Biashara ya dagaa

Biashara ya dagaa ina hela ila ukiifanya vizur mkuu nisha hustle sana na hii biashara lakin naamin itanipa hela tu . Nisha tapeliwa na watu wa kisiwan nishatapeliwa na watu wa sokon nishapata hasara lakin siichok na soon nataka nirud na mkakati mpya wakisasa kwenye hii biashara
 
Pole
 

Umeelezea yaliyokusibu pole,mpe muongozo mleta mada.
 
Pole sana mkuu, unafikiri
Ni wapi ulikosea ili wemgine wapate kujifunza?
 
Kuna yule mdada yuko twitter (X) maarufu kwa kuuza dagaa na samaki kutoka Mwanza unaweza kumcheki pia anajiita TricyLove anaweza kukupa 1 na 2 ya hiyo biashara
 
Biashara ya Dagaa haina bei fixed(wakati wa kununua), huo ndo ukweli.

Bei yake inabadirika kwa kila Giza( Hiki ni kipindi ambacho uvuvi wa Dagaa ufanyika ndani ya kila mwezi,, simply ni kipindi ambacho kunakuwepo na giza kabla ya mbalamwezi kuanza kuchomoza).

Pia kwenye Giza hilo hilo, bado bei ya kununulia ubadirika siku kwa siku, kutokana na upatikanaji wa Dagaa yenyewe ulivyo.

Hapo nimezungumzia udhoefu wa upatikanaji wa Dagaa(kununua) kutoka huko visiwani.
 
Mfano katika kipindi hiki,, bei kidogo ipo juu maana mvua zinanyesha sana huko visiwani, kwahiyo Kuna uhaba wa jua( Nishati inayotumika kukausha Dagaa).

Dumu linauzwa hadi Shilling 24000/=.

Gunia linakuwa na ujazo wa Dumu 20 au 10.

Uzito wake waweza kuwa Kg 80 kwa gunia lenye ujazo wa dumu 20 na Kg 40 kwa gunia la dumu 10.
 
Oh Asante bro ni miezi gani huko kisiwani mvua zinakata
 
Oh Asante bro ni miezi gani huko kisiwani mvua zinakata
Kwa experience ya visiwa vya Bukoba mvua zinaweza nyesha kwa huu mwezi wa 9 na 10 pia.

Lakini nachoweza kukushauri ni kwamba ingia mzigoni mkuu upige kazi,, kwenye icho kipindi cha mvua,, mzigo unaweza kuwa changamoto kukusanya lkn uzuri ni kwamba ukiupata, sokoni pia utauza kwa bei nzuri sana.
 
Nauli ya kutoka mwanza mpaka kwenye hicho kisiwa bukoba ni kiasi gani

Nataka nikatafute connection kule au nimpeleke mtu awe ananitumia mzigo mi nausambaza
 
Nauli ya kutoka mwanza mpaka kwenye hicho kisiwa bukoba ni kiasi gani

Nataka nikatafute connection kule au nimpeleke mtu awe ananitumia mzigo mi nausambaza
Inategemea sasa ndg unataka kwenda kisiwa cha wapi..

Binafsi,, nina taarifa na kisiwa kimoja kinachoitwa MULUMO, kutoka mwanza mpaka hapo kuna wastani wa Shilling 25000.
 
mkuu kisiwa cha GOZIBA ushafika? Nimeshauriwa nitulie mpaka mvua zikate kwanza kwasababu sasa hivi bei ya dagaa ipo juu itanisumbua kupata mteja sokoni hii ni kweli mkuu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…