Biashara ya mchele wa jumla Arusha

missfancy

Member
Joined
Jun 10, 2014
Posts
33
Reaction score
5
Habari zenu wakuu....je biashara mchele wa jumla jijini arusha unalipa?je mtaji wake unaweZa kua bei gani?na huwa inakuaje....naomba kueleweshwa tafadhali....
 
Kama una millioni mbili na nusu inatosha kabisa mchanganuo no kama ifuatavyo mzani 150,000 , gharama ya kusafirisha mzigo(Mchele) wa kutosha kutoka kahama au mbeya 1,200,000 , fremu, kodi(TRA) na gharama nyingine 700,000. Anyway gharama nilizoweka ni makadirio ambapo kwa hiyo 1,200,000 inaweza kuchukua gunia za kilo hamsini kama ishirini hivi kutoka kahama(shinyanga)
 

Manunuzi na usafiri hadi Arusha tsh 1200 kwa kilo? Usafiri mbeya hadi Arusha upi?
 
Mkuu mim hapa hata sijaelewa, kwanini umependa kufanyia Arusha? mchele ni shida uko? kama ndo hivyo mchangiaji aliesema gharama za kusafirisha kutoka mbeya au kahama ni 1,200,00, nafikiri wewe kwa kua una anza hiyo hela inaweza kuwa kubwa kama hauna mtaji wa kutosha hivyo bas, kama uko arusha fanya utafiti kama kuna magari ya mizigo yanatoka Arusha kwenda kahama au mwanza au mbeya kupeleka mizigo. nina hamini lazima yapo, ukisha yajua ongea nao kwamba wakimaliza kushusha mzigo uko, wakati wanarudi arusha uwape mzigo wako kuja nao, kwa hapo gharama itakuwa ndogo kidogo kwa sabb mwenye gar akishusha mzigo kurudi na gari ikiwa empty umgharim sana.

Lakini pia, kama hiyo itashindikana, uko mbeya au kahama kuna magari yatakuwa yanakuja arusha kuleta mizigo ya watu, fanya utafiti kama yapo ulizia mawasiliano yao hivyo unaweza kupata gari ina miziko ya watu wawili na wewe ukawa watatu mkalijaza gari kubwa hivyo gharama ya usafiri itakuwa imepungua kwako.
 
Kilo ni shilling ngapi Arusha,nina tan kadhaa,na naweza pata shule kuwauzia mchele safi kabisa grade 1,I mean mbegu inayoitwa Zambia na faya dume zote kutoka Mbeya,ila hela ni cash
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…