Analyse
JF-Expert Member
- Jan 19, 2014
- 17,637
- 47,413
Najua pesa imekuwa ngumu sana mtaani. Inapatikana kwa shida sana, so chunga usije kuitoa kwa urahisi.
Kuna jamaa mmoja huko IG anajiita "big sales" akijinadi kuwa ni official samsung na LG seller kwa east africa. Ukitembelea page yake anavitu vingi vizuri, ila vinapatikana kwa bei chee sana. Location yake anasema ni Chakechake Pemba, opposite na NMB bank ya zamani.
Wandugu huyo mtu ni tapeli na hana duka kule Pemba. Mpaka sasa najua wengi sana wameshalizwa na huyu jamaa, ila wanalia kimya kimya.
Najua JF sio mahala pake, ila nimeamua kuandika hapa nikiamini wengi wapo humu. Na sababu ya kuandika imetokana na kukutana na binti ambae alikuwa amekubalia na big sales amuuzie Iphone kwa tsh milion moja. Binti katanguliza laki 7,hiyo 3 iliyobaki wakakubaliana ataimalizia akishapatiwa mzigo wake. Baada ya kulipa, binti alifika hadi pale dukani akagandishwa zaidi ya masaa 4 anasubiria. Baadae ikabidi akubali kuwa kalizwa, akaondoka analia.
Sababu ya pili ambayo pia imepeleka niandike ni kumsaidia yule Mzee halisi mwenye duka lililopo opposite na NMB bank pale chake. Huyu Mzee ameshapata kesi na malalamiko mengi ambayo hayajui, imefikia hatua ameenda polisi kulipoti na kupatiwa RB. Maana wateja wanaenda pale kwa wingi kufata mali zao walizolipia ambazo yeye (Mzee) hazifahamu.
Hapo juu ni link ya ukurasa wa wa huyo mtu anayejiita big sales.
To share is to care.
Thanks.
Analyse.
Kuna jamaa mmoja huko IG anajiita "big sales" akijinadi kuwa ni official samsung na LG seller kwa east africa. Ukitembelea page yake anavitu vingi vizuri, ila vinapatikana kwa bei chee sana. Location yake anasema ni Chakechake Pemba, opposite na NMB bank ya zamani.
Wandugu huyo mtu ni tapeli na hana duka kule Pemba. Mpaka sasa najua wengi sana wameshalizwa na huyu jamaa, ila wanalia kimya kimya.
Najua JF sio mahala pake, ila nimeamua kuandika hapa nikiamini wengi wapo humu. Na sababu ya kuandika imetokana na kukutana na binti ambae alikuwa amekubalia na big sales amuuzie Iphone kwa tsh milion moja. Binti katanguliza laki 7,hiyo 3 iliyobaki wakakubaliana ataimalizia akishapatiwa mzigo wake. Baada ya kulipa, binti alifika hadi pale dukani akagandishwa zaidi ya masaa 4 anasubiria. Baadae ikabidi akubali kuwa kalizwa, akaondoka analia.
Sababu ya pili ambayo pia imepeleka niandike ni kumsaidia yule Mzee halisi mwenye duka lililopo opposite na NMB bank pale chake. Huyu Mzee ameshapata kesi na malalamiko mengi ambayo hayajui, imefikia hatua ameenda polisi kulipoti na kupatiwa RB. Maana wateja wanaenda pale kwa wingi kufata mali zao walizolipia ambazo yeye (Mzee) hazifahamu.
Hapo juu ni link ya ukurasa wa wa huyo mtu anayejiita big sales.
To share is to care.
Thanks.
Analyse.