Lady Whistledown
JF-Expert Member
- Aug 2, 2021
- 1,147
- 2,008
Watu Watatu, wakiwemo Waziri wa zamani na Mkuu wa Ulinzi wa Rais Patrice Talon, wamekamatwa kwa tuhuma za kupanga mapinduzi, huku uchunguzi mkali ukiendelea ili kuwabaini Wahusika wengine
Mwendesha Mashtaka wa Serikali aliwaambia Waandishi wa Habari, Waziri wa zamani wa Michezo, Oswald Homeky, alikamatwa Septemba 24, 2024 akimkabidhi Mkuu wa Walinzi wa Rais, Elonm Mario Metonou, Mifuko 6 ya pesa
Wapelelezi walisema Kanali Djimon Dieudonne Tevoedjre alikuwa akihongwa ili asipinge mapinduzi yaliyopangwa kufanyika Septemba 27, 2024 nchini humo
Pia alikamatwa mfanyabiashara, Olivier Boko, rafiki wa Rais Talon, ambaye hivi karibuni alionyesha kuwa na malengo ya kisiasa. Mawakili na wafuasi wa Boko walilaani kukamatwa kwake wakikiita "utekaji nyara" na wanataka aachiliwe mara moja. Uchunguzi unaendelea kubaini washukiwa wengine, mwendesha mashtaka alisema.
Kumekuwa na mapinduzi ya kijeshi mara nane na majaribio kadhaa ya mapinduzi tangu mwaka 2020 katika Afrika Magharibi na Afrika ya Kati, maeneo ambayo yalikuwa yamepiga hatua kuondoa sifa yake kama "ukanda wa mapinduzi," lakini ukosefu wa usalama na ufisadi unaoendelea umefungua tena mlango kwa viongozi wa kijeshi kuchukua hatua
Mwendesha Mashtaka wa Serikali aliwaambia Waandishi wa Habari, Waziri wa zamani wa Michezo, Oswald Homeky, alikamatwa Septemba 24, 2024 akimkabidhi Mkuu wa Walinzi wa Rais, Elonm Mario Metonou, Mifuko 6 ya pesa
Wapelelezi walisema Kanali Djimon Dieudonne Tevoedjre alikuwa akihongwa ili asipinge mapinduzi yaliyopangwa kufanyika Septemba 27, 2024 nchini humo
Pia alikamatwa mfanyabiashara, Olivier Boko, rafiki wa Rais Talon, ambaye hivi karibuni alionyesha kuwa na malengo ya kisiasa. Mawakili na wafuasi wa Boko walilaani kukamatwa kwake wakikiita "utekaji nyara" na wanataka aachiliwe mara moja. Uchunguzi unaendelea kubaini washukiwa wengine, mwendesha mashtaka alisema.
Kumekuwa na mapinduzi ya kijeshi mara nane na majaribio kadhaa ya mapinduzi tangu mwaka 2020 katika Afrika Magharibi na Afrika ya Kati, maeneo ambayo yalikuwa yamepiga hatua kuondoa sifa yake kama "ukanda wa mapinduzi," lakini ukosefu wa usalama na ufisadi unaoendelea umefungua tena mlango kwa viongozi wa kijeshi kuchukua hatua