Biashara ya nafaka Dar ipoje?

Wazo zuri sana
 
ishi hapa mkuu
 
Usipotoshe watu humu hakuna ufuta wa kununua buku huku kwa kilo...nakuambia hivyo kwasababu mimi hizi ndizo biashara zangu nina vituo kuanzia matekwe,mihima,nakiu,ngumbu,kibutuka,kiperemende,nangulugai huko kote ni chaka langu na laiti ingekuwa hivyo unavyodai mimi leo ningekuwa bilionea
 
Kweli kabisa wewe ni mfanyabiashara huyo bwamdogo anahesabu za kwenye madaftari mno
 

Njoo mkoa wa lindi,wilaya ya kilwa,tarafa ya njinjo huku ufuta tunanunua buku buku tu na ukipanda saana buku jero na gharani hapo inakuwa bei 3800 mpaka 4000+ acheni ujuaji wa kila kitu au mnataka kila mtu aonyeshe assets zake kupitia hii biashara ya ufuta mfano mzuri mwaka jana kuna watu watu huku wamepiga hela balaa maana walinunua ufuta buku buku mnada wa kwanza wakauza 3000+ na bei za minada ikawa imepanda mpaka mnada wa mwisho ulikuwa 4250.
 
Huyu kwanz nahis hayupo mtwara maana analahisisha tu mambo.
kasikia wapi cjui eti ufuta kilo ununue buku

Mm nipo mkoa wa lindi,wilaya ya kilwa,tarafa ya njinjo.Ingis field mwenyewe dogo usipende sana kila kitu kuuliza huku wengine wapo kwa shemeji zao hawajui chochote kuhusu kilimo.KILIMO NI UTAJIRI
 
Kama muda unao mdogo wangu, mtafute mtu mmoja ambae ni ndugu yako mnaewezana awe mkubwa kdg kukuzidi ambae ana mishe za kuungaunga kisha mwambie kuna boss anahitaji vijana wawili...jifanye kuwa anataka ma agent wa kumuuzia mzigo dar.

Wakati huo inabidi ujue mahindi utakuwa una chukulia wapi ukipata tenda.

Cha kufanya... Toa kma laki 1.5 muwe na Sampo yenu ya mahindi halafu mnakuja dar sehemu ambazo zina mashine za kusaga (msije mpaka mjue kwanza zinapatikn wapi) mkija mnapita kila mashine ili kujinadi kuwa mnauza mahindi kwa rafiki (na wakati huo inabidi mjue bei za dar zipo vipi ili mjue mtauzaje)... Mkifanya survey kuna kitu pia mtajifunza na kusoma zaidi Fursa za biashara.

Nafikiri kidogo nitakuwa nimeeleweka... Au kwa huko ulipo ni zao gani lina bamba sana, kisha nitakwambia nini cha kufanya... Ikiwezekana njoo pm nitaona ujumbe wako kwa haraka zaidi na kueleweshana
 
Dqrvhata u
Dar hata ukileta mavi ya kuku utauza.
 
Acha uongo wewe unaowazungumzia wewe ni waliokopesha kula maua na sio kwamba eti walikuwa wananunua wakati wa mavuno
 
Mm nipo mkoa wa lindi,wilaya ya kilwa,tarafa ya njinjo.Ingis field mwenyewe dogo usipende sana kila kitu kuuliza huku wengine wapo kwa shemeji zao hawajui chochote kuhusu kilimo.KILIMO NI UTAJIRI
Ingekuwa hivyo mwaka jana tusingenunua 2800 huku nangulugai wote tungekuja huko njinjo hebu nikuambie kitu nina mtandao mpana sana wilaya ya kilwa kiasi kwamba kokote bei zikishuka huwa naambiwa...kama kweli upo njinjo unamjua au umewahi kulisikia jina la mtu anaitwa JANDO?
 
Thanks nitalifanyia kazi
 

Nitumie namba yako ya WhatsApp nikutumie stakabadhi zangu za mwaka jana kuanzia mnada wa kwanza kabisa mwezi wa tano ulipigwa mpaka mnada wa mwisho mwezi wa kumi ulipigwa.Huyo dogo aingie mwenyewe field sio kila kitu kuomba ushauri tu humu anapoteza muda bure.Humu wengi munamtandao wa madalali tu
 
Mac Alpho nisindikize zangu Lindi tafadhali, ama hutaki ile aiseT yako tena..??[emoji2960]

Tena kama unakuja Lindi dada yangu njoo wilaya ya kilwa tarafa ya njinjo na kata ya miguruwe kuna kijiji kama zinga kitongoji cha nanyumbu huko watu wanalima ufuta balaa tena wapo wasukuma wanapata mpaka gunia mia moja halafu hawapendi kwenda kuuzia kwenye maghala waanze kusubiri hela wiki mzima wao wanauza chomachoma tu ufuta wao.KILIMO NI UTAJIRI
 
Hiyo biashara ya ufuta inahitaji mtaji kama kiasi gani
 
Mimi sio dalali ila ninachokuambia ni ukweli kama kwasasa watu wanakopesha kula maua kwa bei ya 1000 kwa kilo labda wewe ndie unachanganya mambo,mkulima hawezi kukuuzia wewe ufuta ulio tayari kwa bei ya 1000 wakati tayari ameshajua bei ya mnada kuwa ni 3500
 
Hiyo biashara ya ufuta inahitaji mtaji kama kiasi gani

Kama ndio unaanza kujitafuta ww njoo uanze hata na laki sita tu bei inaanza buku kwa kilo unapata gunia sita hapo na ikifika buku jero unapata gunia nne hapo na bei ghalani yani kwenye vyama vya ushirika inaanza 3000+ ila itahitaji upate mwenyewe tu ili uweze kupata mzigo kwa haraka au kama una mtaji wa kutosha anza na milioni mbili tu kwa kuwa ndio unaanza ili upate uzoefu na mwenyeji muaminifu hata ukija tena msimu mwingine unakuwa sio mgeni tena.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…