Biashara ya uji

Biashara ya uji

noony

Member
Joined
Apr 6, 2018
Posts
65
Reaction score
52
Habari za majukumu wanajamvi, matumaini yangu mnachukua taadhari dhidi ya janga hili la Corona.

Niende moja kwa moja kwenye mada. Mimi ni binti miaka 25 nimemaliza chuo mwaka wa tatu sasa sijabahatika kupata ajira rasmi ila nnajishughulisha na shughuli za hapa na pale mradi mkono uende kinywani.

Ninatamani kuanzisha biashara ya kuuza uji katika sehemu zenye watu wengi. Kwa sasa naishi Iringa. Malengo yangu ni kuwa na sehemu kama 10 za kuuza uji (sio ofisi bali vijana wa kutembeza katika maeneo hayo 10) asubuhi na jioni kwa mtaji wa sh 300,000.

Naomba kwa mwenye ujuzi au uzoefu au hata mawazo bunifu au ushauri wowote juu ya biashara hii.

Asante.
 
Fanya lakini sikushauri kuanza na pesa yote hiyo.

Anza hata na Themos 3 au 5 na utakuwa unaongeza kidogo kidogo kulingana na mwenendo wa biashara utakavyokuwa.
 
Ni Idea nzuri sana, Ila kuna vitu unapaswa kuvifanya,

1.lazima uzalishe uje very Unique
2. Distribution model yako iwe tofauti kabisa.

3.packaging yako iwe tofauti kabisa

Nitafute kwa wakati wako nikupe dondoo hasa Packaging unaweza fanya vipi na Distribution model iweje.


Sent using Jamii Forums mobile app
Asante. Ntakutafuta
 
Hizo vitenge sio Common? Kinacho kosekana ni Ubunifu na sio common
Tuseme za ukweli uji umekuwa common kwa sasa!....sijajua km kuna kipya!
Ningekuwa ndo mie Maathai ningeenda Katoro kuchukua vitenge vya bei chee!...kila kitenge sikosi 4000!.chukua kitenge kwa 18000uza kwa 25000

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom