Mkuu Hongera sana kwa jitihada zako, mkuu hizi ndo moja ya aidia ambazo zinamshiko mkuu.
- Labuda mimi nikushauri kitu kimoja mkuu,
1. Hii biashara kama ziilivyo biashara nyingine ni lazima ziww zinatambulika na serikari yetu, hii ni pamoja na kuwa na
- TIN NO
- LESENI
- TFDA CHETI
Mkuu huwezi fanya hiyo viashara bila kuwa na hivi vitu na kitu kama TBS kupata nembo yao si kitu cha mchezo mkuu inaweza kukuchukua miaka kama usipo kuwa makini, make hawa jamaa wanataka
- ENEO LA KUOKEA LIWE SAFI
- VIFAA VISAFI
- NYUMBA AMBAYO IMEJITENGA YENYEWE NA HAISHI BINADAMU HUMO NA IWE NA MADIRISHA NA MWANGA WA KUTOSHA
- WAFANYA KAZI WAKO LAZIMA WAVAE MAVAZI MALUUMU
- NA MENGINEYO
Mkuu si kwamba ukitimiza haya ndo utapewa TBS, razima wakapime na hiyo mikate yako na watakuwa wakifanya ukaguzi wa kushitukiza kuona kama unafuata taratibu zote, na hawakuambii siku wanakuja, na wakikukuta umevunja baadhi ya masharti ndo sahau kabisa, itabidi uanze tena mwanzo
MKUU KUHUSU ENEO LA KUWEKA HII KITU,
- Mkuu naamini Dar, Arusha, Mwanza, Mbeya na miji mingine mikubwa kuna viwanda vya kutosha vya mikate, na ukisema uweke Dar, inakuchukua muda mrefu sana kuja kukopinti na watangulizi ambao wameisha kamata soko vya kutosha, na itakuhitaji kuwa na mtaji wa kutosha ili ufanye matangazo na lazima uwe na Distribution chanel za ukweli, so inahitaji capita ya uhakika.
- MKUU SASA UFANYE NINI?
- Mimi ningekushauri fanya utafiti wa kutosha katika miji mingine hapa Tanzania ambayo hakuna kiwanda cha hii kitu, na ukiona kuna demand fungua huko mkuu, ili uweze kukua vizuri, si razima Dar tu.
- Mkuu hata wawekezaji unao waona huku Africa wamekimbia stiff competition huko Ulaya, Marekani na Asia na kuja huku, mitaji yao haiwaruhusu kuendesha biashara huko kwao kwa sababu ya competition kubwa sana
- So hata sisi sometime ili kuepuka kutumia nguvu nyingi kufungua biashara kwenye miji mikubwa ambayo tiyali kuna business za aina hiyo nyingi tunaweza enda mikoani ambako tutatumia capital kidogo na ukisha kuwa unaweza rudi mjini kushindana na hao waliopo