Biashara ya Uokaji (Bakery): Mbinu, Ushauri na Changamoto Zake

Evmen ningewashauri mjipange vizuri ili muanzishe a modern bakery. Ninazumgumza hivi kwani sehemu nyingi watu wanaanzisha bakery ndogo ndogo na kikubwa wanashindwa kukidhi mahitaji ya watu. Mfano anzisha bakery maeneo ya tegeta na ukidhi demand ya market area ya tegeta, boko na bunju, pia kuna bidhaa nyingine

Packaging ni muhimu sana .... lazima muwe na vifungashio attractive na vinavyoendana na wakati

hivyo mtahitaji kuwa na vifaa ambavyo ni semi industrial ... kwa ufahamu wangu mnahitaji stainless steel tables, dough mixer, rotary oven and shelves vitu vingine ni vidogo vidogo

pia mnaweza kuingia kwenye associated products kama hizi.

 
Asante, LAT, Lengo letu ni kuanzisha modern bakery and iwe na vifaa vya kisasa, ndo maana I need list ya vifaa vinavyoitajika and kama possible sehemu zinapatikana ili tutembelee tukaone then we decide, coz we want to make not only bread but everything a bakery can make kama cakes etc
Kama labda kuna mtu anajua web where I can get more info ntashukuru pia
 
Jaribu searching ya ALIBABA.COM kuna watengezaji wengi tu wa hizi machine..All the best!
 
Baada ya tatizo la kupata kazi kuwa kitendawili kisichoteguliwa naomba msaada wa machines gani zinazohitajika kwa kuanzia kufungua small bakery any idea plz naomba mnisaidie kwa wale wanaojua. thanks
 
Ndg zangu wanaJF, kwanza poleni sana kwa msiba wa mwanaJF mwenzetu RM iliyotuchukua almost the whole week kuomboleza.

Napenda kusema yote ni mipango ya Mungu na tulio bado hai let us make this world a better place for US and next GENERATION.

Naomba wenye UELEWA na biashara ya BAKERY wanijuze if it is a good business to engage in (is it paying?), tayari ninayo OVEN yenye uwezo wa kutengeneza walau Mikate 20 at once.

Nashindwa kuanza bcoz nimeambiwa lazima niwe na TIN no, LESENI, TFDA, Mazingira masafi etc, so where can i get all these things guyz or is it possible nikaanza bila moja ya hivyo vitu?

Mie ningependa nianze polepole wakati biashara ikikuwa, walau hata nikianza atleast na mikate 50 per day i have NO PROBLEM with that.

Natanguliza shukrani zangu ndg zangu.
 
Mkuu Hongera sana kwa jitihada zako, mkuu hizi ndo moja ya aidia ambazo zinamshiko mkuu.

- Labuda mimi nikushauri kitu kimoja mkuu,
1. Hii biashara kama ziilivyo biashara nyingine ni lazima ziww zinatambulika na serikari yetu, hii ni pamoja na kuwa na
- TIN NO
- LESENI
- TFDA CHETI

Mkuu huwezi fanya hiyo viashara bila kuwa na hivi vitu na kitu kama TBS kupata nembo yao si kitu cha mchezo mkuu inaweza kukuchukua miaka kama usipo kuwa makini, make hawa jamaa wanataka

- ENEO LA KUOKEA LIWE SAFI
- VIFAA VISAFI
- NYUMBA AMBAYO IMEJITENGA YENYEWE NA HAISHI BINADAMU HUMO NA IWE NA MADIRISHA NA MWANGA WA KUTOSHA
- WAFANYA KAZI WAKO LAZIMA WAVAE MAVAZI MALUUMU
- NA MENGINEYO

Mkuu si kwamba ukitimiza haya ndo utapewa TBS, razima wakapime na hiyo mikate yako na watakuwa wakifanya ukaguzi wa kushitukiza kuona kama unafuata taratibu zote, na hawakuambii siku wanakuja, na wakikukuta umevunja baadhi ya masharti ndo sahau kabisa, itabidi uanze tena mwanzo

MKUU KUHUSU ENEO LA KUWEKA HII KITU,

- Mkuu naamini Dar, Arusha, Mwanza, Mbeya na miji mingine mikubwa kuna viwanda vya kutosha vya mikate, na ukisema uweke Dar, inakuchukua muda mrefu sana kuja kukopinti na watangulizi ambao wameisha kamata soko vya kutosha, na itakuhitaji kuwa na mtaji wa kutosha ili ufanye matangazo na lazima uwe na Distribution chanel za ukweli, so inahitaji capita ya uhakika.

