SoC04 Benki Kuu (BoT) ifanyie kazi maendeleo ya Sarafu za mtandaoni na serikali ipitishe matumizi yake Nchini

Tanzania Tuitakayo competition threads

pro12membe

Member
Joined
Jun 2, 2024
Posts
37
Reaction score
66
UTANGULIZI
Mafanikio siku zote hayaendi kwa watu wanaosubiria hali au mazingira yawe kamili ,
Bali mafanikio huenda kwa wale wanaojitoa na kufanyia kazi mambo au fursa zote zinazokuja mbele yao.

Hivi karibuni kumeibuka wimbi kubwa la matumizi ya sarafu za mtandaoni, kwa nchi zilizoendelea zinazojulikana kama cryptocurrency.

Ni ukweli usiofichika kuwa dunia sasa inakuwa na kuendelea haraka sana kiteknolojia, muda si mrefu watu wengi watatoka katika matumizi ya sarafu za kawaida zijulikanazo, kama ( fiat money/ currencies), na kuhamia katika matumizi ya sarafu za mtandaoni.

Ni nini maana ya sarafu za mtandaoni ( cryptocurrency ).
Sarafu za mtandaoni; ni aina za sarafu za kidijitali ambazo zinategemea sana teknolojia ya blockchain katika kufanikisha miamala na matumizi yake.
Sarafu hizi zinapatikana katika simu janja za mikononi , hivyo inatoa fursa kwa watu wasio na akaunti za benki kutumia huduma za kifedha pia.
Mfano wa sarafu za mtandaoni ambazo ni marufu na zinatumika na watu wengi ni pamoja na Bitcoin (BTC), Ripple(XRP), Litecoin (LTC), Cardano (ADA) na pi (π )


Jee kuna haja kwa benki kuu kufanyia kazi maendeleo haya?.

Nikijiuliza swali hilii, naona majibu yake sahihi kabisa ni Ndio. Hii ni kwasababu tayari baadhi ya watu katika nchi yetu,
na mimi nikiwa kama mmoja wa hao watu tunafanyia kazi fursa hii na baadhi ya watu tayari wameanza kufaidika, na matunda ya sarafu hizi.
Nikinukuu kauli ya mheshimiwa Raisi, Samia Suruhu Hassan.
kutoka katika moja ya hotuba (speech) yake anasema,

" kwa mfano kwa upande wa sekta ya fedha tumeshuhudia kuibuka kwa sarafu mpya zinazotumika kwa njia ya kimtandao yaani Blockchain au cryptocurrency. Najua nchi nyingi ikiwemo Tanzania hazijakubali au kuanza kuzitumia sarafu hizo . Hata hivyo wito wangu kwa benki kuu ni vyema mkaanza kufanyia kazi maendeleo hayo".

Hivyo basi kauli hiyo inaonyesha ni wazi na dhahiri kuwa kuna umuhimu wa bank kuu kuanza kufanyia kazi maendeleo ya Sarafu za mtandaoni kutokana na faida na ubora wa miamala yake.

Faida ya sarafu za mtandaoni kwa nchi na watumiaji kwa ujumla.
Sarafu za mtandaoni au cryptocurrency zina faida nyingi ambazo zimevutia watumiaji wake na wawekezaji kote ulimwenguni , zifuatazo ni badhi ya faida chache zitokanazo na sarafu za mtandaoni.

1. Uhamisho wa haraka wa fedha na Rahisi:
sarafu za mtandaoni zinaruhusu uhamisho wa fedha wa haraka na rahisi bila kuhitaji kupitia benki au huduma za kati, mfano wakala na vituo vingine vya kifedha, hii imekuwa faida kubwa sana kwa uhamisho wa kimataifa ambapo hufanyika kwa muda mchache kulinganisha na ule wa ki benki za kawaida.

2. Inatoa uhuru wa kifedha : watumiaji wa sarafu za mtandaoni wanapata uhuru zaidi wa kudhibiti pamoja na kutumia fedha zao kwani hakuna mamlaka ya kati kama vile benki au taasisi za kifedha za mtu binafsi wala za serikali inayodhibiti Sarafu hizi.

