Bidhaa za China kuuwa uchumi wa Africa

maaka

Senior Member
Joined
Jan 8, 2014
Posts
109
Reaction score
44
Matokeo ya nchi zinazoendea ikiwemo tanzania kuamua kutokuzalisha bidhaa zake yenyewe na kukimbilia kuagiza tuu bidhaa feki za China... ni sababu kubwa na ya msingi inayosababisha mfumuko wa bei na umaskini. Najua wewe pia na shuhuda kwa kuwa na namna moja au nyingine umewahi kuzitumia bidhaa za china tena nyingi zikizalishwa kienyeji hapahapa tz....inasikitisha. angalia Mfano wa bidhaa nilizotumia za kichina na matokeo yake.

Viatu vya mtoto vya elfu 10 vimedumu siku mbili
Kabati la kichina laki 3 limedumu mwaka 1

Calculator aina ya casio elfu 25 imedumu siku 3

Chupa ya chai elfu 30 imekaa miezi 2

blender kachine ya elfu 40 imedumu mwezi 6

meza ya kioo ya laki na ishirini imekaa 1 year.

and much more....
hoja sasa kwa nini watengeneze bidhaa feki hata wanadai wanawezapia kutengeneza bidhaa nzuri ila sera yao ni kuwa cheap(fake) for Africa market. What kind of partnership is this? Hapo tumeangalia tuu bidhaa za nyumbani bado dawa na mengeniyo. Hivi nini maana ya standards? TBS Mpo? Serikali mpo. MUNGU TUOKOE WAAFRIKA HASA TZ
 
Mi kwa mtazamo wangu ni kwamba sisi wenyewe ndio tunaoua uchumi wetu,vingi ama karibu ya vyote ulivyotaja vinatengenezwa huko hulo kwao na ni watz kama wewe ndio wanao vifuata na kuvileta huku.

Pili ni kwamba tuna taasisi za kuhakiki viwango ambazo hazina hata mchina mmoja,iweje sasa vitu hivyo vinaingia sokoni???

Mwosho ni kwamba china wanavyo vitu bora vingi sana,tatizo tukienda kununua tuna chagua vibovu ilihali tunajua ama tulidanganywa na bei nafuu.

Hili ni la kwetu na si china,japo ni kweli uchumi utaathirika maana hatubadiliki.
 
tz tu ndio bongo lala mkuu wengine wana standard huwezi ingiza vitu feki kwao ata apo kwa jirani zetu kenya :embarassed2:
 
 
Ulaya na US wanatumia bidhaa zao toka China na viwanda vingi vimehamia China hata ofisi zao za makampuni mengi wana makazi china na india, hizo bidhaa zina viwango kwa mfano Nike utapata mpaka $200 lakini ukifika Dar unanunua cha kiwango cha chini shilling 30,000, sasa ukiletewa kwa laki 3 ni wangapi watanunua ndio maana mmnapendelea cheap goods wakati mwingine nunua yenye ubora, pia serikali inachangia kuingiza bidhaa feki, mbona enzi zetu kulikuwa mambo haya hakuna vitu vyote vilikuwa vyenye ubora? Lakini mwenye uwezo alikuwa ananunua kama serikali ingekataa feki na kuwapiga faini wachina wanawauzia watanzania bidhaa mbovu kushirikiana na serikali ya China tusingekuwa na feki
 
UK USA wanatumia pia vitu toka China mbona vyao vinadumu?

Swali zuri sana!

Utofauti ni kwamba kuna bidhaa za Kichina zinazotengenezwa mahsusi kwa Africa (ubora duni) na kuna zile zinazotengenezwa kwa ajili ya nchi nyingine (imara sana).

Wengi wanasema tatizo ni wafanyabiashara wetu na mitaji yetu. Wengine wanasema serikali za Kiafrica ndo haziko makini kufuatilia ubora wa bidhaa kwa kisingizio cha soko huria.

Mimi naomba nije na hoja tofauti. Tatizo letu ni mawazo ya watu wetu; wafanyabiashara, serikalini na wateja - wengi wanaangalia leo tu wala si kesho. Uchumi wa nchi haujengwi kwa kuingiza bidhaa kiholela bila udhibiti wa ubora wake!
Lakini huko mashuleni na vyuoni ni kwanini jitihada zisifanyike kuwawezesha vijana/watu kibao wenye utundu, ujuzi na vipaji adimu ili nchi ifikie kipindi inauwezo wa kuendeleza teknolojia yake??! Tumekalia elimu ya vitabuni tuuu bila kuzingatia elimu ya vitendo!!

Elimu ya biashara inahimiza sana kusoma kwa undani na kuainisha mahitaji ya wateja, sheria za nchi husika na kipato vile vile... Hapa ndipo wachina walifanya tafiti zao wakabaini kuwa soko letu linahitaji nini na ndicho wanacholileta sokoni.

Binafsi natumia simu ya KICHINA iliyonunuliwa ebay (UK). Yaani huwezi kubaini kuwa ni ya KICHINA hadi usome label ndani yake! Na bei yake si ghali sana ukilinganisha na za KICHINA zinazouzwa humu nchini.

Tumekubali kugeuzwa nchi ya wachuuzi bila kujali kuwa "any cheap item is at the end very expensive!"
 
Bila kusahau pikipiki a.k.a bodaboda.

Wachina wamenufaika sana na ujinga na uduni wa nchi za kiafrika...na tumekuwa na mchango mkubwa kwenye ukuaji wa uchumi wao.....na ndio maana wanatukumbatia coz wanajua ndio soko la uhakika kwa viwanda vyao vidogo vya bidhaa gushi.

Hizo bidhaa hazifiki Ulaya, Marekani na hata kwa wenzao wa Asia....mfano mnakumbuka wakati marekani walipogomea bidhaa za midoli ya watoto kutoka China...China walihaha kuweka mambo sawa na kuimaliza ile ishu....so hii ni kuonyesha kuwa wanapodili na watu wenye akili zao, hawako tayari kuharibu.

Tuna wafanyabiashara wa TZ wamekuwa mamilionea kwa hizi biashara za bidhaa Gushi....na hata leo hii wakiamua kujaza madukani bidhaa za Japan, Ulaya na Marekani.....uwezo wa wanainchi kununua ni mdogo.

Tutakapoweza kutengeneza vya kwetu, ndio ufumbuzi...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…