Biashara ya bolt na nut

Biashara ya bolt na nut

Patroman

JF-Expert Member
Joined
Nov 12, 2018
Posts
809
Reaction score
1,222
habari? Kama kuna mtu ana ufahamu mzuri wa biashara tajwa hapo juu, nahitaji mchango wake , naipenda sana hii biashara tatizo siijui undani wake.
 
habari? Kama kuna mtu ana ufahamu mzuri wa biashara tajwa hapo juu, nahitaji mchango wake , naipenda sana hii biashara tatizo siijui undani wake.
Biashara nzuri sana na faida/margin kubwa sana changamoto yake kubwa kupata site ya kuweza kupata mauzo ya kutosha ili kukidhi gharama zako kwa muda stahiki.
Mfano tu wa gharama zako kwa mwezi, mshahara wenu, pango, kodi viwe sh 300,000=
kuuilima hiyo unahitaji mauzo ya sh 900,000= tu sababu 33% faida kwa bolt na nuts inawezekana sana TAABU ni hapo kupata hayo mauzo

Ndiyo maana hiyo biashara haiwezi jitegemea dukani inabidi kujumuika na bidhaa zingine kama Spare parts au Hardware kama nyongeza.

Margin za baadhi ya biashara kwa uzoefu wangu:
1. Bolt and Nuts 25% to 100% 2. Tools, Fixes Hardware 15% to 30% 3. Car Spare Parts 15% to 30% 4. Building Materials 10% to 15% 5. Whole sale merchandise 2% to 5%
Lakini hizo data inategemea sana na eneo lako la biashara na site ilivyokaa.
 
habari? Kama kuna mtu ana ufahamu mzuri wa biashara tajwa hapo juu, nahitaji mchango wake , naipenda sana hii biashara tatizo siijui undani wake.
Mkuu kwa ushaur wangu Mimi uza duka la spares mchanganyiko na usiuze bolts & nuts peke yake.
Ingawa wapo watu wanafanya hyo biashara na inawalipa lkn shida Ni kwamba inachukua muda mrefu sana kuupata umaarufu ktk mji husika.
Kuna vitu vingi vidogo vidogo tu vya kuuza na kukupatia faida.
Mfano: Bearings,Oil seals, bolts,nuts,snap rings,engine & gearbox oils,spanners,bushes.
Hivi ndio vitu vinanunuliwa mara kwa mara so hizo bolts/nuts unaongezea tu dukani Kama akiba.
Kwa sababu bolts/nuts hadi ikatike au ifunguke na kupotea inachukua muda nrefu sana,labda duka lako liwe limezungukwa na viwanda ndio angalau kutakuwa na mzunguko.
 
Biashara nzuri sana na faida/margin kubwa sana changamoto yake kubwa kupata site ya kuweza kupata mauzo ya kutosha ili kukidhi gharama zako kwa muda stahiki.
Mfano tu wa gharama zako kwa mwezi, mshahara wenu, pango, kodi viwe sh 300,000=
kuuilima hiyo unahitaji mauzo ya sh 900,000= tu sababu 33% faida kwa bolt na nuts inawezekana sana TAABU ni hapo kupata hayo mauzo

Ndiyo maana hiyo biashara haiwezi jitegemea dukani inabidi kujumuika na bidhaa zingine kama Spare parts au Hardware kama nyongeza.

Margin za baadhi ya biashara kwa uzoefu wangu:
1. Bolt and Nuts 25% to 100% 2. Tools, Fixes Hardware 15% to 30% 3. Car Spare Parts 15% to 30% 4. Building Materials 10% to 15% 5. Whole sale merchandise 2% to 5%
Lakini hizo data inategemea sana na eneo lako la biashara na site ilivyokaa.
hapana mi nimeshaona duka la bols, nuts, washers etc wanauza sana sana kozi wako peke yao hapo mkoani
 
