Habari za mchana wana jamvi.
Naomba ushauri kuhusiara na biashara niliyotaja hapo juu.
Mimi ni mtaalamu wa mambo ya saikolojia, tuna ofisi yetu na mwenzangu, tumekuwa tukifanya biashara ya kutoa ushauri ila tunaona kama vile hailipi. Sasa tunataka tuwe tunatoa mihadhara kwa kiingilio yaani tunaandaa mada ya kuiwasilisha
tunatoa matangazo, siku, saa na mahali seminar itakapofanyika naomba ushauri mwenye uzoefu tafadhali.