Mngurimi
JF-Expert Member
- May 27, 2020
- 819
- 790
Nimetoka kusikiliza mahojiano ya mgombea urais wa JMT kupitia tiketi ya chama cha ACT-Wazalendo muda mfupi uliopita kwenye kituo cha DW. Mtangazaji katupa maswali ambayo nilikuwa nikitamani sana siku moja kusikia BM mwenyewe akiyatolea ufafanuzi licha ya kusikia juu juu tu.
Moja kati ya swali ambalo kaulizwa ni kuhusu yeye kuhusishwa sana na ukachero na yawezekana kabisa akawa amepandikizwa na chama tawala ili kuuwa nguvu ya upinzani kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 28 mwaka huu.
Bernard Kamillius Membe ameweka wazi kabisa kuwa, yeye ameamua mwenyewe kugombea na kuwania nafasi ya urais wa JMT wala sio pandikizi kama fikra za baadhi ya watu zinavyodai. "Kama ni kutumwa, unadhani nitakuwa nimetumwa na nani? Kwa lengo lipi? Au kwa kupata cheo kipi, ambacho kufumba na kufumbua unaweza kujikuta umetumbuliwa?", amesema Membe.
Mbali na hayo yote, Ndugu Bernard Kamillius Membe amesema kitendo cha yeye kuja ACT-Wazalendo ni kwa sababu ya kuchoshwa na mambo yalivyokuwa yakifanyika upande wa pili na ndiyo maana kulikuwa na idadi kubwa sana ya wabunge waliomfuata na wala hawakwenda kwenye vyama vingine.
Source: DW
Moja kati ya swali ambalo kaulizwa ni kuhusu yeye kuhusishwa sana na ukachero na yawezekana kabisa akawa amepandikizwa na chama tawala ili kuuwa nguvu ya upinzani kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 28 mwaka huu.
Bernard Kamillius Membe ameweka wazi kabisa kuwa, yeye ameamua mwenyewe kugombea na kuwania nafasi ya urais wa JMT wala sio pandikizi kama fikra za baadhi ya watu zinavyodai. "Kama ni kutumwa, unadhani nitakuwa nimetumwa na nani? Kwa lengo lipi? Au kwa kupata cheo kipi, ambacho kufumba na kufumbua unaweza kujikuta umetumbuliwa?", amesema Membe.
Mbali na hayo yote, Ndugu Bernard Kamillius Membe amesema kitendo cha yeye kuja ACT-Wazalendo ni kwa sababu ya kuchoshwa na mambo yalivyokuwa yakifanyika upande wa pili na ndiyo maana kulikuwa na idadi kubwa sana ya wabunge waliomfuata na wala hawakwenda kwenye vyama vingine.
Source: DW