Besigye ashinda kesi, kulipwa Sh80 milioni

Besigye ashinda kesi, kulipwa Sh80 milioni

real G

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2013
Posts
5,227
Reaction score
5,299
Aliyekuwa mgombea urais Dk Kizza Besigye ameshinda kesi yake dhidi ya Shirika la Utangazaji Uganda (UBC) kwa kukataza matangazo yake ya kampeni za mwaka 2011.

pic+besigye.jpg


Mahakama Kuu chini ya Jaji Margaret Ogulion Jumatatu ilitoa hukumu iliyompa ushindi Dk Besigye na fidia ya Sh80 milioni zikiwa ni gharama na uharibifu baada ya kusikia alililipa shirika hilo la kitaifa Sh21 milioni kwa ajili ya matangazo yake ya kampeni kabla ya uchaguzi wa rais mwaka 2011, lakini wao (UBC) walishindwa kuheshimu makubaliano hayo.

Wakati wa usikilizwaji wa kesi, Besigye alilitaka shirika la UBC kumrejesha Sh21 milioni.

Aliiambia mahakamani kuwa shirika hilo la kitaifa lilichukua fedha zake wakati wa kampeni ya urais wa 2011, lakini kamwe halikutangaza matangazo yake ya kisiasa.

Hilo lilimkasirisha Besigye ambaye pia alisema kesi yake imechukua muda mrefu katika mahakama baada ya kufunguliwa mwaka 2011.

Miongoni mwa yaliyopewa uzito, pia Besigye aliomba UBC izuiwe kufanya ubaguzi wa watu kwa misingi ya itikadi za kisiasa.

Kwa mujibu wa kesi hiyo iliyofunguliwa dhidi ya UBC na Mkurugenzi Mtendaji wa zamani Edward Musinguzi, kampuni hiyo ya utangazaji ilipokea Sh21 milioni kutoka kwa wakala wa vyombo vya habari wa Besigye, Big Ideas, ili kutangaza mara 200 kampeni zake za urais mwaka 2011, lakini hawakufanya hivyo.

Chanzo: Mwananchi
 
Yeah vizuri. Ndiyo mambo ya TBC ya ubaguzi wa kuonyesha mikutano ya vyama vingine vya kisiasa zaid ya CCM. Wakati TBC ni chombo cha walipa kodi wote bila kujali vyama vyao. Ubaguzi huo peke yake ni kesi dhidi ya TBC ya kutotoa haki sawa.
 
Back
Top Bottom