Biashara gani ulifanya ukiwa chuoni?

Hapa ndipo unakosea,

Tambua nyumbani umetoka peke yako, Na mwisho wa masomo kila mmoja atakuwa na maisha yake akipambana kivyake.

Fanya kile chenye manufaa kwako kwa sasa na kwa maisha yako ya baadae.
Sawa mkuu
 
Nipo njia panda mpaka sasa, mwakani namaliza chuo home hali sio nzuri, nawaza nikatafute mtaji chuoni kwa kujishughulisha na chochote kitu. Naomba ushauri wa biashara nzuri.

Mawazo yenu yana umuhimu.

Chuo: UDOM
Anza kukupesha kwa riba, lakini unatakiwa uwe katili
 
Nipo njia panda mpaka sasa, mwakani namaliza chuo home hali sio nzuri, nawaza nikatafute mtaji chuoni kwa kujishughulisha na chochote kitu. Naomba ushauri wa biashara nzuri.

Mawazo yenu yana umuhimu.

Chuo: UDOM
2016-2019 nimeuza nguo, viatu na marashi.
Mwishoni niliongeza udalali.
 
Kumekua na maswali mengi saana ya namna hii , unakuta mtu anakwambia labda ni mtaji kiasi Fulani nikafanye biashara Gani au Nina Elekea kuimaliza chuo/Niko likizo nikafanye kazi Gani huo muda ambao ntakua free!!!

Sasa Leo ngoja niseme kitu kimoja baishara ni kama Hobby ya mtu na mtu ( Ukifanya kitu unachokipenda au biashara unayoipenda) pia lenga Na Kipengele kimoja "KUTOA HUDUMA KWA JAMII" ( yaani biashara yako isiwe tu kwa ajili ya faida)

Nazani Ukitaka kuanzisha baishara utakuwa unavitu viwili mezani
-mapenzi ya biashara(hobby) + Kutoa Huduma hivyo vitu Kamwe havimtupi mtu na vinaongeza Ubunifu kwenye Biashara maana tayari unafanya kitu unachokipenda

NB: Kwa upande wangu Mimi Huwa naamini hivi Sio Binadamu wote tuwe wafanyabiashara, wengine wanamikono(nyota/hobby) ya kilimo,ufugaji Ufundi, technology, Tiba, Hivi vitu ukizingatia Kisha Ukajitafuta( find urserf) ni Watu unafiti nazani Utafanikiwa saana na mfano mzuri Huwa ninawaambia watu Kila siku sio alochokofanya mtu Fulani na wewe Ukifanya Utafanikiwa tunapishana kwenye Mapenzi ya kufanya vitu(hobby) plus Nyota

Sent from my CPH1989 using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…