Hamjambo Watanzania!
Ikiwa imepita miezi michache tangu benki ya Twiga iunganishwa na TPB kutokana na kushindwa kujiendesha yenyewe sasa ni zamu ya TWB.
Hali ya taasisi za kifedha kuunganishwa haikuwahi kutokea kwa mfululizo miaka ya nyuma.
Kwakuwa TPB BANK PLC ni mali ya umma basi tunayo nafasi ya kujadili kwa lengo la kujenga uchumi wetu hususani katika taasisi za kifedha. Awali najiuliza ni kwanini benki zinazofeli zinaunganishwa na TPB wakati inajulikana zina NPL kubwa na small customer base?