Bernard Morrison aomba radhi Simba kwa utovu wa nidhamu alioufanya

John Haramba

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2022
Posts
365
Reaction score
1,374
Mshambuliaji wa Simba, Bernard Morrison ameomba radhi kwa wachezaji wenzake, benchi la ufundi pamoja na kwa uongozi wa klabu yake kwa utovu wa nidhamu aliouonyesha.

Imeelezwa kuwa Morrison ambaye ni raia wa Ghana ametumia group la mtandao wa WhatsApp kuomba radhi kwa wenzake kisha akaomba wafikishe salamu kwa uongozi, lakini pia aliutuma ujumbe huo pia kwa viongozi.

Mchezaji mmoja wa Simba ameeleza kuwa Morrison ambaye alidaiwa kutoroka kambini wiki iliyopita, kisha kusimamishwa na uongozi wa klabu kutokana na kufanya matukio ya kujirudia, anajutia makosa yake aliyoyafanya lakini uongozi haujatoa jibu lolote kwake hadi sasa, na hata wachezaji wenzake hawajamjibu chochote.

Simba wapo katika mchakato wa kujiandaa na mchezo wa Hatua ya Makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya ASEC Mimosas ya Ivory Coast, Jumapili Februari 13, 2022.

Source: Mwanaspoti

 
Ile post yake ya something huge ilikuwa ni mbwembwe kuonesha mchizi ana plan B

Lakini baada ya GSM kujitoa udhamini na mfululizo wa malalamiko kutoka Yanga jamaa amefikia maamuzi mazuri kaweza kuzisoma alama za nyakati

Kagundua wazo la kurudi yanga ni wrong move
 
Huyo ameshasaini mkataba wa awali huko Utopolo asituchanganye aende huko kwa wavuta bangi wenzake
 
Leta ushauhidi......
.
Morrison kagoma kuandika barua ya kuomba radhi
 
Morrison aondoke Simba hana maana yoyote, wala asiombe msamaha wowote.
 
"haa bana nugu nugu ni mtu mbaya sana,ananifundisha mimi kiswahili ya matusi bana"
Nikasema"hii maweee"Nungungungu atatuharibia huyu mtu.
 
source mwanasport? Uko serious kabisa unawaamin mwanasport
 
yaani akiruhusiwa kurudi kambini tuu, atawaraghai wachezaji woote na mwisho wa siku simba itafungwa na kila itakayo kutana nayo...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…