Clouds haitaathirika chochote na kama ingekuwa ni kuathirika wangeathirika wakati wa mgogoro wao na SUGU!! Jide kwa sasa ananunfaika coz' anapata public sympathy na hii itasaidia sana kwenye show yake to the point hata kama ingekuwa ni uwanja wa taifa, angejaza tu! Hata hivyo, hili ni la kupita tu kwani linachangiwa sana na dasturi ya wana-Darisalama na Watanzania kwa ujumla....ni watu wa matukio! Habari ya mujini kwa sasa ni Jide vs Clouds, haya yatapita na si ajabu yasifike hata mwishoni mwa July; Jide atasahaulika na wana matukio kujikita kwenye matukio yaliyo hot!
Jide akitaka kunufaika, ni kabla huu upepo haujapita, anatakiwa kufanya show nyingi iwezekanavyo! Aende Mwanza, Arusha, Mbeya na miji mingine!! Narudia, huu ni upepo tu; JIDE atasahaulika na Clouds wataendelea kuwepo!! By the way, wadau wakubwa wa Clouds ni Wafanyabiashara wakubwa wanaopeleka matangazo pale ambao wala hawana muda wa kusikiliza ujinga unaondelea kwenye mitandao ya kijamii!!
Kuhusu kwamba Clouds watakimbiwa na wasanii, mnajidanganya!! Kila msanii anapenda kazi zake zipigwe Clouds; msizani kwamba haya yanayotokea sasa ndo yatawafanya wasanii wasipeleke kazi zao Clouds! Tuhuma dhidi ya Clouds hazijaanza leo! Kwa wasiofuatilia muziki wanazani hii ndo mara kwanza lakini wanaofuatilia tuhuma dhidi ya Clouds zimeanza miaka kadhaa iliyopita! Tuhuma dhidi ya Clouds zilianza hata kabla ya Sugu hajaanza kuwachana, in fact more than five years ago; lakini bado wasanii wanaendelea kupeleka kazi zao pale!! Hutaki unaacha, lakini Clouds wanaifahamu entertainment industry, wengine wote wanajaribu ili wawe kama Clouds. Na kutokana na ukweli huo, ndio maana msanii nyimbo yake isipopigwa radio station nyingine, husikii maneno lakini isipopigwa Clouds, tayari issue wakati ukweli ni kwamba Radio Station zote, narudia RADIO STATION ZOTE zinabana!!! Haya ya Jide na Clouds wengi wetu tunadandia treni tusiyojua inakotokea wala inakoelekea matokeo ndo haya unakuta hata mtu kama SUGU nae amejiingiza huku akiamini kwamba ni mapambano dhidi ya hujuma kwa wasanii unless kama nae ameamua tu kununua kesi kwavile ana bifu na Clouds na hivyo kuamua kumuunga mkono yeyote atakayetangaza vita na Clouds bila kujali dhima ya vita husika!!