Benki ya Posta, fungueni tawi Wilaya Kilindi

CK Allan

JF-Expert Member
Joined
Aug 14, 2013
Posts
2,781
Reaction score
6,139
kwa wafanyakazi, na watu binafsi waliopo wilaya ya kilindi watakubaliana na mimi kuwa uwepo wa benki moja tu (nmb) unazua mafanikio mengi mfano suala la mikopo... nmb wameweka masharti kibao ambayo yanamnyima mtu kupata mkopo kwa wakati na pia mikopo wanayotoa ni midogo sana... benki ya posta ikatumia makosa na udhaifu wa nmb kujitanua zaidi, katika mkoa wa tanga ni wilaya mbili tu lushoto na kilindi ambazo benki ya posta wanadai wamewekewa zengwe... kuna siku niliwasiliana na afisa mikopo wa benki ya posta tanga kumuuliza kwanini hawana tawi kilindi akadai mkurugenzi amegoma kusaini mikataba yao...

Kiukweli nimechoka kuwa mteja wa nmb ingawa sina jinsi maana ipo benki pekee hapa kilindi... Tafadhali benki ya posta kama handeni mmeweza msishindwe kilindi...
allan.
 
Kaka, NMB wamerekisha mikopo yao kuanzia mwisho wa mwezi huu, ambapo sasa unaweza kukopa hadi kwa miezi 60
 
Kaka, NMB wamerekisha mikopo yao kuanzia mwisho wa mwezi huu, ambapo sasa unaweza kukopa hadi kwa miezi 60

ni kweli kaka, lakini bado masharti yao magumu kaka, nimefika juzi wamenizingua.
 

Ndo tunalifanyia Kazi hilo!
 

Ndo tunalifanyia Kazi hilo! Hii ndo nchi pekee naona mtu mmoja anataka kufunguliwa Bank! imuhudumie yeye tuu! mkuu huwa tunafanya Market Research kwanza kabla ya kupenyeza tawi lolote la bank hii!
 
Ndo tunalifanyia Kazi hilo! Hii ndo nchi pekee naona mtu mmoja anataka kufunguliwa Bank! imuhudumie yeye tuu! mkuu huwa tunafanya Market Research kwanza kabla ya kupenyeza tawi lolote la bank hii!

Acha uongo wa wazi wazi, ndugu unataka umeshawahi kufika kilindi? umeshafika pale posta na kumuuliza yule dada .... kuwa ni wafanyakazi wangapi wanaulizia benki ya posta? je unajua kuna wengi wameenda hadi handeni? nahisi wewe ni nmb unaogopa.
 
Acha uongo wa wazi wazi, ndugu unataka umeshawahi kufika kilindi? umeshafika pale posta na kumuuliza yule dada .... kuwa ni wafanyakazi wangapi wanaulizia benki ya posta? je unajua kuna wengi wameenda hadi handeni? nahisi wewe ni nmb unaogopa.

ni kweli kaka, lakini bado masharti yao magumu kaka, nimefika juzi wamenizingua.


Hhaha!
Kaka ya kweli hayo?
Hilo tawi halina MAnager ukalalamika?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…