Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 2,060
- 5,648
Athanas Michael Masubo mwenye umri wa miaka 65 mkazi wa mtaa wa Kashishi kata Nyamhongolo wilaya ya Ilemela mkoani Mwanza anashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kumbaka na kumlawiti bibi wa miaka 68 wakati wakinywa pombe aina ya Konyagi.
Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza Wilbrod Mutafungwa amesema tukio hilo limetokea tarehe saba ya mwezi huu nyumbani kwa mwanaume huyo mtaa wa Kashishi kata ya Nyamhongolo wilaya ya Ilemela, ambapo inadaiwa bibi huyo alifika nyumbani kwa Athanas ambaye ni jirani yake, na kumkuta akinywa pombe aina ya Konyagi ndipo akakaribishwa na kisha wakaanza kunywa wote pombe hiyo.
Soma, Pia: Mwanza: Jeshi la Polisi latoa taarifa za uhalifu ikiwemo ulawiti na ubakaji pamoja na wanawake wanaojihusisha na ukahaba
Kamanda Mutafungwa amesema wakati wakiendelea kunywa pombe hiyo, ndipo Athanas akamuagiza binti wa kazi dukani kununua pombe nyingine ili waendelee kunywa na hapo akamshikia panga bibi huyo huku akimtishia kumuuwa, kisha akatumia mwanya huo kumuingilia kimwili kwa kumbaka na kumlawiti.
Kamanda Mutafungwa amesema baada ya tukio hilo bibi huyo alifanikiwa kukimbia na kutoa taarifa kwa jeshi la polisi ndipo uchunguzi ukaanza na Atanas kutiwa nguvuni na kuhojiwa.
Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza Wilbrod Mutafungwa amesema tukio hilo limetokea tarehe saba ya mwezi huu nyumbani kwa mwanaume huyo mtaa wa Kashishi kata ya Nyamhongolo wilaya ya Ilemela, ambapo inadaiwa bibi huyo alifika nyumbani kwa Athanas ambaye ni jirani yake, na kumkuta akinywa pombe aina ya Konyagi ndipo akakaribishwa na kisha wakaanza kunywa wote pombe hiyo.
Soma, Pia: Mwanza: Jeshi la Polisi latoa taarifa za uhalifu ikiwemo ulawiti na ubakaji pamoja na wanawake wanaojihusisha na ukahaba
Kamanda Mutafungwa amesema wakati wakiendelea kunywa pombe hiyo, ndipo Athanas akamuagiza binti wa kazi dukani kununua pombe nyingine ili waendelee kunywa na hapo akamshikia panga bibi huyo huku akimtishia kumuuwa, kisha akatumia mwanya huo kumuingilia kimwili kwa kumbaka na kumlawiti.
Kamanda Mutafungwa amesema baada ya tukio hilo bibi huyo alifanikiwa kukimbia na kutoa taarifa kwa jeshi la polisi ndipo uchunguzi ukaanza na Atanas kutiwa nguvuni na kuhojiwa.