Biashara ya kuchimba mawe ya gypsum

Biashara ya kuchimba mawe ya gypsum

Habari
Naomba kufahamu anayeijua biashara ya kuchimba mawe ya gypsum. Kwa maeneo ya kilwa au makanya. Gharama Hadi kiwandani ni kiasi gani, na faida ni kiasi gani

Nawasilisha
Huwa naona sana maeneo ya kilanjelanje wanapanga mawe kwenye malori..ngoja waje kutupa muongozo.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari
Naomba kufahamu anayeijua biashara ya kuchimba mawe ya gypsum. Kwa maeneo ya kilwa au makanya. Gharama Hadi kiwandani ni kiasi gani, na faida ni kiasi gani

Nawasilisha
Hapo ni kilwa katika majimbo ya Gypsum, picture hiyo ni yangu nilipiga mwaka2019.
Kama unahitaji kuwekeza kwenye gypsum karibu kwa full and complete analysis kuanzia kupata eneo Hadi kuchimba na kupeleka kiwandani kuuza.
IMG_20190214_112300.jpg
 
Habari
Naomba kufahamu anayeijua biashara ya kuchimba mawe ya gypsum. Kwa maeneo ya kilwa au makanya. Gharama Hadi kiwandani ni kiasi gani, na faida ni kiasi gani

Nawasilisha
Karibu ndgu brown.
Mimi nina kitalu cha kuchimba gypsum stone na gypsum powder maeneo ya Bendera Mkomazi njia baada ya Bwiko ukiwa unatoka Dar.
Tunatoa gypsum stone na powder ambayo ni sulphate ake ni almost 80%
Gharama za kusafirisha mzigo toka hapo kwenye kitalu ni almost 1,150,000 hadi 1,200,000 kwa gari ya tonne 30 kupeleka hadi viwanda vya gypsum au vya cement vya dar maeneo ya mbagala kwa mbele nadhani ni kivule kule kwenye viwanda vya Dangote na Camel. Mara nyingi tumekuwa tukiwauzia wafanyabiashara na huleleka Dar, kitalu kimesajiliwa na kuna kijiko maalumu kwa ajili ya kuchimba na kukusanya mzigo.
Nakushauri kama unataka magari ya uhakika kukusafirishia mzigo na kwa guaranteed katika biashara yako tumia magari za moshi au himo kwenye kampuni sio kudandia njiani, mfano KANAAN TRANSIT, na nyingine za moshi.. maana ni rahisi upatikanaji wake otherwise wawe booked ila wana magari mengi.
Kingine unaweza kutumia madalali ambao mara nyingi wapo hapo MAKANYA mzani au Kwa Bon wana uzoefu wa kujuana na madereva wengi wa malori, pia HEDARU kuna madalali unaweza watumia ila changamoto za madalali kazi zao ni za kubahatisha bahatisha anaweza akapewa kazi na dereva yuko boda ya namanga akasubirisha, dereva akifika arusha anakutana na kazi imeiva hawezi kuiacha pesa anabeba anakukatia vumbi.
Ni hayo tu kama unahitaji biashara ya Gypsum stone and gypsum powder tafadhari nipigie kwenye namba hii chap tuyajenge
+255 712 36 33 58.

Karibu sana mkuu, hata kwa ushauri zaidi maana tumebobea kwenye gypsum raw materials.

AmockView attachment 2190703
images%20-%202022-02-27T172255.109.jpg
 
Hapo ni kilwa katika majimbo ya Gypsum, picture hiyo ni yangu nilipiga mwaka2019.
Kama unahitaji kuwekeza kwenye gypsum karibu kwa full and complete analysis kuanzia kupata eneo Hadi kuchimba na kupeleka kiwandani kuuza.
View attachment 2189658
Hii biashara imekaaje..kwa upande wa investment na return on investment.

#MaendeleoHayanaChama
 
Hii biashara imekaaje..kwa upande wa investment na return on investment.

#MaendeleoHayanaChama
Ipo vizuri Sana Ila inahitaji capital kubwa Sana maana viwanda vingi vinahitaji supplying then wakulipe. Unahitaji uwe na excavator, gari za kusafirishia mizigo Hadi viwandani, compressor kwa ajiri ya blasting drilling na pia miripuko then kazi. Return ni zuri. Kama huna leseni huwa zinakodishwa huko kwa muda na unachimba. Kwanza tafuta mtaji, Kisha tafuta eneo baada ya hapo tafuta tenda kazi inaendelea. Hayana hasara ili mradi namna ya uchimbaji uwe vizuri ili production cost iwe economic.
 
Ipo vizuri Sana Ila inahitaji capital kubwa Sana maana viwanda vingi vinahitaji supplying then wakulipe. Unahitaji uwe na excavator, gari za kusafirishia mizigo Hadi viwandani, compressor kwa ajiri ya blasting drilling na pia miripuko then kazi. Return ni zuri. Kama huna leseni huwa zinakodishwa huko kwa muda na unachimba. Kwanza tafuta mtaji, Kisha tafuta eneo baada ya hapo tafuta tenda kazi inaendelea. Hayana hasara ili mradi namna ya uchimbaji uwe vizuri ili production cost iwe economic.
Kuna mdau hapo juu amock ,amesema yeye anamiliki kitalu, sasa nafikiri hapa tujulishane gharama za kununua mzigo, na gharama za usafirishaji na viwanda vinavyonunua mzigo, na wananunua wa bei gani, ili tuangalie faida yake ipoje,
 
Kuna mdau hapo juu amock ,amesema yeye anamiliki kitalu, sasa nafikiri hapa tujulishane gharama za kununua mzigo, na gharama za usafirishaji na viwanda vinavyonunua mzigo, na wananunua wa bei gani, ili tuangalie faida yake ipoje,
Viwanda vyote vinavyotengeneza cement vinatumia gypsum, viwanda vyote vya kutengeneza gypsum board wanatumwa gypsum, viwanda vyote wanavyotengeneza gypsum powder wanatumia gypsum. Mkuu issue siyo kujua Nani anatumia. Issue ni kupata tenda huko. Bei ya usafirishaji inategemea unatolea wapi. Maana same Moshi ipo, itigi singida ipo, hotel tatu na kilanjelanje kilwa pia zipo.
 
Habari
Naomba kufahamu anayeijua biashara ya kuchimba mawe ya gypsum. Kwa maeneo ya kilwa au makanya. Gharama Hadi kiwandani ni kiasi gani, na faida ni kiasi gani

Nawasilisha
Hello brown ulifanikiwa kupata data za kutosha juu ya biashara ya uwekezaji ktk Gypsum? Kama bado tuwasiliane. Nina vitalu makanya, bendera mkomazi na kilwa

Sent from my MRD-LX1F using JamiiForums mobile app
 
Hapo ni kilwa katika majimbo ya Gypsum, picture hiyo ni yangu nilipiga mwaka2019.
Kama unahitaji kuwekeza kwenye gypsum karibu kwa full and complete analysis kuanzia kupata eneo Hadi kuchimba na kupeleka kiwandani kuuza.
View attachment 2189658
Ruby naomba tuwasiliane, nina jambo langu la gypsum hapo kilwa. Nicheki kwenye 0712363358

Asante

Sent from my MRD-LX1F using JamiiForums mobile app
 
Viwanda vyote vinavyotengeneza cement vinatumia gypsum, viwanda vyote vya kutengeneza gypsum board wanatumwa gypsum, viwanda vyote wanavyotengeneza gypsum powder wanatumia gypsum. Mkuu issue siyo kujua Nani anatumia. Issue ni kupata tenda huko. Bei ya usafirishaji inategemea unatolea wapi. Maana same Moshi ipo, itigi singida ipo, hotel tatu na kilanjelanje kilwa pia zipo.
Ruby naomba tuwasiliane, nina jambo langu la gypsum kilwa. Nicheki 0712363358

Sent from my MRD-LX1F using JamiiForums mobile app
 
Biashara hio ni nzuri cha kwanza nenda kwenye kiwanda husika unakubaliana nao bei kua utawauzia gipsum stone kwa tani shiling ngapi

Na wao watakuambia wanahitaji tani ngap na watakulipa hela yako ukifikisha tani ngapi

Baada ya hapo unatafuta gari unakubaliana nao kua utawalipa ela yao mzigo wako, ukishapokelewa kiwandani na tani zako zile walizobeba ziwe azijapungua

Kwaio wenyegar utawalipa wew ukishalipwa. Pia ukatafute mzigo uwe na uhakika wakupata mzigo hata kama eneo huna utanunua jiwe kwa wenye mzigo ambao hawamudu garama za kusafirisha
Uwe na hela ya kibali maliasili hii sio ela nyingi

Pia uwe na hela ya wapakiaji
Cha mwisho uwe na mawasiliano mazur na wanaopokea mzigo wako kule kiwandan pindi ikitokea mzigo wako unahitilafu waweze kuupokea ili usipate hasara
Mim nime deal na ubebaji wa mizigo hio kwenye semi
Viwanda vya kupeleka inategemea

Kuna tanga cement ,kuna nyati dar kimbiji, kuna twiga hii ni dar wazo, kuna diamond cement hii ni dar vikindu

Machimbo ya mawe kuna bwiko na makanya hii ni same njia ya arusha

Pia kuna kiranjeranje hii ipo kilwa njia ya kwenda mtwara
 
Back
Top Bottom