Benki nyingi nchini Kenya zakabiliwa na kushuka kwa mitaji

Benki nyingi nchini Kenya zakabiliwa na kushuka kwa mitaji

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Benki nyingi nchini Kenya zinakabiliwa changamoto ya kusawazisha gawio kwa wanahisa na kuhifadhi mtaji kustahimili misukosuko ya kiuchumi inayosababishwa na janga la Covid-19.

Chama cha Mabenki cha Kenya (KBA) kinasema benki zinakabiliwa na kushuka kwa mitaji.

Habil Olaka, mtendaji mkuu wa KBA aliambia gazeti moja la Afrika Mashariki Kuna uwezekano mkubwa wa mkusanyiko wa benki kuzorota wakati huu wa janga la Covid-19 kwa sababu idadi ya wakopaji wanakabiliwa na changamoto na wana uwezekano mkubwa wa kutotimiza masharti yao ya ulipaji wa mkopo.

Sekta ya benki ya Kenya inakabiliwa na uwezekano wa kushuka kwa faida kwa mwaka ulioishia Desemba 31, 2020.

Benki sita - Standard Chartered Bank Kenya, Absa Bank, I&M Bank, Diamond Trust Bank (DTB), NCBA na Benki ya Ushirika - wametoa onyo la faida kwamba mapato yao yangeanguka kwa zaidi ya asilimia 25 ikilinganishwa na 2019.
 
Tatizo riba,
Ukichunguza zile bank zinafanya biashara ya share na si riba utakuta wako vizuri tu
Riba ni unyonyaji
 
Back
Top Bottom