Biashara ya viatu Nairobi kuja bongo

Biashara ya viatu Nairobi kuja bongo

Grena

JF-Expert Member
Joined
Jul 30, 2016
Posts
656
Reaction score
1,553
Habari zenu wakuu,
Msaada wa mtu yoyote ambaye ashafanya ama anajua mtu anayefanya biashara ya viatu vya mtumba kutoka Nairobi kuja bongo.
 
Alafu hizi biashara mbona zinachanganya? Kuna watu juzi tumekutana kariakoo wanachukua viatu aina ya sandals zile za fashion, wanasema wanapeleka Kenya. Kwa bei ya jumla tuliokuwa tunauziwa pale tsh 10,000 kwa hela ya kwao walisema tsh 600, na sandals kama hizo kwa hela ya kwao huko zinauzwa tsh 1400.
 
Viatu gani? Bear in Mind kwamba Pesa ya Kenya inanguvu sana, Hahaa Pesa ikiwa na nguvu hifanya watu wanao taka kuuza bidhaa nje kupata wakati mgumu sana na wale wanao ingiza kuwa na Advantage.

Ndo maana bidhaa za Kenya Tanzania huwa bei imechangamka sana ni kutokana na wao pesa yao kuwa na Thamani kubwa.

Pia hii inategemeana na kama nchi ina Production ya kueleweka. Tanzania pesa yetu iko chini na tungekuwa na Viwanda vya kutosha tungefaidi sana au basi mifumo ya Kodi ingekuwa Chini tungefaidi sana.
Habari zenu wakuu,
Msaada wa mtu yoyote ambaye ashafanya ama anajua mtu anayefanya biashara ya viatu kutoka Nairobi kuja bongo.
 
Moja ya watu kukimbilia Uganda ukiacha kwamba labda Kodi iko chini ila kikubwa ni pesa yao kuwa ndogo kuliko yetu.

Uganda wanawasumbua sana kenya kwa sababu **** bidhaaa kibao za Uganda kama Maziwa, Mayai, na kadhalika zinaingia kenya na kuuzwa very cheap.

Sisi tungekuwa wajanja tungeuza sana Kenya make pesa yao iko juu.

Wakenya wanapata shida sana kuuza Uganda na Tanzania kwa sababu ya Pesa yao
 
Alafu hizi biashara mbona zinachanganya? Kuna watu juzi tumekutana kariakoo wanachukua viatu aina ya sandals zile za fashion, wanasema wanapeleka Kenya. Kwa bei ya jumla tuliokuwa tunauziwa pale tsh 10,000 kwa hela ya kwao walisema tsh 600, na sandals kama hizo kwa hela ya kwao huko zinauzwa tsh 1400.
Kweli biashara zinachanganya. Kuna wengine bado wanatoa viatu vipya eastleigh Nairobi wanaleta huko. Mimi nlikuwa naulizia viatu vya mtumba coz Nairobi Ni Bei rahisi Sana. Wanavitoaga huku kuleta Bongo.

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom