Biblia kwa Jicho Jingine

Mkuuuu hata ww unaamiin hhayupo ila haujui kama hayupo?


Ivyo imani ni bora kuliko kujua.
Mimi siwez kumsaidia Mungu Majukumu Yake ww kamaHuamini uwepo wake huwez kubali Majibu yangu,
Huwezi kumsaidia Mungu majukumu yake.

Umesemakweli.

Huwezi kumsaidia Mungu majukumuyake, kwa sababu Mungu hayupo.

Kama unabisha, thibitisha yupo.
 
Wasabato pia huwa wana version yao kuhusu Roho mrakatifu. Najua si mjadala kuhusu RM ila nilitaka kuchangia kidogo hapo. Naendelea kufatilia
 
Mkuu phoneme hujakutana na maandiko yanayoelezea jinsi Yohana alivyoona mji mtakatifu ukishuka au Yesu alivyosema anaendatuandalia makao yet hapa unasema majengo yatabaki ? Au mimi sielewi?
 
Mkuu Hii makala ipo Vizuri sana, japo baadhi unayoongea hapo hayapo kwenye Biblia...
Vp umewahi kufika Mbinguni, maana naona kama movie vile!
 
Hujaelewa kitu kidogo tu. Ukifa leo na ulimkiri Yesu Kristo kuwa ni bwana na ukakaa ktk maaguzo yake utaenda mbinguni. Baada ya dnia hii kufika mwisho wake yale makao yaliondaliwa na Yesu yatashuka hapa duniani na siyo hii ya sasa umeshau habari ya nchi mpya na mbingu mpya mara hii ? Si usome ufunuo. Kumbuka si mpango wa Mungu sisi tukaishi Mbinguni, tangu mwanzo sisi ni wa hapa hapa. Ila tutakaa ktk nchi mpya siyo hii...hapana utashuka mji mwingine si majengo haya
 
James umesoma ayo maandiko niliyoyaweka? Na wewe hizi habar zako mbona hazina maandiko? Kama nikifa leo naenda mbinguni moja kwa moja embu nieleweshe suala la ufufuo! Nitafufuliwa lini?
Kama umetenda mema ni paradiso, paradiso ni kama mbinguni au ni kama mtu aseme reception ya hotel tuu...lakini reception si iko hotelini hapo nimejumuisha. Ni sawa na kuzimu na jehanamu ya moto. Kule raha huku ktk kuzimu na jehanum kote ni shida tuu
 
Mkuu jadili mada Mtume (S.AW) ebu muache kwanza utatuaribia uzi huu
 
Mkuu jadili mada Mtume (S.AW) ebu muache kwanza utatuaribia uzi huu
jina La Yesu halitajwi ovyo kama unavyofikiri.usisahau ata wachawi na washirikina pia wanalitaja.na hata biblia imezungumza kuhusu hao wanaolitaja bure na siku za mwisho atawakana kwakua walilitaja bure bila kumaanisha.
 
jina La Yesu halitajwi ovyo kama unavyofikiri.usisahau ata wachawi na washirikina pia wanalitaja.na hata biblia imezungumza kuhusu hao wanaolitaja bure na siku za mwisho atawakana kwakua walilitaja bure bila kumaanisha.
Unamaanisha nini mkuu?
 
Mada nzuri,nice presentation! Naomba rejea zako tafadhali.
 
Kabla ya yote hayo, thibitisha Mungu yupo.

Sikumbuki ni Injili gani kati ya vitabu ambavyo havikuweka kwenye Biblia aliulizwa Yesu na watu wasioamini kuwa Mungu yupo.

Imeeandikwa humo kuwa Yesu alijibu swali hilo kwa mfano huu.

Kuwa katika mto fulani kulikuwa na samaki wasioamini kuwa kuna maji, wakamwendea samaki mmoja mzee wakamwuliza kama kuna maji, Yule samaki akawaambia kwa suala hili nendeni baharini mtamkuta samaki mmoja mwenye hekima huyo atawaeleza na kuwapa majibu yenu.

wale samaki wakaenda kama walivyoagizwa, walipofika kule wakamweleza yule samaki kuhusu mashaka yao kuhusu kuwepo kwa maji.

Yule samaki mwenye busara akawaambia hamuamini kuhusu kuwepo kwa maji, wakati ndani yake mnazaliwa, mnaishi, mnakula mnakwenda na ndani yake mnakufa.

Kuwepo kwa aliyeumbwa maana yake Muumba yupo, kuwepo kwa meza na viti maana yake seremala yupo. Kuwepo kwangu mimi maana yake yupo aliyeniumba, ukitaka kumuona Mungu angalia kazi zake mojawapo ni mimi.

Hao unaowataja kwa sasa hawapo, lakini kazi zao ndizo unazozisoma.

Hata akilini inatambulika kwa kazi zake haonekani kwa macho, sina hakika ulishawahi kukutana na akili macho kwa macho.

Ukitaka kumuona Mungu angalia kazi zake, amekupa utashi wa kuchagua kuamini au kutokuamini. Kutokuamini kwako hakumfanyi apungue wala kuamini kwako hakumfanyi aongezeke.

Mungu anatawala na kukaa na watu kwa njia ya imani na kuwafanya watu kuwa wema kama yeye alivyomwema na nimaamuzi ya mtu mwenyewe kuamini au kutokuamini. Hapa msistizo uko kwenye mtu zaidi ya mwili na vya mwilini. Mungu naye ana watu anaowaita watu wake. Nao hao wako kwenye jitihada za kuwaongeza watu waaminio Mungu na nguvu zake.

Shetani anatawala watu kwa njia ya hofu na kwafanya watu waovu kama yeye alivyomuovu. Hapa msisitizo uko kwenye mambo ya mwilini na vionjo vyake. Ndilo linapokuja swali la ulishawahi kumuona Mungu kwa macho msisitizo ni kwenye mambo ya mwilini. Shetani nae anawatu wake ambao wamejitoa kwa kujua au kutokujua kufanyakazi zake mojawapo ni kuasi tu mambo ya Mungu, ikiwezekana msisitizo uwe hayupo tu.

Kwa hiyo ninakuona wewe unapost humu ni uthibitisho tosha kuwa Mungu yupo na shetani yupo pia.

Yeremia kuna sehemu aliambiwa nenda kwa mfinyanzi na kule nitaongea na wewe, alipofika kule alimkuta mfinyanzi akifanya kazi yake ya kufinyanga na aliamua analotaka udongo huu akatengeneza kikombe huu sahani kadri ya maamuzi yake. Mungu akamuuliza yeremia je Mimi nisiwe na uamuamuzi wa kufanya mambo kadri nitakavyo kama afanyavyo mfinyanzi huyu?

Kuishi katika mwili huo ilionao milele sio mpango wa Mungu hata kama unaupenda sana huo mwili wako, siku ikifika utachomoka tu. Ni hekima yake Mwenyezi ambayo hata unayoyaona mapumbavu ni zaidi sana ya hekima ya mwanadamu. Na hao unaosema wapenzi wako katika mwili huu wataondoka na wewe utailia vilevile, shida hasa kwako kulia kwako ni kubaya kwa sababu huna tumaini baada ya kufa, tofauti na wenye tumaini baada ya kufa.

Bwana uinuke utende sawasawa na mapenzi yako, kwani ni nani atakuuliza unafanya nini hapo? Sikumbuki huu mstari unapatika wapi? Naona ni vyema kufunga na mstari huo kwa sasa
 
Mungu ajidhihilisha ktk kazi zake, waisrael walimuomba akutane nao live wakisema kwa nini aongee na Muda pekee, lakini Mungu alishuka katikaumbo la kazi zinazomtukuza mfano moto, mawe yakatoa moshi, ngurumo, nk
 
[emoji3][emoji16][emoji16] kaazi kwelikweli
 
jina La Yesu halitajwi ovyo kama unavyofikiri.usisahau ata wachawi na washirikina pia wanalitaja.na hata biblia imezungumza kuhusu hao wanaolitaja bure na siku za mwisho atawakana kwakua walilitaja bure bila kumaanisha.
mzee mbona unakuwa mbovu wa uelewa?
hebu soma juu comment yangu
utanielewa nilikuwa namanisha kipi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…