Biashara ya miti ya mbao Iringa

Biashara ya miti ya mbao Iringa

JOSEPHAT_07

JF-Expert Member
Joined
Aug 8, 2011
Posts
303
Reaction score
181
Naomba kujua kuhusu bishara ya miti yambao Iringa. Ninataka kununua shamba ili nipande miti then baadae nije kuiuza. Nilichokuwa nataka kujua ni...

*Je, huwa inachukua miaka mingapi?
*Bei ya kila mti ni shillingi ngapi?
*Na pia gharama zingine kama zipo
*Na weza nikaanza na heka ngapi

Kuhusu kununua eneo gharama hakuna tatizo. Naombeni msaada kwa wale wanaoifanya shughuli hii.
 
Ninafahamu kuhusu miche ya miti iringa mafinga nikuanzia Tzs 200... mpaka Tzs 500 haiwezi kuzidi hapo piga ua
 
Ninafahamu kuhusu miche ya miti iringa mafinga nikuanzia Tzs 200... mpaka Tzs 500 haiwezi kuzidi hapo piga ua
Nilikuwa nataka kujua ni bei ya miti iliyokuwa tayari kuvunwa
 
Wadau mnaofanya biashara hii mbona kimya, nahitaji msaada
 
Sisi tunafanya hiyo bihashara ila yupo Mwanza, naweza kukuunganisha na mdau wa hiyo bihashara ni mvunaji kwenye shamba la miti Sao hill. Kuhusu mbao za vijijini hapo sina mtu.

Sent from my SM-A105F using JamiiForums mobile app
 
Naomba kujua kuhusu bishara ya miti yambao Iringa. Ninataka kununua shamba ili nipande miti then baadae nije kuiuza. Nilichokuwa nataka kujua ni...

*Je, huwa inachukua miaka mingapi?
*Bei ya kila mti ni shillingi ngapi?
*Na pia gharama zingine kama zipo
*Na weza nikaanza na heka ngapi

Kuhusu kununua eneo gharama hakuna tatizo. Naombeni msaada kwa wale wanaoifanya shughuli hii.
-Inategemea na aina ya miti. Milingoti inachukua muda mfupi zaidi ya pine. Pina inatumika kweny mbao inachukua si chini ya miaka 9-14 japo unaweza vuna kabla ya hapo ingawa bado haitakua na unene wa kutosha.

-Mlingoti inatumika kweny nguzo, bei zake mara ya mwisho ilikua 35k-50k ila pine wanauza kwa shamba zima bei itategemeana na maelewano yako na mnunuzi/pia unaweza kuvuna mwenyewe uuze mbao.
-Gharama zingine ni kusafisha shamba kila mwaka na kutengeneza fire line njia za kuzuia moto mpakani. hii inakuaga kama 60k kwa eka 1. bei inatofautiana kijiji na kijiji.

-Unaweza kuanza na kiasi chochote kulingana na uwezo wako.

Kila la kheri.
 
-Inategemea na aina ya miti. Milingoti inachukua muda mfupi zaidi ya pine. Pina inatumika kweny mbao inachukua si chini ya miaka 9-14 japo unaweza vuna kabla ya hapo ingawa bado haitakua na unene wa kutosha.

-Mlingoti inatumika kweny nguzo, bei zake mara ya mwisho ilikua 35k-50k ila pine wanauza kwa shamba zima bei itategemeana na maelewano yako na mnunuzi/pia unaweza kuvuna mwenyewe uuze mbao.
-Gharama zingine ni kusafisha shamba kila mwaka na kutengeneza fire line njia za kuzuia moto mpakani. hii inakuaga kama 60k kwa eka 1. bei inatofautiana kijiji na kijiji.

-Unaweza kuanza na kiasi chochote kulingana na uwezo wako.

Kila la kheri.
Asante angalau nimepata Mwanga
 
Naomba kujua kuhusu bishara ya miti yambao Iringa. Ninataka kununua shamba ili nipande miti then baadae nije kuiuza. Nilichokuwa nataka kujua ni...

*Je, huwa inachukua miaka mingapi?
*Bei ya kila mti ni shillingi ngapi?
*Na pia gharama zingine kama zipo
*Na weza nikaanza na heka ngapi

Kuhusu kununua eneo gharama hakuna tatizo. Naombeni msaada kwa wale wanaoifanya shughuli hii.
Nimeifanya biashara ya mbao na magogo kwa miaka Kama 4 hivi.
Miti inauolimwa Sana ni Pine(msindano) na eucalyptus (mlingoti)

Pine
Mche unauzwa 100-200
Ekari 1 inachukua Miche 550-650
Unatakiwa kuihudumia kwa miaka yote mpaka unavuna. Hapa ni kuweka barabara ya kuzuia moto kuzunguka shamba Zima+kukatia matawi mara 2 mpaka kuvuna. Usisahau kupunguzia(thinning) mwaka wa 6 au 7.
Ukitaka ikulipe vizuri inashauriwa itunze mpaka mwaka wa 14 au zaidi. Kwa umri huo unao uhakika wa kuuza 5000-8000 kwa mti mmoja.
Ukivuna mara moja unayokazi ya kupanda mingine tena.

Mlingoti
Mche unauzwa 150-300
Ekari 1 inachukua Miche 650-800 (inabananishwa ili irefuke zaidi).
Utaihudumia kwa miaka 5 ya mwanzoni baada ya hapo unaiacha. Huduma yake hapo ni barabara ya kuzuia moto tu. Hii haikatiwi matawi maana huwa inajipruni yenyewe.
Mwaka wa 8 unaweza kuvuna nguzo ambazo bei huwa ni 15000-30000 kutegemea zilipo. Au ukivumilia mwaka 15 na kuendelea unauza kwa ajili ya mbao. Mti mmoja huuzwa Kati ya 40,000 -100,000 kwa mti mmoja.
Ikishavunwa inaota mingine kutoka kwenye visiki hivyo, utavuna wewe mpaka mjuu wako atavuna pia.

Usiangalie muda wa kuihudumia, angalia utakuja kupata nini na ni lini.
Kila la kheri mkuu.
 
Ekari moja ya miti ya mbao ambayo umeisubiria kwa miaka 10 kabla ya uvunaji ni Tsh 1.2 tu, CCM watatuua walahi
Hakika, Kama hujaihudumia vizuri kutoka mwanzoni na ukavuna umri huo hautoona pesa, especially pine. Ila unayo option ya kulima milingoti pia maana nguzo Ina soko kubwa na mbao yake sokoni haipungui 12,000/= per piece.
 
Back
Top Bottom