Biashara ya Duka la Rejareja: Ushauri, Mchanganuo, Changamoto na Namna ya Kutunza Kumbukumbu

kebi

Member
Joined
Jan 13, 2012
Posts
19
Reaction score
5

Naomba kufahamishwa kwa mwenye kujua duka la rejareja la kuuza mchele, juice na kadhalika linaweza kuitaji mtaji kiasi gani

Ibravo post:
Habari zenu Wana JamiiForums,

Mimi ni mwanafunzi wa chuo mwaka wa tatu,katika harakati za kujiandaa na kupambana na maisha pindi nitakapohitimu elimu yangu na kurudi mtaani, nimetafuta pesa ikiwa kama mtaji wa biashara milioni moja (1,000,000)hasa ya duka la bidhaa za vyakula.

Tatizo ni kwamba si mzoefu katika biashara na ni mara ya kwanza kutaka kuifanya hii biashara kwan matarajio yangu ni kujiajiri mwenyewe.

Naomba ushauri kwa yeyote mwenye uelewa kuhusu hili kunipa mchanganuo wa bidhaa muhimu zinazotakiwa kuwepo dukani kama vile unga kiasi gani,mchele n.k kulingana na mtaji huo wa Milioni Moja.

Natanguliza Shukrani zangu.

BAADHI YA MASWALI YA WADAU WENGINE KUHUSU BIASHARA HII
Mi ni kijana umri miaka 23 nina aidia ya kufungua duka la vyakula rejareja maeneo ya kigambon ila sina uzoefu na biashara na nikiazio kipi cha mkwanja wa kuazia hadi sasa nina 60,0000.

NAOMBA MSAADA KWA WENYE UZOEFU NA BIASHARA.
Habari wanaJF,

Naomba kujua kutoka kwa wazoefu na wajuvi wa mambo hayaaa. Nahitaji kujua namna ya kurekod/ kutrak/kufuatilia au kujua faida na hasara katika duka la rejareja hasa unapokuwa na wateja wengi.

Asanteni


MAONI MBALIMBALI KUHUSU BIASHARA HII


 
Inategemea na unataka kuweka vitu kiasi gani!ila kwa kuanzia milion 2 au 3 inatosha kabisa.
 
naomba kufahamishwa kwa mwenye kujua duka la rejareja la kuuza mchele, juice na kadhalika linaweza kuitaji mtaji kiasi gani

Mkuu majibu mengine ni simple sana, fanya hivi.

Chukua kalamu na Note book then neda kariakaoo na kwingineko tembelea maduka ya jumla chukua bei theni ukukaa chini ukipiga mahesabu utapata kila kitu.

Mkuu ili ufanikiwe katika biashara unatakiwa kuumiza kichwa sana, inatakiwa akili ifanye kazi mara 6 zaidi ya uwezo wake wa kawaida, fanya tafiti mwenyewe mkuu.
 
Ukifanya business plan yako itakupa jibu sahihi kuliko kupoteza muda kwamba hapa tutakupa jibu sahihi kesho utakapoenda kutumia majibu ya hapa ukaona kama umedanganywa.
 
Mie nilimfungulia mama yangu kijijini kwenye frem ya ukubwa wa 3*3 mwanzo wa last year ilinicost jumla ya 3m, I mean niliweka kila kitu kinachostahili katika duka la rejareja.Nafikiri hiyo taarifa inaweza kukusaidia.
 
naomba kufahamishwa kwa mwenye kujua duka la rejareja la kuuza mchele, juice na kadhalika linaweza kuitaji mtaji kiasi gani

Mkuu mtaji alioanza nao Kimario sio lazima na masawe aanze nao huo huo. Halafu mahitaji na gharama yanabadilika kulingana na eneo ulilopo. Kwa mfano kama upo sehemu haina umeme unaweza ukaambulia ushauri uliojumuisha mpaka fridge ya umeme wakati kwako si mufaka.