hapana mi nimeshaona duka la bols, nuts, washers etc wanauza sana sana kozi wako peke yao hapo mkoani
Wapo wanaouza na kupata faida hatukatai lkn sio rahisi kihivyo Kama unavyofikiria.
Hao unaowaona wanauza hizo bolts and nuts hawakuanzia kwenye kuuza bolts and nuts nuts ghafla but unakuta mtu Kama huyo tayari ana hardwares zingine zinamuingizia kipato na badae anagundua kwamba Kuna watu wengi wanakuja kuulizia bolts lkn nafasi ya kwenye hardware yake haitoshi kujaza bolts and nuts nyingi kutokana na wingi wa bidhaa alizonazo na ndipo anaamua kuanzisha branch nyingine kwa ajili ya bolts and nuts.
Lakini sio kwamba mwanzoni kabisa ndio alianza ghafla na kuuza bolts and nuts halaf akae siku nzima auze bolts tatu Sasa atalipaje kodi ya jengo kila mwezi.
 
Binafsi naunga mkono hoja ya kuchanganya na spare nyingine
Naomba kujuzwa; Hizo bolt and nuts zinapatikana wapi kwa Jumla?
 
Binafsi naunga mkono hoja ya kuchanganya na spare nyingine
Naomba kujuzwa; Hizo bolt and nuts zinapatikana wapi kwa Jumla?
Inategemea na mkoa mkuu, kwa dar maeneo mengi wanauza hizo bolt na nut kwa bei ya jumla, Arusha yapo pia maduka, according to my experience, zinapimwa kwa kg. Tusubiri michango mingine
 
Inategemea na mkoa mkuu, kwa dar maeneo mengi wanauza hizo bolt na nut kwa bei ya jumla, Arusha yapo pia maduka, according to my experience, zinapimwa kwa kg. Tusubiri michango mingine
ok asante
naomba kujua maduka kwa Dar
 
ok asante
naomba kujua maduka kwa Dar
Sijajua ule mtaa wanauitaje ila ni nyuma ya jengo la kariakoo shimoni, soko la nje, mtaa unaoelekea kwenye maduka yanayouza spea za pikipiki, frem za mwanzo ukivuka duka la spea za SUNMOTO wanauza bolt na nut kwa jumla.
 
Sijajua ule mtaa wanauitaje ila ni nyuma ya jengo la kariakoo shimoni, soko la nje, mtaa unaoelekea kwenye maduka yanayouza spea za pikipiki, frem za mwanzo ukivuka duka la spea za SUNMOTO wanauza bolt na nut kwa jumla.
Mkuu unamaanisha huu mtaa wanakopaki magari ya masaki au yanapoingilia magari ya makumbusho na kawe?
 
Mkuu kwa ushaur wangu Mimi uza duka la spares mchanganyiko na usiuze bolts & nuts peke yake.
Ingawa wapo watu wanafanya hyo biashara na inawalipa lkn shida Ni kwamba inachukua muda mrefu sana kuupata umaarufu ktk mji husika.
Kuna vitu vingi vidogo vidogo tu vya kuuza na kukupatia faida.
Mfano: Bearings,Oil seals, bolts,nuts,snap rings,engine & gearbox oils,spanners,bushes.
Hivi ndio vitu vinanunuliwa mara kwa mara so hizo bolts/nuts unaongezea tu dukani Kama akiba.
Kwa sababu bolts/nuts hadi ikatike au ifunguke na kupotea inachukua muda nrefu sana,labda duka lako liwe limezungukwa na viwanda ndio angalau kutakuwa na mzunguko.
Mkuu kwa makadirio mtaji kiasi gani unahitajika
 
Mkuu kwa makadirio mtaji kiasi gani unahitajika
Kiukweli hakuna mtaji maalum coz Kuna levels nyingi sana so inategemea unataka uanze biashara ya viwango gani.
Ila kwa ushaur wangu Mimi ili biashara isikuumize kichwa uwe na angalau milioni 15 kwa kuanzia then baada ya hapo unaongezea polepole
 
Dar boss hii biashara si mpaka uwe fundi
sio lazima uwe fundi, ila lazima uwe karibu na mafundi, mi nauza ingawa nimechanganya na biashara nyingine ila nina mafundi. Kwa wanaouza bolt na nut kwa jumla wao hawaitaji kabisa mafundi.
 
Back
Top Bottom