Biashara ya nyumba ya wageni yenye kifungua kinywa

Biashara ya nyumba ya wageni yenye kifungua kinywa

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
Mahitaji ya nyumba ya kulala wageni yapo kila sehemu hasa kama kuna shughuli za uchumi mfano mgodi wa madini, kilimo hasa cha mazao ya biashara kama pamba na korosho.

Hata shughuli za utalii zinaleta fursa kwa nyumba za wageni hasa kwa wale low budget tourist. Siku hizi Waafrika wanapenda kutembeza watoto katika nchi zenye vivutio. Unaweza kukuta familia ina budget ya $500.

Mwenyewe uwe na mapenzi na biashara hii. Uwe na uzoefu kidogo na housekeeping, catering na bar tender.

Kwa nyumba ya vyumba 20 kuwa na kama shuka 200. Si lazima ufue kila siku unaweza kufua mara mbili kwa wiki kama ni low season.

Uwe na washing machine hata ya kilo kumi inatosha. Shuka zinazochafuka sana tupa zitakugharimu kuzirudisha katika ubora.

Uwe na uhakika wa maji na umeme.

Usiku mmoja Tshs 5,000, kifungua kinywa kinaweza kuwa ndizi, matango, chai au kahawa, mayai mawili na kipande cha mkate.

Kwa anaetaka kula mchana, atoe order wakati wa chai na wa usiku waeleze mapema.
 
Mikoani hakuna hata biriani....hata pilau kulipata utatembea wee .hata ukiwa na mgahwa standrd upike fresh bites nzuri juic kuntu hutok kapa
 
Usisahau na tv [emoji12]
1573610442742.jpeg
 
Nilielnda Wilaya za Kasulu na Kibondo mkoani Kigoma kule Gest zinalipa asikuanbia mtu.

Kibondo kuna UN Agency zisizo kuwa na idadi baado Intenational NGOs bado local NGOs.

Aisee mji kama Kibondo kila siku kuna semina na Gest ni nyingi na zinajaaa zote the same Kasulu.

Gest ukiwa location ya Sehemu zenye pilikapilka za mikutano ndo vizuri.
 
Wanao Jaza Gest sana ni Watu wanao kuja kwa ajili ya Mikutano kama semina na Wafanya biashara. Wafabya biashara ni Dai 1 anasepa ila watu wa mikutano ni siku hadi 24 wapo hapo kwako tu.

Tofauti na hapo labda wale wageni wenyeji basi.
 
Back
Top Bottom