Wana jf,mim ni mfanyabiashara mdogo,sasa hivi karibuni kuna ndg yangu kanipa deal ya kuuza matunda nje ya nchi hasa Dubai,naomba kwa wanaofahamu wanipe muongozo wa biashara hii na jinsi ninavyoweza kuyapata haya matunda kwa urahisi!matunda yenyewe ni Maembe,Machungwa,Mananasi na mengeneyo!!AHSANTENI!!
Mkuu nikukosoe kidogo, Ni kweli inaweza kuwa ngumu kusafirisha mazao ya vyakula, lakini hizo pande za dunia ulizotaja nyingi zao hata muhogo haumei, mara nyingi matunda na mazao mengi ya misosi wanatoa kutoka nchi tofauti za latin america na mengine spain, Africa pia tunapeleka sana mazao yetu huko kwa *THE YES PLEASE' sijui kama apo humu lakini wakulima wengi wanarusha mazao yao ulaya. kenya ndio usiseme, tani na tani ziainuka kila siku. Ila tu Ni kweli ugumu wake unakuja pale kwenye kukamilisha na kufuata sheria zao. kwa mtazamo wangu mimi, kama mtu anaweza kudili na huu usumbufu tunaoupata hapa nchini kwetu kwa kuendeleza taifa, basi hiyo ya ulaya haitomshinda kwa sababu kule usumbufu na maringo maofisini hakuna. angalau sio kama yalivyozidi hapa kwetuWazo lako ni zuri sana na kwa mtu anayetegemea maendeleo hii ni fursa.
Hatua ya kuamua kusafirisha matunda/chakula ktk nchi zilizoendelea ni suala la kisheria mkuu.
Nchi zilizoendelea zina sera za uzalishaji pamoja na viwango vyake katika imported ya chakula kama matunda.
Kule katika mataifa yaliyoendelea kuna baadhi ya inchi ambazo hazipokei chochote kutoka nje ya inchi .
Afrika kwa bahati mbaya tumekua ni bara ambalo nchi zilizoendelea huuza bidhaa zao ikiwemo matunda, ni mara chache sana sana kwa nchi zilizoendelea kuinported mzigo wa chakula kutoka nje,
Sikukatishi tamaa lakini ukweli ni kuwa sera za ulaya na magharibi ni kuuza bidhaa africa, sasa wakiruhusu africa kuuza chakula ulaya na mash-kati huoni soko lao litakufa ,maana africa hawatanunua tena na viongozi wa rasi ya eneo hilo hawatakubali kutokea kitu kama hicho.
Ni heri ungeangalia soko hapa karibu na nyumbani.
Mfano.Kenya,South africa,Zimbabwe na Ethiopia
Wazo lako ni zuri sana na kwa mtu anayetegemea maendeleo hii ni fursa.
Hatua ya kuamua kusafirisha matunda/chakula ktk nchi zilizoendelea ni suala la kisheria mkuu.
Nchi zilizoendelea zina sera za uzalishaji pamoja na viwango vyake katika imported ya chakula kama matunda.
Kule katika mataifa yaliyoendelea kuna baadhi ya inchi ambazo hazipokei chochote kutoka nje ya inchi.
Afrika kwa bahati mbaya tumekua ni bara ambalo nchi zilizoendelea huuza bidhaa zao ikiwemo matunda, ni mara chache sana sana kwa nchi zilizoendelea kuinported mzigo wa chakula kutoka nje,
Sikukatishi tamaa lakini ukweli ni kuwa sera za ulaya na magharibi ni kuuza bidhaa africa, sasa wakiruhusu africa kuuza chakula ulaya na mash-kati huoni soko lao litakufa ,maana africa hawatanunua tena na viongozi wa rasi ya eneo hilo hawatakubali kutokea kitu kama hicho.
Ni heri ungeangalia soko hapa karibu na nyumbani.
Mfano.Kenya,South africa,Zimbabwe na Ethiopia
si kweli matunda na vyakula kama ndizi ambazo viko marekan vinatoka uganda na jamaica. tatizo la watanzania atuchangamkii fursa.
majiran zetu kenya na uganda wanachangamkia. Africa atuwez kuuza nje electronics au magari kwa vile atutengenez lakin chakula kama matunda tunaweza.
Kuna kitu kinaitwa AGOA watz wengi awajui hiyo ilianzishwa na marekan kusaidia wafanyabiashara ndogo ndogo watokao nchi masikin kama Africa kuuza bidhaa zao marekan bila kukatwa kodi.
mim uwa nawaona wakenya, waganda, na wengine wakitumia fursa hiyo watanzania tunatishana pia hakuna elimu nzuri kujua bidhaa gani zina soko ulaya, marekani na uarabuni.
pia watanzania ni waoga wa kuthubutu
inataka utafiti wa soko na viwango nilisha jaribu kufanya utafiti .kuna senta ya biashara Dubai na uingereza zote watakupa mwongozo nini cha kufanya maana zipo kwenye balozi zetu.
Mkuu unaonaje ukifunguka Zaidi khs utafiti uliofanya naamini Utasaidia wengi hapa Jukwaani!
mwenye thread ameuliza jinsi ya kupata mzigo tu, mchongo wa soko tayari anao, sasa nyie mnakuja na siasa nyiiingi! uko wapi lucky sabasaba jamaa anataka kuleta bidhaa huko jamaa wanamtisha! Malila mzee wa shamba msaada wako unahitajika huku!
Naomba kuwasiliana na wewe mkuukama uarabuni matunda ni biashara kubwa ila kuna viwango mfano Maembe kuna aina wanazi hitaji na kuna aina ya uandaji kuna madawa ya kupiga ili ziwe kwenye kiwango chao.
Niproject kwakua pengine uwe na shamba uzalishe mwenyewe au utoe elimu Kwa wakulima wazalishe wewe ununue kutoka kwao.
sema maelezo ni marefu siwezi kuandika yote.
uni pm nikupe maelezo ya kutosha
NAOMBA MAWASILIANO NA HAO VIJANA WA NJOMBE PLSNilikuwa shamba Njombe,
Ni kweli soko la Ulaya linataka viwango ila lipo na linakuwa sana. Wapo vijana njombe wanauza parachichi Italy, na mimi nimefika shambani kwao. Nikiwa Njombe mjini nimeshuhudia maandalizi ya kilimo cha Matunda kule Ihanga,pia Madeke Lupembe kuna nanasi la kufa mtu na kiwanda kinajengwa. Kwa sasa parachichi zinasindikwa Kiwira Mby, akina Chai bora wanalima parachichi for export kule Mby/Mufindi.
Kwa ufupi, soko la matunda huko majuu lipo sana toka huku kwetu, kama mtu yuko serious aseme nimpe simu ya vijana pale njombe aone nini kinaendelea.
Ni vizuri kujua mteja anataka viwango gani na wewe utimize,usichakachue. Nikiwa Iringa ktk kiwanda fulani, Waholanzi walimwaga mzigo wetu wote baharini kwa sababu tuliongeza sukari kidogo ktk pineapple rings tulizopeleka.