5523
JF-Expert Member
- Nov 13, 2014
- 2,275
- 2,410
Vita inaingia kwenye sura nyengine
20 Novemba 2024
Rais wa Marekani Joe Biden amekubali kuipa Ukraine mabomu ya kutegwa ardhini, afisa wa Marekani ameiambia BBC.
Afisa huyo ambaye alizungumza kwa sharti la kutotajwa jina, anasema mabomu ya aina hiyo yatapelekwa hivi karibuni na Washington inatarajia yatatumika katika eneo la Ukraine.
Kyiv pia imeahidi kutotumia mabomu hayo katika maeneo yenye raia wa Ukraine, afisa huyo amesema.
Hatua hiyo inaonekana kama jaribio la kupunguza kasi ya wanajeshi wa Urusi ambao wamekuwa wakisonga mbele kwa kasi mashariki mwa Ukraine katika miezi ya hivi karibuni.
20 Novemba 2024
Rais wa Marekani Joe Biden amekubali kuipa Ukraine mabomu ya kutegwa ardhini, afisa wa Marekani ameiambia BBC.
Afisa huyo ambaye alizungumza kwa sharti la kutotajwa jina, anasema mabomu ya aina hiyo yatapelekwa hivi karibuni na Washington inatarajia yatatumika katika eneo la Ukraine.
Kyiv pia imeahidi kutotumia mabomu hayo katika maeneo yenye raia wa Ukraine, afisa huyo amesema.
Hatua hiyo inaonekana kama jaribio la kupunguza kasi ya wanajeshi wa Urusi ambao wamekuwa wakisonga mbele kwa kasi mashariki mwa Ukraine katika miezi ya hivi karibuni.