Betri ya gari yenye waranti ya mwaka mmoja imekufa baada ya miezi 10 wanakataa kunibadilishia

Betri ya gari yenye waranti ya mwaka mmoja imekufa baada ya miezi 10 wanakataa kunibadilishia

Silicon Valley

JF-Expert Member
Joined
Mar 6, 2012
Posts
1,092
Reaction score
1,118
Kama kichwa kilivyo,

Nilinunua battery ya gari March 2019, leo imekufa narurisha dukani , wanagoma kunibadilishia wakidai ilitakiwa ninunue battery kubwa zaidi kwa ajili ya hiyo gari yangu, na tulibadilisha na kuweza saizi ile ile iliokuja na gari, na ndio saizi yake halisi.

Ni wapi niyapeleke haya malalamiko yangu?

Naombeni ushauri.
 
Unawaonea mkuu...wangekuwa wao ndo manufacture sawa ila na wao ni wafanyabiashara

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni kweli ki binadamu unaongea vizuri, hatujasumbuana hata kidogo, kama ni hivyo hakuna haja ya wao kutumia warranty kibiashara na tunanunua kwa bei za juu kwa sbb ya warranty feki, mbaya zaidi tunazo battery zaidi ya 10 kutoka kwa huyo huyo supplier tukijivunia warranty yake ?
 
Usijekuingia mkenge kushawishiwa kununua kitu chochote (kama ulikuwa ukipendi) eti kwasababu ya warrant! Warrant zote zinakuwa na vigezo na masharti ambayo ukienda kuwashitaki wanakugeuzia kibao kuwa ulivunja kigezo fulani na sharti Fulani! Warrant za uhakika ziko kwa products ambazo wanazimonitor wenyewe. Kwa mfano kuna kampuni ya umene wa jua inaitwa "Zola" ambayo wanakukopesha products zenye thamani hadi million 6 unalipa kidogo kidogo kwa muda wa miaka 3 usipolipa hupati umeme na ukishindwa wanakuja kuchukua mitambo yao! Sasa hao wakikupa warrant ya miaka 3 ni uhakika ndo maana wanakupa kwa kianzio cha bei chini ya 5% ya gharama halisi. Lakini wengine wakupe product uende nayo hawajui unakaa wapi na mazingira yapi alafu utegemee kikiharibika ukirudishe wakubadilishie? Thubutu? Nilinunua Freezer Mlimani city yenye warrant ya mwaka mmoja! Ikazingua nawapigia simu wakanizingua mpaka nikachoka! Afrika bado saana! Nunua chochote at your own risk!
 
Kama kichwa kilivyo,

Nilinunua battery ya gari March 2019, leo imekufa narurisha dukani , wanagoma kunibadilishia wakidai ilitakiwa ninunue battery kubwa zaidi kwa ajili ya hiyo gari yangu, na tulibadilisha na kuweza saizi ile ile iliokuja na gari, na ndio saizi yake halisi.

Ni wapi niyapeleke haya malalamiko yangu?

Naombeni ushauri.
Kwanza naomba nikuelekeze kitu kwanza unapochagua battery ya gari usichague battery kulingana na ukubwa wake Bali chagua battery ambayo inatoa kiasi cha moto kinachoendana na matumizi ya gari yako, kwa mfano gari kama crown, mark x ni miongoni mwa gari ambazo kitako chake cha battery kinaruhusu kuweka battery yenye ukubwa wa N40/NS45 lakini ni miongoni mwa gari ambazo zinaitaji battery yenye moto mwingi kuanzia 350Amp sasa chukulia mfano ukaenda dukani unaitaji battery za crown ambazo kiuhalisia ni N40/NS45 ukamkuta muuzaji ana kampuni 3 spark MF, exide (power last) na let say atlas na hizo battery zote tatu zinatofautiana bei kulingana na ubora na kiwango cha moto kilichomo lakin kutokana na spark kuwa bei rahisi kuliko brand nyingine ukaamua kuchukua hiyo kisa tu inalingana na battery ambayo inatoka kumbe umesahau gari yako inahitaji umeme mwingi sana na huo ambao unatoka kwenye battery mpya ulioiweka haina uwezo wa kutoa kiasi hicho, ninachokuomba na kukusiistizia nunua battery kulingana na kiasi cha moto kinachotolewa ndani yake na sio size ya battery. Na jiulize kwann BMW series 03 inachukua battery yenye size ya N40/NS45 lkn ukiifungia spark MF au exide yenye ukubwa huo inaweza isiwake? Ni kwa sababu hiyo battery haina moto wa kutosha kuwasha mitambo iliyomo kwenye gari hiyo, narudia kusisitiza nunua battery ya gari yako kulingana na moto unaotoka kwenye battery na sio size na ndo maana zinatofautiana bei na ubora ijapokua zote ni size tofauti
Tena kubwa tu mfano wake ni spark MF N40 ni 135,000 exide N40 ni 150,000 na atlas N40 ni 210,000? Hiyo tu inatosha kukuonyesha battery gani ununue kulingana na gari yako na kitu cha mwisho warranty ya battery inatolewa na watengenezaji wenyewe na sio mawakala na ukisoma hicho kitabu kimeandikwa kabisa wakala au seller haruhusiw kukupa warranty yoyote hivyo kama kuna muuzaji anawambia ana warranty huyo anakosea sisi wauzaji hatuna uwezo wa kukupa mteja warranty

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni kweli ki binadamu unaongea vizuri, hatujasumbuana hata kidogo, kama ni hivyo hakuna haja ya wao kutumia warranty kibiashara na tunanunua kwa bei za juu kwa sbb ya warranty feki, mbaya zaidi tunazo battery zaidi ya 10 kutoka kwa huyo huyo supplier tukijivunia warranty yake ?
Nunua kitu kulingana na ubora na sio warrant supplier hatoi warrant ya battery ila mtengenezaji ndo mwenye jukumu la kukupa warranty soma kitabu chao hasa kwa spark MF na poweelast wana vitabu juu ya battery vimeandikwa kabisa wakala hatoi warrant yyt ya battery na sometime Haya madude ya umeme sio ya kulaumu sana maana nayo yanatengenezwa na binadamu pengine mchanganya kemikali alikosea kiwango kinachostahil akaweka kidog hivyo ndo sababu imekosa nguvu na Haya madude ni kubahatisha tu mengine yanatumikaga miez 3 tu yanagoma

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom