Bible Mysteries: Q source iko wapi

Bible Mysteries: Q source iko wapi

zitto junior

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2013
Posts
20,537
Reaction score
31,729
Habari za jioni wana JF, ni muda mrefu kidogo sijaweka mada humu ila leo tupate wasaa kidogo tukumbushane mambo machache kuhusu Bible.

NB: Angalizo hii mada ni purely objective tusiiweke kidini na kuanza kashfa, matusi na kejeli kwa imani fulani. Natamani iwe hoja juu ya hoja ili wote tujifunze.
images.jpg


Utangulizi
Kumekua na contradiction sana kwenye vitabu vya gospel hata kwa vitu vidogo tu mfano tarehe ya Yesu kuzaliwa na kufa ama Story ya wale wafungwa pembeni ya Yesu msalabani n.k. Na huu mkinzano unawapa fursa watu kuiona Biblia kama nadharia tu au hadithi za kufikirika (Myhtology) na sababu kuu ni taarifa kadhaa kukinzana.

Kutokuwepo kwa vyanzo halisi vya injili nayo imekua changamoto na inafikia wakati watu wanahoji uhalisia wa matukio ya kipindi cha Yesu. Yaani yalikua verified wapi ama version ipi ya vitabu vya injili ni credible zaidi. Ili kusolve haya yote wanatheolojia walijaribu kujikita katika kutafuta vyanzo vya vitabu vya injili.

Q Source
Msimamo uliopo kwenye ulimwengu wa kitheolojia na imani ni kwamba kitabu cha kwanza kuandikwa ni Marko maana ushahidi ni kwamba Mathayo na Luka wamenakiri masuala mengi kutoka injili ya Marko. LAKINI kuna maandiko yaliyopo katika Mathayo na Luka ILA hayapo kwenye injili ya Marko. Hiko chanzo cha pili kikapewa nickname ya Q yaani Quelle source.
images.png

Chanzo hiki kina nadharia mbili kwanza; ni simulizi za moja kwa moja walizosikia hao waandishi wa Mathayo na Luka kutoka kwa Yesu na wanafunzi wake. Nadharia ya Pili ni kwamba ni maandiko yaliyoandikwa yakiwa na yamenakiriwa original kabisa kutoka kwa Yesu ama wanafunzi wake.

Kupitia nadharia ya pili swali linakuja.... Je Q source iliandikwa na nani?

Q source kwanini isingekua kitabu kabisa kwenye Biblia?

Je kilifichwa ili kuondoa ukweli wa taarifa fulani?

Kuondoa Sintofahamu

Ikumbukwe kma Q source ni original script yenye uhalisia zaidi. Ingesaidia kuondoa sintofahamu hasa kwa kukinzana kwenye masuala kadhaa ya kibiblia mfano nitoe

Mathayo 2:1 inaonyesha Yesu alizaliwa kipindi cha Herode (4 BC) ila Luka 2:2-3 inaonyesha Yesu alizaliwa kipindi cha Governor Quirinius (6 AD). Ila kungetumika source moja tu mfano hyo Q source ingesaidia kuondoa discrepancy zote zilizopo na kuweka msimamo mmoja wa Injili.

Mat 12:39 Akajibu, akawaambia, Kizazi kibaya na cha zinaa chatafuta ishara, wala hakitapewa ishara, ila ishara ya nabii Yona

Marko 8:12
12 Akaugua rohoni mwake, akasema, Mbona kizazi hiki chatafuta ishara? Amin, nawaambieni, Hakitapewa ishara kizazi hiki.

Mfano hapa je mtu wa kizazi kile ataamini kipi? Yesu alitoa ishara ama hakutoa yoyote? Je haiwezi mchanganya mtu kiimani?
images (1).jpg

Hitimisho
Nimeleta mada ili tujadili hapa je Q source ipo? Na kama Ipo Iko wapi? Je ingeweza kusaidia kuondoa ukinzano? Je ukinzano huu wa injili hauondoi credibility ya Biblia kma kitabu kitakatifu (maana tunaamini imeandikwa kwa uvuvio wa Roho Mtakatifu)

Karibuni kwa mjadala
 
Kabla hatujaenda mbali mm nilitaka kujuzwa kwann biblia ina copy rights ( haki miliki) je hiyo pesa ya copy rights huwa analipwa nan?

Nawasilisha!
Mkuu bible haina copyright ila wachapishaji wa biblia ndio wanaweka copyright kwa version zao.

Mfano New International Version ilikua inachapishwa chini ya Zondervan/Harper-Collins. Hivyo ina copyright/patent chini ya hyo kampuni husika na version husika.

Hta ww leo ukija na tafsiri yako ya Biblia maybe ya Kisukuma unaiwekea copyright kwa version husika na pesa itakuja kwako if at all mtu akitaka kuprint na kuuza.

I hope imekaa sawa
 
Usipate shida sana. Biblia imeandikwa ni wanadamu kuna historia, unabii,mashairi, n.k. msingi mkuu ukiwa ni ujumbe maalum.

Sijui ingekuwaje kama ingesemekana ilishushwa, halafu ukute kuna vitu humo havijakaa sawa.
Mkuu Yesu alisema kwenye kitabu cha ufunuo kwamba watu wasiongeze au kupunguza kitu kutoka kwa maneno yake.

Ssa huo ukinzano wa baadhi ya mistari ya vitabu vya injili hauoni vinakiuka maagizo yake?

Je huoni ingetumika source moja kuu say Q source ingesolve changamoto hii?
 
Mkuu Yesu alisema kwenye kitabu cha ufunuo kwamba watu wasiongeze au kupunguza kitu kutoka kwa maneno yake.

Ssa huo ukinzano wa baadhi ya mistari ya vitabu vya injili hauoni vinakiuka maagizo yake?

Je huoni ingetumika source moja kuu say Q source ingesolve changamoto hii?
Kwanza nakupongeza kwa kuanzisha mada kama hii.Nyingine hata vichwa vya habari vinatia kichefu chefu.

Halafu ama Biblia hujaisoma vizuri( sio lazima uelewe) au hoja yangu umeipitia juu kwa juu.

Kwenye Biblia na hasa agano jipya kuna maneno aliyosema Yesu mwenyewe lakini hakuyaandika yeye.

Na inaonyesha hakuamua kuandika kitabu kwasababu kusoma alikuwa anafahamu.

Hayo maandishi ambayo inasemekana alisema Yesu mwenyewe, kwenye Biblia nyingine yameandikwa kwa rangi nyekundu ili kurahisisha wasomaji. Na pia nakukumbusha biblia hata agano jipya yako maneno mengine ambayo sio ya Yesu.

Na hata yaliyokuwa ya Yesu Yesu mwenyewe hakushika kalamu kuandika kitabu. Hivyo pointi yangu ya kwanza uizingatie.Binadamu ni Binadamu.
 
Kwanza nakupongeza kwa kuanzisha mada kama hii.Nyingine hata vichwa vya habari vinatia kichefu chefu.

Halafu ama Biblia hujaisoma vizuri( sio lazima uelewe) au hoja yangu umeipitia juu kwa juu.

Kwenye Biblia na hasa agano jipya kuna maneno aliyosema Yesu mwenyewe lakini hakuyaandika yeye. Hayo maandishi kwenye Biblia nyingine yameandikwa kwa rangi nyekundu ili kurahisisha wasomaji. Na pia nakukumbusha biblia hata agano jipya yako maneno mengine ambayo sio ya Yesu.

Na hata yaliyokuwa ya Yesu Yesu mwenyewe hakushika kalamu kuandika kitabu. Hivyo pointi yangu ya kwanza uizangatie.Binadamu ni Binadamu.
Mkuu issue yangu sio direct quotation ya maneno ya Yesu au kuweka maneno yasiyo ya Yesu ila mfano hapo juu nimeeleza vzuri.....

Mark 8:12 na Mathew 12:39.... Yesu anasema hatoi ishara mara tena anatoa Ishara moja tu. Then ndio hapo either wameongeza au wamepunguza quotation zake but mmoja lazima awe amepotosha.

Na hapo changamoto sio binadamu bali ni vyanzo walivyotumia kuwa vingi.... Kma wangetumia common source huoni ingefuta contradiction hizi?
 
Mkuu issue yangu sio direct quotation ya maneno ya Yesu au kuweka maneno yasiyo ya Yesu ila mfano hapo juu nimeeleza vzuri.....

Mark 8:12 na Mathew 12:39.... Yesu anasema hatoi ishara mara tena anatoa Ishara moja tu. Then ndio hapo either wameongeza au wamepunguza quotation zake but mmoja lazima awe amepotosha.

Na hapo changamoto sio binadamu bali ni vyanzo walivyotumia kuwa vingi.... Kma wangetumia common source huoni ingefuta contradiction hizi?
Ok hiyo common source usilazimishe. Hiyo ipo kwenye dini nyingine. Yesu alijua kusoma na kuandika na alipokuwa anaondoka aliaga vizuri sana na aliacha maagizo kibao. Lakini hakuyaandika na alijua mapungufu ya mitume wake hata yeye mwenyewe walimzingua sana.


Common source ndio kushushwa. We acha ilivyo kama ilivyo.

Kwa taarifa yako hata hao wenye common source wana contradiction. Sababu wewe ni mwanazuoni tumia intanet ikusaidie utaona hao wenye common source pia wana contradiction.

Sasa hiyo ni balaa wakidai source yao ni Mwenyezi Mungu mwenyewe halafu wana contradiction.
 
Mwisho nawakumbusha wote wanaosoma Biblia hakuna contradiction katika mstari huu Yohana 14: 6
 
Habari za jioni wana JF, ni muda mrefu kidogo sijaweka mada humu ila leo tupate wasaa kidogo tukumbushane mambo machache kuhusu Bible.

NB: Angalizo hii mada ni purely objective tusiiweke kidini na kuanza kashfa, matusi na kejeli kwa imani fulani. Natamani iwe hoja juu ya hoja ili wote tujifunze.
View attachment 1703065

Utangulizi
Kumekua na contradiction sana kwenye vitabu vya gospel hata kwa vitu vidogo tu mfano tarehe ya Yesu kuzaliwa na kufa ama Story ya wale wafungwa pembeni ya Yesu msalabani n.k. Na huu mkinzano unawapa fursa watu kuiona Biblia kama nadharia tu au hadithi za kufikirika (Myhtology) na sababu kuu ni taarifa kadhaa kukinzana.

Kutokuwepo kwa vyanzo halisi vya injili nayo imekua changamoto na inafikia wakati watu wanahoji uhalisia wa matukio ya kipindi cha Yesu. Yaani yalikua verified wapi ama version ipi ya vitabu vya injili ni credible zaidi. Ili kusolve haya yote wanatheolojia walijaribu kujikita katika kutafuta vyanzo vya vitabu vya injili.

Q Source
Msimamo uliopo kwenye ulimwengu wa kitheolojia na imani ni kwamba kitabu cha kwanza kuandikwa ni Marko maana ushahidi ni kwamba Mathayo na Luka wamenakiri masuala mengi kutoka injili ya Marko. LAKINI kuna maandiko yaliyopo katika Mathayo na Luka ILA hayapo kwenye injili ya Marko. Hiko chanzo cha pili kikapewa nickname ya Q yaani Quelle source.
View attachment 1703067
Chanzo hiki kina nadharia mbili kwanza; ni simulizi za moja kwa moja walizosikia hao waandishi wa Mathayo na Luka kutoka kwa Yesu na wanafunzi wake. Nadharia ya Pili ni kwamba ni maandiko yaliyoandikwa yakiwa na yamenakiriwa original kabisa kutoka kwa Yesu ama wanafunzi wake.

Kupitia nadharia ya pili swali linakuja.... Je Q source iliandikwa na nani?

Q source kwanini isingekua kitabu kabisa kwenye Biblia?

Je kilifichwa ili kuondoa ukweli wa taarifa fulani?

Kuondoa sintofahamu
Ikumbukwe kma Q source ni original script yenye uhalisia zaidi. Ingesaidia kuondoa sintofahamu hasa kwa kukinzana kwenye masuala kadhaa ya kibiblia mfano nitoe

Mathayo 2:1 inaonyesha Yesu alizaliwa kipindi cha Herode (4 BC) ila Luka 2:2-3 inaonyesha Yesu alizaliwa kipindi cha Governor Quirinius (6 AD). Ila kungetumika source moja tu mfano hyo Q source ingesaidia kuondoa discrepancy zote zilizopo na kuweka msimamo mmoja wa Injili.

Mat 12:39 Akajibu, akawaambia, Kizazi kibaya na cha zinaa chatafuta ishara, wala hakitapewa ishara, ila ishara ya nabii Yona

Marko 8:12
12 Akaugua rohoni mwake, akasema, Mbona kizazi hiki chatafuta ishara? Amin, nawaambieni, Hakitapewa ishara kizazi hiki.

Mfano hapa je mtu wa kizazi kile ataamini kipi? Yesu alitoa ishara ama hakutoa yoyote? Je haiwezi mchanganya mtu kiimani?
View attachment 1703066
Hitimisho
Nimeleta mada ili tujadili hapa je Q source ipo? Na kama Ipo Iko wapi? Je ingeweza kusaidia kuondoa ukinzano? Je ukinzano huu wa injili hauondoi credibility ya Biblia kma kitabu kitakatifu (maana tunaamini imeandikwa kwa uvuvio wa Roho Mtakatifu)

Karibuni kwa mjadala
SHALOM! Zitto Jr.

Kwanza Kabisa pongezi kwako kwa Utafiti na uchunguzi wa Maandiko!
Vitabu vya Injili vyote - Four Gospel kwa jina moja vinajulikana kama Synopsis kutokana na Ujumbe zilioubeba unafanana kwa ukaribu sana.

Mathayo - Amejikita katika katika Ukoo wa Yesu.
Luka - ameeleza Maisha ya Yesu kwa Ujumla wake bila Kubakiza.
Marko - inakazia matendo,Uthabiti na Uimara wa Misheni ya Yesu
hasa hasa mwishoni mwa maisha yake.
Yohana - Anamweleza YESU kwa Nafasi ambayo injili zote hazijamueleza kabisa,Yaani Ukuu na Uungu wa YESU,Mamlaka na Nafasi yake Katika Utatu Mtakatifu - Kifupi Inaeleza Mamlaka Makuu ya YESU kama MUNGU.

Nani aliviandika Vitabu haina Maana sana kwangu Mimi niungane na Mchangiaji mwenzangu aliyepita - Kikubwa ni Ujumbe Mahususi uliobebwa hapo.

Hiyo unaoiiita Q Theory ni Nadharia ya Watu wadadisi ambao hauwezi kujibiwa kwa urahisi kiasi hicho - Mtu katengeneza Swali ambalo ni uhakika linatokana na Utofauti wa maneno machache sana ambayo hayapotezi maana ya Msingi (Intellectual arguments).

Mfano :- Mathayo 2:1 inaonyesha Yesu alizaliwa kipindi cha Herode (4 BC) ila Luka 2:2-3 inaonyesha Yesu alizaliwa kipindi cha Governor Quirinius (6 AD). Ila kungetumika source moja tu mfano hyo Q source ingesaidia kuondoa discrepancy zote zilizopo na kuweka msimamo mmoja wa Injili.

JIBU:- YESU alizaliwa Wakati wa Utawala wa WARUMI,Rumi iliitawala Yerusalemu na kuweka Indirect Rule ili kutosababisha Sintofahamu za utofauti wa Mila na Desturi za Wayahudi na Warumi ( HAWACHANGAMANI KABISA NA MATAIFA - GOYIM). Ndio maana wakaruhusu awepo Mtawala anayejua Mambo yao HERODE.
Hivyo kwa mantiki hiyo hakuna Utofauti hapo - Herode alikuwepo na Warumi walikuwepo - Overlapping.

Mwisho - Yapo mambo mengi yenye Utofauti kwa Mfano Kwenye Mathayo 7:7 ... Yesu ametumia mfano wa JIWE na MKATE, kwenye Marko akiyarudia Maneno yale yale ametumia Mfano wa YAI na NGE. - Maneno Tofauti Maana Ile ile.
No big Deal here.

Ikumbukwe hayo yalioandikwa ni machache sana ya yale yaliyotukia katika Maisha ya YESU - Biblia imelisema hili vema kabisa,kuwa iwapo yote yangeliandikwa isingetosha...

Asante .
 
Kwanza nakupongeza kwa kuanzisha mada kama hii.Nyingine hata vichwa vya habari vinatia kichefu chefu.

Halafu ama Biblia hujaisoma vizuri( sio lazima uelewe) au hoja yangu umeipitia juu kwa juu.

Kwenye Biblia na hasa agano jipya kuna maneno aliyosema Yesu mwenyewe lakini hakuyaandika yeye.

Na inaonyesha hakuamua kuandika kitabu kwasababu kusoma alikuwa anafahamu.

Hayo maandishi ambayo inasemekana alisema Yesu mwenyewe, kwenye Biblia nyingine yameandikwa kwa rangi nyekundu ili kurahisisha wasomaji. Na pia nakukumbusha biblia hata agano jipya yako maneno mengine ambayo sio ya Yesu.

Na hata yaliyokuwa ya Yesu Yesu mwenyewe hakushika kalamu kuandika kitabu. Hivyo pointi yangu ya kwanza uizangatie.Binadamu ni Binadamu.
Wanasema yesu akuwa anajua kusoma wala kuandika bwashee.
 
SHALOM! Zitto Jr.

Kwanza Kabisa pongezi kwako kwa Utafiti na uchunguzi wa Maandiko!
Vitabu vya Injili vyote - Four Gospel kwa jina moja vinajulikana kama Synopsis kutokana na Ujumbe zilioubeba unafanana kwa ukaribu sana.

Mathayo - Amejikita katika katika Ukoo wa Yesu.
Luka - ameeleza Maisha ya Yesu kwa Ujumla wake bila Kubakiza.
Marko - inakazia matendo,Uthabiti na Uimara wa Misheni ya Yesu
hasa hasa mwishoni mwa maisha yake.
Yohana - Anamweleza YESU kwa Nafasi ambayo injili zote hazijamueleza kabisa,Yaani Ukuu na Uungu wa YESU,Mamlaka na Nafasi yake Katika Utatu Mtakatifu - Kifupi Inaeleza Mamlaka Makuu ya YESU kama MUNGU.

Nani aliviandika Vitabu haina Maana sana kwangu Mimi niungane na Mchangiaji mwenzangu aliyepita - Kikubwa ni Ujumbe Mahususi uliobebwa hapo.

Hiyo unaoiiita Q Theory ni Nadharia ya Watu wadadisi ambao hauwezi kujibiwa kwa urahisi kiasi hicho - Mtu katengeneza Swali ambalo ni uhakika linatokana na Utofauti wa maneno machache sana ambayo hayapotezi maana ya Msingi (Intellectual arguments).

Mfano :- Mathayo 2:1 inaonyesha Yesu alizaliwa kipindi cha Herode (4 BC) ila Luka 2:2-3 inaonyesha Yesu alizaliwa kipindi cha Governor Quirinius (6 AD). Ila kungetumika source moja tu mfano hyo Q source ingesaidia kuondoa discrepancy zote zilizopo na kuweka msimamo mmoja wa Injili.

JIBU:- YESU alizaliwa Wakati wa Utawala wa WARUMI,Rumi iliitawala Yerusalemu na kuweka Indirect Rule ili kutosababisha Sintofahamu za utofauti wa Mila na Desturi za Wayahudi na Warumi ( HAWACHANGAMANI KABISA NA MATAIFA - GOYIM). Ndio maana wakaruhusu awepo Mtawala anayejua Mambo yao HERODE.
Hivyo kwa mantiki hiyo hakuna Utofauti hapo - Herode alikuwepo na Warumi walikuwepo - Overlapping.

Mwisho - Yapo mambo mengi yenye Utofauti kwa Mfano Kwenye Mathayo 7:7 ... Yesu ametumia mfano wa JIWE na MKATE, kwenye Marko akiyarudia Maneno yale yale ametumia Mfano wa YAI na NGE. - Maneno Tofauti Maana Ile ile.
No big Deal here.

Ikumbukwe hayo yalioandikwa ni machache sana ya yale yaliyotukia katika Maisha ya YESU - Biblia imelisema hili vema kabisa,kuwa iwapo yote yangeliandikwa isingetosha...

Asante .
Nakushukuru sana ..itoshe tu kwa hayo
 
SHALOM! Zitto Jr.

Kwanza Kabisa pongezi kwako kwa Utafiti na uchunguzi wa Maandiko!
Vitabu vya Injili vyote - Four Gospel kwa jina moja vinajulikana kama Synopsis kutokana na Ujumbe zilioubeba unafanana kwa ukaribu sana.

Mathayo - Amejikita katika katika Ukoo wa Yesu.
Luka - ameeleza Maisha ya Yesu kwa Ujumla wake bila Kubakiza.
Marko - inakazia matendo,Uthabiti na Uimara wa Misheni ya Yesu
hasa hasa mwishoni mwa maisha yake.
Yohana - Anamweleza YESU kwa Nafasi ambayo injili zote hazijamueleza kabisa,Yaani Ukuu na Uungu wa YESU,Mamlaka na Nafasi yake Katika Utatu Mtakatifu - Kifupi Inaeleza Mamlaka Makuu ya YESU kama MUNGU.

Nani aliviandika Vitabu haina Maana sana kwangu Mimi niungane na Mchangiaji mwenzangu aliyepita - Kikubwa ni Ujumbe Mahususi uliobebwa hapo.

Hiyo unaoiiita Q Theory ni Nadharia ya Watu wadadisi ambao hauwezi kujibiwa kwa urahisi kiasi hicho - Mtu katengeneza Swali ambalo ni uhakika linatokana na Utofauti wa maneno machache sana ambayo hayapotezi maana ya Msingi (Intellectual arguments).

Mfano :- Mathayo 2:1 inaonyesha Yesu alizaliwa kipindi cha Herode (4 BC) ila Luka 2:2-3 inaonyesha Yesu alizaliwa kipindi cha Governor Quirinius (6 AD). Ila kungetumika source moja tu mfano hyo Q source ingesaidia kuondoa discrepancy zote zilizopo na kuweka msimamo mmoja wa Injili.

JIBU:- YESU alizaliwa Wakati wa Utawala wa WARUMI,Rumi iliitawala Yerusalemu na kuweka Indirect Rule ili kutosababisha Sintofahamu za utofauti wa Mila na Desturi za Wayahudi na Warumi ( HAWACHANGAMANI KABISA NA MATAIFA - GOYIM). Ndio maana wakaruhusu awepo Mtawala anayejua Mambo yao HERODE.
Hivyo kwa mantiki hiyo hakuna Utofauti hapo - Herode alikuwepo na Warumi walikuwepo - Overlapping.

Mwisho - Yapo mambo mengi yenye Utofauti kwa Mfano Kwenye Mathayo 7:7 ... Yesu ametumia mfano wa JIWE na MKATE, kwenye Marko akiyarudia Maneno yale yale ametumia Mfano wa YAI na NGE. - Maneno Tofauti Maana Ile ile.
No big Deal here.

Ikumbukwe hayo yalioandikwa ni machache sana ya yale yaliyotukia katika Maisha ya YESU - Biblia imelisema hili vema kabisa,kuwa iwapo yote yangeliandikwa isingetosha...

Asante .
Nashukuru kwa Mchango wako mkuu lakini ningependa tuweke facts straight!!

1. Si kweli kwamba Q source ina maneno machache tu bali inabeba zaidi ya 42% ya kitabu cha Luke ikimaanisha karibu nusu ya kitabu cha Luka hakina maneno kutoka Marko ambaye ndio alikua chanzo kikuu kwake na Mathayo.
Sasa kma 42% ya maandiko ya kitabu cha injili hayafahamiki source yake je hatuoni ndio chanzo cha ukinzano.

2. Umedai kwamba haitoi context halisi kuna mfano niliweka hapo juu

Yesu alisema kizazi kinasubiri ishara ili kiamini.... Majibu ni haya

Mark 8:12 kizazi hakitapewa ishara
Mat 12:39 hakitapewa ishara, ila ishara ya nabii Yona

Je mkuu kitu kama hiki huoni kinaleta discrepancy..... Na mifano ni mingi sana tena mikubwa kabisa.

Mfano wale wezi pale msalabani kuna wakati tunafundishwa mmoja alimkiri Yesu but Q source na vyanzo vingine vinakinzana.

Mark 23 Inasema Mwizi mmoja alimkiri Yesu huku mwingine akimkejeli

Mathayo 27 inasema Wote wawili walimkejeli Yesu.

Sasa mfano kma huu sio crucial kwenye mafundisho? Haina impact yeyote kwenye kudistort ukweli kwamba Yesu huwa na msamaha kwa watu wote irrespective of their past deeds?
 
Back
Top Bottom