Biashara ya vyakula afrika kusini na south sudan.

John Deer

Member
Joined
Sep 15, 2011
Posts
36
Reaction score
9
Nimekuwa najihusisha na ununuzi na uuzaji wa mazao hapa nchini tanzania, sasa nafikiria sana kwenda afrika kusini na south sudan.Ninaomba mwenye uzoefu au fursa kwamba naweza KUUZA NINI katika nchi hizo mbili tafadhari naomba michango yenu.
 
Ya sudan sijui ila ya SA ilivuma kuna kipindi hadi wanawake walikuwa wakipeleka prawns (kamba kochi) kule bi weekly nilisikia bei yake nzuri, sijui kwa sasa vingine matunda na nafaka kuku na maziwa kule vipo vingi kwasababu wameendelea sana kuhusu kilimo
 
International trade ni very complicated mkuu, na inahitajika uwe umepractise sana soko la ndani kwanza. Na kwa biashara inayo husu afya za watu ni balaa. Ingekuwa madini sawa. Na kwa South si dhan kuna cha kuwauzia, wale wako mbali sana na kilimo chao ni cha mechanization na gharama zao za uzalishaji ziko chini sana ni vigumu kushindana nao kwenye soko. Na wale wengi ni producer sasa huku wewe unategemea misimu wakati wao ni full time
 

Very good insight Chasha kwa upande wa S.A kwa S.Sudani fursa bado ipo kubwa tu vijana ichangamkieni
 
Ni kweli mkuu saizi yetu ni Sudani, kwa Zuma wale hatuwawezi wako mbali sana. Na unatakiwa kujipanga vilivyo wale wanashindana na wakina Brazil. Na naamini bado kuna furusa kwa soko la ndani, na ili u trade international unatakiwa uwe umekidhi soko la ndani kwanza na ziada ndo inaenda nje
 

Mchele, vitunguu nimesikia kuwa vinapelekwa S.Sudan na watoto wa Moi, kama unaweza kuchanga karaka zako vizuri, hapo ndo pa kuanzia.
 
Ya wanachukua Mchele Magugu wanapaki na kupeleka South Sudani, vitunguu wanachukua kutoka Karatu
 
Hapo kwenye mchele na vitunguu ni pazuri bw malila...ila kama unafahamu kampuni au mtu anayepeleka mzigo ningefurahi zaid ili wadau tupate uelekeo wake.
 
Hapo kwenye mchele na vitunguu ni pazuri bw malila...ila kama unafahamu kampuni au mtu anayepeleka mzigo ningefurahi zaid ili wadau tupate uelekeo wake.

Huwa nawaona pale Ruaha mbuyuni, Mahenge wamepark mifuso wanapakia mzigo, sijawahi kuwadadisi, zamani walikuwa ni Wapemba wakipeleka Comoro, sasa ikaja kuonekana Comoro ni zurumati sana, jamaa wamegeukia Sudan, nafikiri urahisi wa usafirishaji umepelekea watu kugeukia Sudan.
 
Mchele, vitunguu nimesikia kuwa vinapelekwa S.Sudan na watoto wa Moi, kama unaweza kuchanga karaka zako vizuri, hapo ndo pa kuanzia.

Mkuu Malila hapo kwenye mchele huwa ni pagumu kidogo nadhani zuio la kuexport Vyakula hasa mahindi/unga na mpunga/mchele bado lipo
 
Vitunguu maji na vitunguu saumu viko na bei poa sana sudan
 
Mie ninae rafiki yangu pale Juba, alichonieleza ni kwamba fursa ipo kubwa sana kibiashara.
Hususan supply ya Mchele, Sembe, Vitunguu pamoja na Asali.
 
Kwa asali lita moja bei yake ni S.S Pound 20 kwa masoko ya uraiani, kwa supermarkets ni S.S Pounds 45 ambayo ni sawa na Tsh 18,000/-
 
We need appropriate info bureaus to assist our emrging businesses
 
Kwa asali lita moja bei yake ni S.S Pound 20 kwa masoko ya uraiani, kwa supermarkets ni S.S Pounds 45 ambayo ni sawa na Tsh 18,000/-

Mbona unaweza nunua huko na kuja kuuza Bongo? Au wanachukua Ethiopia? Make Ethiopia ndo the kiongozi kwa ishu za asali baarani Africa
 
Asante Chipukizi!

Kama una mtu/suppiler au kwa una connection yeyote tutashukuru kwa maelekezo tafadhari.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…