Bidhaa tokea Kenya zilipanda sana mwanzoni mwaka huu

Bidhaa tokea Kenya zilipanda sana mwanzoni mwaka huu

masai dada

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2013
Posts
16,207
Reaction score
14,343
Mwishoni mwa mwaka jana, baadhi ya bidhaa, hasa zile zinazotumika kupika vitu mbalimbali, zilikuwa na bei ya chini. Hata hivyo, mwanzoni mwa mwaka huu hadi mwezi wa tatu, bei ya bidhaa hizi zilikuwa zimepanda sana.

Naamini hasira nyingi za Wakenya zinaelekea kwenye mswada wa marekebisho ya kodi. Hata kabla ya mswada huu, bidhaa zilikuwa tayari zimeanza kupanda bei. Sasa, je, mswada wa marekebisho ya kodi ukipita itakuaje?

Kwa mfano, tunaingiza siagi kutoka Kenya ambayo ni bora sana. Kwa sasa, bei yake imepanda na haimiliki kabisa. Pia, icing sugar ambayo hatuzalishi nchini, tunaiagiza. Hadi mwezi wa tatu mwaka huu, bei yake kutoka kiwandani ilikuwa Tsh 60,000 kwa carton, lakini sasa ni Tsh 81,000 ikiwa hapo Trufoods kabla hata ya kuitoa nje ya geti.

Hizi ni baadhi tu ya bidhaa nyingi ambazo bei yake imepanda sana.

Kwa ladha, kwa mfano, fleva za vyakula za mls 50 kutoka kampuni maarufu Kenya zilipanda kutoka Tsh 1,800 hadi Tsh 3,000 kabla hujaitoa hapo Keekrok Road.

Hata sisi tutaathirika sana na ongezeko hili la bei, kwa sababu kodi kubwa hulipwa na mlaji wa mwisho. Kumbuka, tunaingiza bidhaa nyingi sana kutoka Kenya. Waokaji, nafikiri mlishaanza kuonja joto hili kuanzia mapema mwaka huu.

#Wakenya wana kila sababu ya kuandamana

F3E4F226-6648-43F8-BD89-9165087579A0.png
 
Changamoto mno kwa kweli.
Sana na ubaya ni bidhaa za kuzalisha vyakula kwa mfano mkate
Mkate unatumika sana kenya
Ukishapandiaja unga,sukari,siagi
Tayari bei ya mkate iko juu
Ni slightly tu baada ya ruto kuingia vitu vilianza kupanda
Na hata sijui kwa sababu gani
 
Sana na ubaya ni bidhaa za kuzalisha vyakula kwa mfano mkate
Mkate unatumika sana kenya
Ukishapandiaja unga,sukari,siagi
Tayari bei ya mkate iko juu
Ni slightly tu baada ya ruto kuingia vitu vilianza kupanda
Na hata sijui kwa sababu gani
Tulivyo kuwa tunafuatilia kampena za Ruto tulidhani kenya watakuwa wamepata bahati ya pekee, lakini matokeo yametofautiana na matarajio.
Siasa kwa ujumla wake zinakuwa mbaya sana haswa zinavyo ingilia maslahi ya uma ya wengi.

Naendelea kuwaunga waandamaji huko kenya , huwenda itachipusha nuru mpya hata kwetu pia.
 
Tulivyo kuwa tunafuatilia kampena za Ruto tulidhani kenya watakuwa wamepata bahati ya pekee, lakini matokeo yametofautiana na matarajio.
Siasa kwa ujumla wake zinakuwa mbaya sana haswa zinavyo ingilia maslahi ya uma ya wengi.

Naendelea kuwaunga waandamaji huko kenya , huwenda itachipusha nuru mpya hata kwetu pia.
Sahihi kabisa
Kenya ina export all over africa
Maamuzi ya wabunge yalitakiwa yaangalia hata hali ya uchumi wa dunnia kwa ujumla
 
Sahihi kabisa
Kenya ina export all over africa
Maamuzi ya wabunge yalitakiwa yaangalia hata hali ya uchumi wa dunnia kwa ujumla
Mimi nadhani wanasiasa wengi wakiwemo wabunge huwa hawana maslahi na mambo yanayo gusa uma kwa ujumla wa yote, wabunge wa kenya walicho fanya leo hawana tofauti na wabunge wa Tanzania ambao kiujumla tunadhubutu kuwaita wasaka tone.
 
La kariakoo ushuru wanaotozwa wafanya biashara mpka inafika nandilinyi huko huoni unaona ya Kenya kweli nyan haoni kundule
 
Kesho nitajipa muda nisome chanzo cha huu maandamano

Nijue ukweli na uongo
 
Back
Top Bottom