Bench la ufundi Serengeti boys kuendelea kuwepo mpaka sasa ni dharau kwa Watanzania

Bench la ufundi Serengeti boys kuendelea kuwepo mpaka sasa ni dharau kwa Watanzania

redio

JF-Expert Member
Joined
Aug 27, 2016
Posts
5,813
Reaction score
12,921
Uzarendo ni pamoja na kukubali kushindwa katika michezo na kuwapa nafasi watanzania wengine wajaribu kutengeneza timu iliyo bora zaidi ya Serengeti boys.
Kwa michezo yote mitatu iliyochezwa hakuna namna benchi lote la ufundi kuendelea kufundisha timu iyo.Itakua ni matumizi mabaya ya fedha na rasilimali za Nchi kwa benchi la ufundi kuendelea kuwepo.
Mkumbuke Tff moja ya vyanzo vyake vya fedha ni wananchi mmojammoja pamoja na viingilio kwenye mechi mbalimbali za ligi, viwanja vya serikali ambavyo kwa ujumla ni vinatokana na kodi za Watanzania au Nguvu walizotumia kujengwa kwa viwanja ivyo.
 
Mtukufu wetu. Angejua kwamba hivi vitoto vitakuja kutia haibu ni Bora ili bilioni 1 angepeleka madawa zaidi maosptalini kuliko kufedheheshwa namna hii.
 
Kwani wanajitambua sasa ? yaani wanataka washindweje ndo wapishe hizo nafasi ?
 
Kwani hadi sasa bado benchi la mvundo sorry ufundi lipo? Linatutafuta nini
 
Halafu benchi lenyewe sasa ni kina Peter manyika!! Yaani unafikiria mara mbili kumtimua manyika? Sijui mkapa? Kwa CV ipi hasa walizonazo?
 
Hizi habari kwamba watoto wenye uwezo waliachwa wakachukuliwa watoto ambao wazazi wao wanazo ni za kweli?
 
Tanzania hatuna utamaduni wa kuwajibika hadi utimuliwe, so watakuwepo na undugu ndugu wao
 
Hizi habari kwamba watoto wenye uwezo waliachwa wakachukuliwa watoto ambao wazazi wao wanazo ni za kweli?

Lolote linawezekana. Hata ukiliangalia benchi la ufundi, utakuja kugundua tff waliamua kuwaachia timu watu wenye njaa ili iwe rahisi kwao tff kupiga pesa ya umma vizuri. Kuna mastermind wa ile timu (Kim Poulsen) aliondolewa kimya kimya kwenye benchi la ufundi pasipo wadau wa michezo kujua sababu! na mwisho wa siku aibu tumebeba watanzania wote.
 
Back
Top Bottom