Biashara ya kuanzia mtaji milion 200

Mkuu unaweza kutupa ABC za ufanyaji wa hii biashara.
Kuanzia namna ya kupata vibali na kuendelea
Nilikuwa na shamba la uridhi lenye heka 79 zenye hati, nikapewa wazo la kuonana na kampuni moja (property) nikaongea nao baada ya kupata taarifa wenye maeneo makubwa watanyang'anywa, wakanishauri kukata viwanja Kwa makubaliano maalumu, kila kitu watashughulikia wao ninachotakiwa kuwapa muda wa kufanya kazi, makubaliano ni baada ya mradi tutagawana % za viwanja ambao wao watachukua 30% nami 70% . Kila kitu kinachangamoto zake mradi niliambiwa utakamilika baada ya miezi sita lakini ukakamilika baada ya Mwaka, viwanja 89 ndiyo vilivyopata prove ya kuanza kuuzwa, vilivyosalia prove yake imetoka last month.
Sina process yoyote niliyofanya mwenyewe kila kitu walifanya wenyewe.
 
Mkuu nina interest sana na hilo eneo lakini naona kama soko gumu, hebu dadavua kidogo hizo ideas kama hutojali, tujiongeze. Ni haya mambo ya kupack korosho, kusaga unga etc? Hebu fafanua
Soko sio gumu mkuu ,inategemea na creative yako na stuffs utakao waajiri ,kwa mfano ukiamua kutengeneza snacks za 200tsh ukizifanyia marketing nzuri utapiga hela tuu coz biashara yako ni cheap na ndio biashara zinazofanya vizuri sokoni kwakuwa watz wengi ni price sensitive sana ,au kwenye kutengeneza vijuice vya watoto ambavyo ni nya bei rahisi kama kuna kampuni moja ina vijuice vya sh100 na 200 wanauza sana mkuu juice zao zinatafutwa kama madini na hao jamaa hata hawajui marketing vizuri ..Tafakari mkuu ukiwa interested nichek nitakusaidia hapa na pale .
 
Mkuu unaweza kutupa ABC za ufanyaji wa hii biashara.
Kuanzia namna ya kupata vibali na kuendelea
Katika kuuza pia sikuhangaika Sana kuna baadhi ya kampuni zilihitaji viwanja 50 za ukubwa tofauti, Mimi nilipanga kila sqm nitauza Kwa 18000/= lakini kutokana na Hali ya uchumi nilipata Wateja wanne tuu waliochukua Kwa bei hiyo, nikaona nachelewa nikafanya majadiliano na hiyo kampuni wakachukua hivyo viwanja Kwa mkataba wa kunilipa kila baada ya miezi mitatu ndani ya miaka 2, na nikawauzia sqm 1= 10,000/= Kwa sasa tayari nina miezi sita napokea hiyo pesa bila usumbufu. Sijauza vyote nimebakiza vichache vya familia yangu huko mbele Mungu akinijalia kuipata.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…