Kama ungetaka ushauri halisi basi ungeweka data zote hadharani ili ushauriwe lakini kulingana na maelezo yako mimi ninakushauri uanze na hicho kiasi ulichonacho (kama unaeneo la kufanyia biashara), hivyo vitu vingine utaongeza taratibu baada ya kupata faida au fedha za ziada.
 
inategemea na unataka kuweka vitu kiasi gani!ila kwa kuanzia milion 2 au 3 inatosha kabisa.

Sasa Parachichi, hapa ndipo tunapokosea halafu tunalalamika kwamba biashara ni mbaya. Wewe hupasi kuwa na vitu vyako unavyotaka kuweka dukani. Wewe unapaswa kuwa msilikilizaji tu, na unalisikiliza soko linakwambia nini.
 
Mkuu kwani wewe ulikuwa na mtaji wa sh ngapi labda tuangalie ni vitu gani vya muhimu vya kuanzia hiyo biashara yako.
 
Salaam zenu wote! Naomba ushauri wenu kwa mwenye uzoefu wa aina hii ya biashara, je ni mtaji kiasi gani unafaa kuanzia, na faida iko je na jinsi ya kutunza kumbukumbu. Siku hizi ajira ndio hiziii.

Karibuni kwa ushauri.
 
Wakuu,

Natarajia kuwa na duka kwa mara ya kwanza, duka ni la bidhaa za matumizi nyumbani mfano chumvi, sukari, dawa ya meno n.k.

Kwakweli sijui namna bora ya kujua hesabu ya bidhaa zilizouzwa na zile zilizobaki dukani, ukizingatia nitaweka mfanyakazi.

Naomba wazoefu mnisaidie mambo ya kufanya ili angalau mahesabu ya bidhaa dukani yadhibitiwe vizuri.

Karibuni nyote na ahsanteni!
 
Unahitaji vitabu (nunua hata counter books) vya kumbukumbu za hesabu kama vile:

KITABU CHA MATUMIZI
KITABU CHA MANUNUZI, KITABU CHA MAUZO
KITABU CHA MADENI - kwa unaowadai na wanaokudai
KITABU CHA MALI YA BIASHARA, KITABU CHA STOCK.

Vilevile unahitaji kununua mafaili ya kutunzia stakabadhi za manunuzi, malipo, bank slips, mikataba, na nyinginezo ktk mpangilio kila moja na faili lake.

Pia unatakiwa kuwa na diary au note book kubwa kuandika bidhaa ambazo hautakuwa nazo wateja ambazo wateja wamehitaji (missing items) ili kukupa kumbukumbu za kuzinunua. Kitu kingine panga vitu ktk mpangilio mzuri usifanye duka ili mradi duka, panga vitu vinavyofanana kwa pamoja na usijaze items nyingi katik display kwa pamoja.

Kauli nzuri kwa wateja, uharaka, uhakika, ubora na hali ya kujali wateja ndo uchawi wako ktk biashara hii. Usisahau kufuga paka mdogo kufukuza panya. JINGINE MUHIMU, hakikisha kila siku asubuhi unapeleka mauzo ya jana yake benki kabla ya kuyatumia, pia usajili biashara yako na uifungulie akaunti ambayo itakuwa na jina la hiyo biashara (mfano MAJIGO RETAIL SHOP).
 
Ni biashara ngumu kidogo kuidhibiti mfano mfuko wa sukari kg 50 badala ya kutoa faida unaweza kukuletea hasara kubwa sana maana akiuza kg 3 na asiweke kwenye hesabu si rahisi kutambua hivyo basi ni vizuri ufahamu mtaji wako ni kiasi gani na ufanye mahesabu ya mali yote dukani mara nyingi uwezavyo kujua dhamani halisi ya duka lako.
 

Mkuu umekumbusha suala muhimu ila kufanya stock si mchezo, itabid angalau niwe nafanya kila baada ya wiki 1
Nashukuru sana!
 

Imekaa vizuri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…