- MKUU SASA UFANYE NINI?
- Mimi ningekushauri fanya utafiti wa kutosha katika miji mingine hapa Tanzania ambayo hakuna kiwanda cha hii kitu, na ukiona kuna demand fungua huko mkuu, ili uweze kukua vizuri, si razima Dar tu.

- Mkuu hata wawekezaji unao waona huku Africa wamekimbia stiff competition huko Ulaya, Marekani na Asia na kuja huku, mitaji yao haiwaruhusu kuendesha biashara huko kwao kwa sababu ya competition kubwa sana

- So hata sisi sometime ili kuepuka kutumia nguvu nyingi kufungua biashara kwenye miji mikubwa ambayo tiyali kuna business za aina hiyo nyingi tunaweza enda mikoani ambako tutatumia capital kidogo na ukisha kuwa unaweza rudi mjini kushindana na hao waliopo
 
Nataka kufanya biashara ya bakery lakini sina hakika kama inalipa au la.

80% ya mikate na bishaa zitakuwa za brown hivyo hatutegemei volumes bali itakuwa ni quality kwenda kwa juu japo itakuwa na bei ya juu kidogo

Naskia kuna wazungu wa Denmark wako Dar wanafanya ila sina hakika jina la bakery yao na kama wanauza sana

Washindani wakubwa wangu ni wale jamaa pale shoppers plaza na pia jamaa wa pale jengo la mkapa. Lakini sisi tutawekeza zaidi kwenye quality, usafi, na niche market ya wasio kula mitake ya white

Je, italipa? na inahitaji kiasi gani?
 
wahi mkuu

soko lipo .... kulipa au kutokulipa itategemea jinsi gharama halisi zitakavyokuwa
 
Kizuri chajiuza! usiweke bei kubwa ambazo watanzania wengi hawawezi kuzimudu, ni vizuri kumix na vitafunwa vingine vingine ili upanue wigo wa walaji, size ya vitafunwa irange from small-medium-large-extra large c'se tegemea wanunuzi wa robo mkate kutokana na vipato/ wengine watakuwa walaji wa njiani (hawahitaji kwenda navyo nyumbani), tafuta baker wazuri waliosomea usiende kuokota uswahilini.
 
Bakery nyingi zikianza huwa zinauza mikate mizuri sana sana lakini baada ya muda mfupi mikate hubadilika, mkate wa leo kama wa majuzi. Wakati mwingine unahisi unakula unga wa ngano, usifanye hiyo tabia mnatuboa sana sisi walaji!
 
Jamani mimi nishasema target market yangu ni ndogo sana.

Ninatarget 1% ya Watanzania. Watu wenye hali za juu ambao najua nitawapa bei za juu na watanunua.

Maybe baadae nitaweza kuwapa hao wengine lakini target ni wale wenye hali nzuri ambao hawato mind kupay the price for a TOP Quality product at a price.
 
Nami ni kuunge mkono, nataka kuanzisha mikoani hasa mwanza ,nahitaji machines zenye kukidhi mahitaji ya kuoka vitafunwa mbalimbali.
 
Kama bado demand sio kubwa sana nna ki suzuki carry truck bado kipya na kiko ktk hali nzuri chaweza kukufaa kwa ajili ya kusambazia Mikate kwa wateja wako; so kama bado huna usafiri wa kufanya hivyo waweza nicheki kwa namba yangu 0714/67/84~476866.
Namba zote hizo tgo,voda na Airtel zipo hewani 24/7 Karibu tugawane umaskini.
 

Kaka nimekupata na nitakupigia

ningependa kutoa taarifa kuwa kazi zetu sisi tutakuwa tunafanya usiku. By Alfajiri tunaanza distribution. Maeneo ni Masaki, Obay, Mikocheni, Msasani, Upanga.

KWA WANAOKAA MBEZI BEACH TUTAWAFIKIA BAADAE LAKINI KWANZA TUTADEAL NA HAO WANAOKAA MAENEO HAYO.
 

Kila la kheri kaka mkubwa
 
Mkuu mtaji ni shilingi ngapi? Na wapi unatoa hizo ingredients?nataka niangalie kama inawezekana nifungue na mie huku Moshi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…