Biashara ya mapambo kwenye masherehe,mikutano na n.k

Biashara ya mapambo kwenye masherehe,mikutano na n.k

sonofobia

JF-Expert Member
Joined
Jun 21, 2015
Posts
1,171
Reaction score
4,295
Kama unataka kutoka bila kutumia nguvu nyingi sana basi fanya hii biashara. Yani biashara ya kuandaa events kama za harusi za mtaani, maulidi, kipaimara, vigodoro, misiba nk.

Unachotakiwa ni kuwa na turubai kubwa la kupanga, viti vya kutosha,meza kadhaa,mikeka, masinia,sahani na mapambo kidogo utapiga hela kila siku hapa Dar es salaam."

Jamani haya maneno niliambiwa na bro mmoja juzi tukiwa tunabadilishana mawazo Barber shop sasa akunifafanulia vitu vingi alisema ndio biashara yake kajenga,kaninua gari mbili moja ya kutembelea na nyingine ya kubebea mizigo yake.

Ombi;
Naomba mwenye uelewa na hii biashara anipe mwanga inakuwaje mtaji kwa anaeanza ,masoko yake unapataje, risk zake zipoje, na faida yake unaitengezaje.

Nitashukuru sana wanajamiiforum
 
Nataka na mimi nianze kukodisha kwa watu kumbe mpaka sahani zinakodishwa nilikuwa sijui Dar hela ipo
 
inalipa ila uwe na marketing nzuri,watu wajue namna ya kukupata,uwe na ofisi,na pia saloon ya kuandaa mabibi harusi hapo deal nyingi za harusi hazichezi mbali.
 
wazo hili ungelifanyia kazi mwezi shaban mtaji ungekuwa umerudi. vingunguti kila cku kulikuwa na ndoa, kigodoro hamna kulala.
 
Watu walishaanza zamani, mitaji irisharudi wakapunguza na bei, walishazoewa na wateja, ubora wa upambaji ulisha ongezeka ukienda ww hupati ng'o.
 
Watu wengi wakijua na wakifanya haitalipa kama inavyolipa..... the higher the supply the lower the demand ...,
 
uwe na muziki wa uhakika na song za hatareeeeee....
 
Wewe umesema inalipa
wewe tena unaomba wenye kuijua wakueleze?
 
watu walishaanza zamani, mitaji irisharudi wakapunguza na bei, walishazoewa na wateja, ubora wa upambaji ulisha ongezeka ukienda ww hupati ng'o.

acha kumkatisha tamaa mwenzako. Inawezekana unaogopa ushindani tu.

Mdau fanya hiyo kitu inalipa sana. Itakulipa kwa kadri utakavyojituma, usilatikatishwe tamaa.
 
Inalipa... ishu kupata hizo tenda, inabidi uwe muhudhuriaji mzuri wa hizo mambo
 
Jambo linapokuwa mwanzo huwa tam sana lakini mabadiriko yanapo tokea hulifanya chungu
 
Uwe mcheza vigodoro, uwe mbeya sana na usiogope kumpa za uso anayekupa mnyanyasiko.
 
inalipa ila uwe na marketing nzuri,watu wajue namna ya kukupata,uwe na ofisi,na pia saloon ya kuandaa mabibi harusi hapo deal nyingi za harusi hazichezi mbali.

Asante sana kwa mawazo positive ..nitafanyia kazi
 
Mwenye kujua vizuri bihashara ya mapambo naomba anijuze nina mtaji wa milioni moja, ni mapambo katika sherehe na hafla mbali mbali. Tafadhali nawasilisha.

===========================================

Biashara ya mapambo inahitaji viti,meza,yale mashuka ya rangi mbali mbali,meza,tents etc....kimsingi milioni moja ni hela ya kununua viti vichache tu,ongeza ongeza iwe hata mil 4 urudi hapa tukuelekeze vizuri mkuu maila
 
Biashara ya mapambo inahitaji viti,meza,yale mashuka ya rangi mbali mbali,meza,tents etc....kimsingi milioni moja ni hela ya kununua viti vichache tu,ongeza ongeza iwe hata mil 4 urudi hapa tukuelekeze vizuri mkuu maila
 
Hii ni mojawapo ya shughuli ninazotaka kufanya
Ni biashara nzuri sana,normally costs nyingi ziko mwanzo wakati unaanza manake itakubidi kununua makorokoro kibao lkn ukishasettle unakula tu hela miguu juu kila wiki una uhakika wa laki 3 take home na kuendelea depending na ukubwa wa event.
 
Back
Top Bottom