Makirita Amani
JF-Expert Member
- Jun 6, 2012
- 1,915
- 3,422
Ajira sio salama tena kama ilivyokuwa zamani. Kwa sasa maisha yamekuwa ghali huku kipato cha ajira kikiwa hakitoshelezi. Hii inawafanya waajiriwa wengi kufikiria kuingia kwenye biashara.
Lakini pia kuingia kwenye biashara sio rahisi kama ambavyo mtu anaweza kuona. Kuna changamoto zake nyingi na kama ndio unatokea kwenye ajira huku ukiwa na mahitaji makubwa ya fedha, sio rahisi kuacha ajira na kuingia kwenye biashara moja kwa moja.
Kushindwa kuingia kwenye biashara moja kwa moja sio mwisho wa wewe kufanya biashara. Inawezekana kabisa ukawa na biashara huku unaendelea na kazi yako unayofanya sasa.
Leo kwenye mtandao huu wa NAPENDA BIASHARA utajifunza biashara tano unazoweza kufanya wakati bado unaendelea na ajira yako.
Kama unataka kufanya biashara ya aina hii jifunze kwanza kwa undani kwa kujisomea wewe binafsi kisha chagua kampuni unayoweza kufanya nayo na jiunge ili uanze kujenga biashara yako. Uzuri wa biashara hii ni kwamba kwa sehemu kubwa utafundishwa mbinu za kuweza kuendesha biashara yoyote.
Kama unataka kufanya biashara hii, chagua watoto wa aina gani unataka kufundisha, kisha angalia katika watu unaowafahamu ni wangapi wenye watoto wanaoweza kufaidi huduma zako. Tafuta wachache wa kuanza nao hata kwa gharama za chini, fanya nao kazi vizuri na kama watafurahia waombe wazazi wao wakutambulishe kwa marafiki zao ambao wanaweza kufaidika na huduma unayotoa.
Kama unataka kuingia kwenye biashara hii ya kutoa ushauri wa kitaalamu, jua ule utaalamu ambao unao, kisha angalia ni watu gani wanaweza kunufaika na ushauri wako kisha tafuta wachache wa kuanza nao. Endelea kutoa huduma hii ya ushauri ukilenga kujenga jina na baadae unaweza kutoza gharama au kuongeza gharama kama ulianza na kidogo.
Kama unataka kuingia kwenye biashara hii ya huduma za kitaalamu, jua ile huduma ambayo unaweza kutoa na anza na wateja ambao hawajafikiwa na watoa huduma waliopo. Tengeneza jina lako kwa kutoa huduma nzuri na kuza biashara yako kuanzia hapo.
Biashara hizi tano tulizojadili hapa unaweza kuanza leo hata kama huna fedha mfukoni. Kazi kubwa kwako ni kuanza na kutafuta mteja. Na uzuri ni kwamba popote ulipo umezungukwa na wateja, sema wengi hawajui kama huduma fulani inapatikana.
Kwa ushauri zaidi kuhusu kuanzisha na kukuza biashara yako piga simu 0713 666 445.
Kupata kitabu SIRI 12 ZA KUPATA WAZO BORA LA BIASHARA, wasiliana nami na utatumiwa kitabu.
PENDA BIASHARA, JIFUNZE BIASHARA.
Lakini pia kuingia kwenye biashara sio rahisi kama ambavyo mtu anaweza kuona. Kuna changamoto zake nyingi na kama ndio unatokea kwenye ajira huku ukiwa na mahitaji makubwa ya fedha, sio rahisi kuacha ajira na kuingia kwenye biashara moja kwa moja.
Kushindwa kuingia kwenye biashara moja kwa moja sio mwisho wa wewe kufanya biashara. Inawezekana kabisa ukawa na biashara huku unaendelea na kazi yako unayofanya sasa.
Leo kwenye mtandao huu wa NAPENDA BIASHARA utajifunza biashara tano unazoweza kufanya wakati bado unaendelea na ajira yako.
- Biashara ya mtandao(network marketing).
Kama unataka kufanya biashara ya aina hii jifunze kwanza kwa undani kwa kujisomea wewe binafsi kisha chagua kampuni unayoweza kufanya nayo na jiunge ili uanze kujenga biashara yako. Uzuri wa biashara hii ni kwamba kwa sehemu kubwa utafundishwa mbinu za kuweza kuendesha biashara yoyote.
- Kuwa mkufunzi binafsi.
Kama unataka kufanya biashara hii, chagua watoto wa aina gani unataka kufundisha, kisha angalia katika watu unaowafahamu ni wangapi wenye watoto wanaoweza kufaidi huduma zako. Tafuta wachache wa kuanza nao hata kwa gharama za chini, fanya nao kazi vizuri na kama watafurahia waombe wazazi wao wakutambulishe kwa marafiki zao ambao wanaweza kufaidika na huduma unayotoa.
- Ushauri wa kitaalamu.
Kama unataka kuingia kwenye biashara hii ya kutoa ushauri wa kitaalamu, jua ule utaalamu ambao unao, kisha angalia ni watu gani wanaweza kunufaika na ushauri wako kisha tafuta wachache wa kuanza nao. Endelea kutoa huduma hii ya ushauri ukilenga kujenga jina na baadae unaweza kutoza gharama au kuongeza gharama kama ulianza na kidogo.
- Huduma za kitaalamu.
Kama unataka kuingia kwenye biashara hii ya huduma za kitaalamu, jua ile huduma ambayo unaweza kutoa na anza na wateja ambao hawajafikiwa na watoa huduma waliopo. Tengeneza jina lako kwa kutoa huduma nzuri na kuza biashara yako kuanzia hapo.
- Anzisha na endesha blog.
Biashara hizi tano tulizojadili hapa unaweza kuanza leo hata kama huna fedha mfukoni. Kazi kubwa kwako ni kuanza na kutafuta mteja. Na uzuri ni kwamba popote ulipo umezungukwa na wateja, sema wengi hawajui kama huduma fulani inapatikana.
Kwa ushauri zaidi kuhusu kuanzisha na kukuza biashara yako piga simu 0713 666 445.
Kupata kitabu SIRI 12 ZA KUPATA WAZO BORA LA BIASHARA, wasiliana nami na utatumiwa kitabu.
PENDA BIASHARA, JIFUNZE BIASHARA.