3. Inatoa fursa za uwekezaji: sarafu za mitandaooni zimekuwa chanzo kikubwa sana katika kutoa fursa za uwekezaji kwa watu wengi ambapo thamani yake hufanya kuwa kama dhahabu inavyopanda siku baada ya siku.

4. Gharama zake ni za chini sana katika uhamisho:
katika suala la ada katika Sarafu za mtandaoni gharama zake ni nafuu sana na mara nyingi ni ndogo ikilinganishwa na ada zinazotozwa na benki au huduma za kutumia fedha.

5. Uwazi na usalama: sarafu nyingi za mtandaoni zinatumia teknolojia ya blockchain hii hutoa uwazi wa miamala na inahakikisha usalama kupitia mifumo wanayotumia, ambapo inafanya kuwa na ugumu kwa wadukuzi wa data kuweza kubadilisha data hizo.

6. Soko lake ni la kimataifa: kutokana sarafu za mtandaoni zinapatikana katika simu ya mkononi na kutumika duniani kote, hivyo basi hii itawezesha biashara pia uwekezaji wa kimataifa bila kubadilisha sarafu za kigeni. Faida hii inakwenda sambambaa kabisa na maono ya waziri wa fedha mheshimiwa Mwigulu Nchemba. kutaka kusitisha matumizi ya (dollars) za kimalekani kwa wafanya biashara na taasisi za kifedha katika nchi ya Tanzania. Hivyo basi sarafu za mtandaoni zitasaidia sana katika kufanikisha jambo hili.

7. Kukuza ujumuishaji wa kifedha: Sarafu za mtandaoni zinaweza kusaidia kwa kiasi kikubwa mno katika kuwajumuisha watu ambao hawana huduma za kifedha kama vile akaunti za benki, katika mfumo wa kifedha wa kidijitali na kupataa huduma za fedha kwa urahisi zaidi.

AINA CHACHE ZA SARAFU ZA MTANDAONI.
Hapaa naweza kutaja na kuelezea sarafu chache maarufu zinazotumika duniani.
Zifuatazo ni aina kadha za sarafu za mtandaoni;
  • Bitcoine ( BTC); Hii ndio sarafu ya kwanza kuazishwa ya mtandaoni, ambayo imeudwa na kundi tuu la watu linalojiita "Satoshi Nakamoto" Mnamo mwaka 2008. Bitcoins ndio sarafu inayoshika kasi zaidi na maarufu zaidi kwa sasa duniani siku hizi inachukuliwa kama dhahabu ya kidijitali. Na ni sarafu yenye gharama kubwa zaidi duniani.
Picha kutoka mtandaoni katika (application ya diagram ie. ) Huu ni mfano wa alama ya sarafu ya mtandaoni ambayo inajulikana kama Bitcoin.
  • Litecoin (LTC); Hili ni tawi dogo la Bitcoin iliyoundwa na mtaalam Charles' lee mnamo mwaka 2011 , hii inajulikana sana kwa miamala ya haraka sana na gharama zake ni nafuu sana , inatumika pia na taasisi za kifedha.


Picha kutoka mtandaoni katika (application ya diagram ie), inaonyesha alama ya Sarafu ya Litecoin ( LTC) inavyoonekana huko mitandaoni ikiwa na picha ya mwanzilishi wa sarafu hiyo.
  • Pi {π} : pia hii ni aina ya Sarafu mpya ya kidijitali ambayo imeingia kwa kasi sana katika nchi nyingi za Afrika na kupata wadau wengi sana ikiwemo Tanzania, sarafu hii inapatika kupitia simu yako yakononi. Kwasasa sarafu hii ipo sokoni katika kutafuta wateja na idadi ya watu iongezeke ili kuweza kuanza na kufanikisha matumizi yake, Na nikawaida kwa kila sarafu ya mtandaoni inapokuwa inaanza huanza kutolewa bure, ili watumiaji wawe wengi. Kama ilivyokuwa kwa Bitcoin ( BTC) na Litecoin (LTC) wakati zinaanza kuingia Nchini nazo zilikuwa bure zinapatikana kwa (ku mining) kuchimba kila siku ndani ya kila baada ya masaa ishirini na nne (24 hours).


Picha kutoka mtandaoni katika (application ya diagram ie); huu pia ni mfano wa sarafu ya pi( π) inavyoonekana huko mitandaoni .

