoendelea huko duniani kwa habari ya namna Nchi zinavyotatua matatizo yao ya Mafuta.

Labda mmeridhika na hali hii[emoji1745][emoji1549]

INASIKITISHA SANA.
 
Mzee unaweza kuandika hata maandiko elfu tatu halafu anakuja Makamba au yule commissioner wa nishati wa EWURA watakupinga kwa hoja dhaifa sana hata Makamba hajui lolote linaloendelea kwenye soko la mafuta na wako tayari hata ikifika Bei Ni elf 5000 Ni sawa tu wao kuona Ni sahii tunashida Sana na Hawa viongozi.

Yaan waziri anasema hata majirani zetu wanabei kubwa bora sisi siwaelewagi kabisa mfumuko huu wa Bei siyo kingine ni Bei ya mafuta serikali imeshindwa kudhibiti na kumanage tutateseka Sana hadi tuite Maji mma.
 
Mzee unaweza kuandika hata maandika elf tatu halafu anakuja Makamba au yule commissioner wa nishati wa EWURA watakupinga kwa hoja dhaifa sana hata Makamba hajui lolote linaloendelea kwenye soko la mafuta na wako tayari hata ikifika Bei Ni elf 5000 Ni sawa tu wao kuona Ni sahii tunashida Sana na Hawa viongozi

Yaan waziri anasema hata majirani zetu wanabei kubwa Bora sisi siwaelewagi kabisa mfumuko huu wa Bei siyo kingine Ni Bei ya mafuta serikali imeshindwa kudhibiti na kumanage tutateseka Sana hadi tuite Maji mma
Wanakera, wanakasirisha na wanaudhi. Inasikitisha.
 
Mwisho wa siku raia wa chini ndio tunateseka na hizo tozo kibao
 
Mwambie makamba kama anautaka u raisi hapa ndio pakuonyesha anaweza, afanye juu chini mafuta yarudi bei ya zamani.

Mama pia kama anataka kurudi 2025 ajitahidi ashushe bei ya bidhaa chini ,
Mafuta ya bei chee yapo watumie akili.

Hizo 100B za ruzuku ni bora wange peleke pale kiwanda cha kichakata mafita ghafi kifufuke tupate mafuta na. Kemikali nyingine.

Hivi jamani mbona mkwawa hakusoma darasa hata moja la wazungu lakini alijua nini wahehe wanataka,uongozi si usome uongozi ni maoni.
 
Mwambie makamba kama anautaka u raisi hapa ndio pakuonyesha anaweza ,afanye juu chini mafuta yarudi bei ya zamani

Mama pia kama anataka kurudi 2025 ajitahidi ashushe bei ya bidhaa chini ,
Mafuta ya bei chee yapo ,watumie akili.

Hizo 100B za ruzuku ni bora wange peleke pale kiwanda cha kichakata mafita ghafi kifufuke tupate mafuta na. Kemikali nyingine.

Hivi jamani mbona mkwawa hakusoma darasa hata moja la wazungu lakini alijua nini wahehe wanataka,uongozi si usome uongozi ni maoni
Hatuwezi kukubali kuwa na rais bogus kama yule. Kichwa chake chenye komwe kama goti la ngamia hakina uwezo wa kuchakata idea nzuri za maendeleo ya hili taifa.
 
Mi naamini solutions za kupata mafuta ya bei rahisi ipo ni vile tu viongozi wetu wamekubali kufikiria sawa na dunia inavyofikiri . Lakini tungepata viongozi ambao ni independent thinkers kama Mwendazake nadhani solution ingepatikana
 
Bei ya mafuta katika nchi yetu inaathiriwa na Kodi pamoja na tozo. Zile tozo za miamia kila lita ziliondolewa halafu zikarudishwa tena halafu mategemeo ya unafuu yanatoka wapi?
Jibu lilikuwa rahisi tu ni kupunguza Kodi kwenye mafuta na kuondoa tozo kwenye mafuta hiyo ingesaidia sana kupunguza ukali wa ugumu wa maisha.
 
Back
Top Bottom