Biashara ya Bia mpya

Biashara ya Bia mpya

Mzee wa Nyayo

Member
Joined
Jul 8, 2015
Posts
5
Reaction score
1
Nataka kuanzisha biashara ya kupika bia. Kwa miaka 2 hivi nimepika na kuwauzia rafiki na majirani huku nyumbani, nao wanasema bia ninayofanya ni nzuri na yenye ladha bora.

Nimetayarisha matangazo ya hiyo bia mpya ambayo mnaweza kuona (nimeambatisha kama attachementi). Lakini sasa nimepata tatizo ambalo ningependa kupata shauri niweze kulisuluhisha.

Wiki iliyopita nilienda Benki nipate mkopo wa kuanzisha kampuni ndogo. Wakaniuliza nimefikia hatua gani mwenyewe, nami nikawaonyesha hayo matangazo ya bia niliyofanya, nao wakanikataa kabisa wakisema bado sijastahili mkopo.

Jamani nifanyeje, wengi wanasema ni bia bora na tamu.

Nashukuru kwa madokezo yanayofaa
 

Attachments

  • Matangazo.jpg
    Matangazo.jpg
    40.7 KB · Views: 1,549
Asante sana, lakini nakaa mbali na rombo basi vipi gharama ya usafirishaji? Tena niliomba dokezo jinsi ya kupata mkopo wa kuanzisha kampuni ndogo. Wateja tayari wapo.

Kule jinsi wanavyopenda ulevi hakika hutakosa wazamini mikopo nje nje
 
Siamini kama uko serious..hasa ukizingatia hilo tangazo..
Kwani nguruwe ana nguvu sana,au hujawahi kumuona?
 
Nguruwe ana kelele mingi kama Nape hana nguvu yoyote!
 
Duh ilo jina sasa,hata ungenikuta mimi nisingekupa mkopo unaonyesha hauko serious kabisa.
 
jina limekuua vibaya halina mvuto...
em cheki hapa...
kilimanjaro
serengeti lager
safari lager
castle lager
tusker lager
pilsner
ndovu
tusker lite
castle lite
guiness
sasa we unaleta gujina gubaya, mhhhhh
hivi hata wale wala nguruwe hawesemi tumekula nguruwe wanasema kitimoto......
nguruwe ni mchafu tuuuuuuuuuu.... badili jina hilo uwezeshwe.....
 
jina limekuua vibaya halina mvuto...
em cheki hapa...
kilimanjaro
serengeti lager
safari lager
castle lager
tusker lager
pilsner
ndovu
tusker lite
castle lite
guiness
sasa we unaleta gujina gubaya, mhhhhh
hivi hata wale wala nguruwe hawesemi tumekula nguruwe wanasema kitimoto......
nguruwe ni mchafu tuuuuuuuuuu.... badili jina hilo uwezeshwe.....

Nimeisha fikiria majina mengi lakini yale kwenye orodha yako tayari yamechukuliwa. Hata simba na chui haiwezekani kwani zipo tayari. Labda fisi ila mimi mwenyewe simpendi. Vipi nikiweka Kitimoto Extra Lager?
 
Nguruwe ana kelele mingi kama Nape hana nguvu yoyote!

Siamini kama uko serious..hasa ukizingatia hilo tangazo..
Kwani nguruwe ana nguvu sana,au hujawahi kumuona?

Anayo nguvu. Watu wanamfuga hapo. Mwaka jana mmoja aligonga fensi naye akaendelea hivyo hadi ikabomoka naye akatoroka shambani huku akiwashambulia wakulima. Basi kwa hayo yaliyotokea naona ana nguvu.
 
Nimeshuka moyo kabisa kwani wengi wamenisema vibaya juu ya jina la bia. Basi nimebadilisha tangazo. Wiki ijayo nitaenda benki tena kuomba mkopo.
 

Attachments

  • Matangazo 2.jpg
    Matangazo 2.jpg
    69.6 KB · Views: 169
acha hlo hlo la kitimoto mimi nitakua mteja wako ila iwe kali kama mkomboji
 
Nimeshuka moyo kabisa kwani wengi wamenisema vibaya juu ya jina la bia. Basi nimebadilisha tangazo. Wiki ijayo nitaenda benki tena kuomba mkopo.
mkuu kama uko serious kwanini usiombe wadau wakusaidie kutafuta majina kwa ajili ya kilevi chako?

mfano

Kaskazini extra lager

Tamtam ice..

Kionjo beer
 
mkuu kama uko serious kwanini usiombe wadau wakusaidie kutafuta majina kwa ajili ya kilevi chako?

mfano

Kaskazini extra lager

Tamtam ice..

Kionjo beer

Huyu jamaa utani mwingi, hata hajamaanisha kaz anatania tu
 
Back
Top Bottom