Jinsi mtu anavyoweza kupata sarafu hizi za mtandaoni.

Ni vigumu kueleza kwa maneno hivihivi, pasi na vitendo. Ilaa nitajitahidi kwa kadri ya uwezo wangu, kuweza kuelezea walau kwa uchache ni vipi mtu anaweza kuzipata sarafu hizi kupitia simu yake ya mkononi na hatua kadhaa chache za kuchukua baada ya kuwa na application hizo.


1. Kwanza kabisa kufungua akaunti ya sarafu ya mtandaoni inaweza kuwa ni Litecoin (LTC) pi π , au nyinginezo.

2. Kisha utahitajika kuchimba
(mining) Kila baada ya masaa 24 kwa siku mara moja, hakuna gharama zozote katika kufanikisha jambo hilo ni wewe kuwa na bando la kutosha tuu kwenye simu yako.

3. Kisha kufuatilia kila siku maelekezo ambayo utakuwa unapatiwa na kuambiwa ufanye katika sarafu husika mfano, kuimarisha security cycle ya akaunti yako pamoja na kumalizia hatua zingine, ili kuruhusu kuanza kufanyika kwa miamala. Mfano Kutoka kwenye mfumo wa pi π kwenda kwenye pesa za kawaida.

4. Pia inaruhusu kualika wengine nao waweze kujiunga na mradi huo, ili kuruhusu ongezeko la watu zaidi.

5. Mwisho kabisa utatakiwa ujisajiri kwa tarifa zako halisi na majina sahihi na sio zakutunga kama majina tunayotumiaga katika mitandao mingine ya kijamii.

Hitimisho.
Tutambue kuwa Hakuna mafanikio ya siku moja , pia tukikubali uhalisia wa mambo tunaweza kubadili Chochote na kukifanya kwa ufanisi mkubwa sana.
Hivyo basi wito wangu kwa benki kuu kuanza kufanyia kazi maendeleo haya ya sarafu za mtandaoni, kama vile kuanda mifumo na njia zitakazotumika katika kulipa na kuhudumia watu ndani ya miaka 5 had 25 ijayo, vilevile serikali ipitishe matumizi yake Nchini.
 
Upvote 57
Ok
 
Asante Kwa hii taarifa
 
Kazi nzuri sana 👊
 
Of course bro hata mim ninayo hii inayoitwa pi na ipo Kasi balaa ni kweli bhana serikali ilione hilii idadi ya watu inazidi kuongezekaa
 
Keep shining
 
Kazi nzuri kabisa Kijana 💪
 
Chapisho zuri sana
Daah itakuwa vizuri sana kama serikali italifatilia hilii kwa kina watanufaika wengi sana na wao piiaaaa
 
Kazi
 
Ni kweli serikali ina haja ya kulitizama hili, uchumi kupanda nikuhakikisha Fursa zilizopo wananchi wake wanaeza kuzitumia kiurahisi na kufaidika nazo.
mfano nchi jirana (Kenya) kwenye suala hili wamepiga hatua mpaka Kuna hizo electronic machine za drawing.,

nikiwa nakuunga mkono ndugu yangu kwahili serikali itengeneze mifumo ifuatayo:-
1. Kuhidhinisha na kutengeneza mazingira wezeshi Kwa biashara ya cryptocurrency, ikiwa forex trading.
2. Kuruhusu njia rahisi ya kuweka pesa na kutoa pesa direct na link bank ilio secure.
3. Kuruhusu mafunzo Kwa mananchi na jinsi ya kunufaika.
4. Serekali inahaja ya kukusanya walio na mafunzo Kwa sasa na kushirikiana nao kwaajili ya kuleta mapinduzi ya kiuchumi.
 
Daah ahsante sanaa bro
Comment nzuri sana hii,,
Tanzania inatakiwaa ilishughurikie hili piaa nakuunga mkono kwa asilimia 💯 🤚 🤚
 
Nzuri iyoo
 
Nice work
 
Mtu wa maana kabisa, vote for Professor Membe hutajutia kura yako
 
Umewaza mbali sana bro
Mm ushauri wangu pia serikali itoe elimu kwa Jamiii kuhusu hiii sarafu Peper au cryptocurrency.

Mdaa utaongeaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…