Big RESCUE Now yapandisha ufaulu

swagazetu

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2013
Posts
4,250
Reaction score
1,470
Baada ya serikali kuona haiwezi kuwatimizia mahitaji yao ya mazingira magumu,posho ya kufundishia na kuongeza mshshara,serikali imeamua kuanzisha mpango wa kuwasaidia watoto kufaulu bila kutegemea mwalimu ili kuonesha kuwa madai yao si ya msingi.

Serikali ilikuja na mpango wa Big Results Now ili kuongeza kiwango cha ufaulu.toka mpango huo uanze hakuna maboresho yoyote iwe mshahara kwa waalimu,nyumba za waalimu wala vifaa vya kujifunzia na kufundishia.lakini watoto wamefaulu kwa kiwango cha juu.

Kwa sababu hiyo kwanza watoto hawajafaulu ila wamefaulishwa.

Mpango wa BRN umethihirisha kuwa ni Big Rescue Now kwa wanafunzi yaani mpango wa UOKOAJI kwa wanafunzi.walimu si lengo lengo ni wanafunzi.

Tanzania,Salute.
 
Nimemsikiliza Mh Jenista Mhagama leo asubuhi katika radio fulani akitetea ufaulu wa wanafunzi na kuwalaumu nyinyi munaopinga kila kitu Serikali hii inachofanya, hasa hapo katika suala la ufaulu wa watoto.......ameenda mbali zaidi kwa kusema kuliko tukosoe tu ni kheri pia tukawaelekeza wataalamu wetu nini cha kufanya ili kuepukana na hii hali ya elimu kudorora.........
Mhagama anasema yeye na Waziri wake hawalali wanafikiria nini cha kufanya ufaulu uzidi zaidi miaka ya mbeleni........binafsi nilitamani na mimi nipige simu kummjibu Mh.jenista kitu kimoja tu kuwa, sio kweli kwamba watu wanapenda kukosoa tu bila kutoa ushauri, tatizo ushauri unatolewa lakini haufanyiwi kazi kwani kila kitu siku hizi ni SIASA.

Mashaka yangu ni pale aliposema yeye na Waziri wake hawalali...........sina uhakika na hili.
 
Matekeo form four 2013 : div- 1-3 ni asiimia 21 na div 4 and 0 ni asilimia. 79(
 
Uko sawa kabisa,mimi nachokiona hapa ni kama usanii fulani,hakuna jitihada zozote zilizofanyika ,iwe kwa wanafunzi kujiusomea au kusomeshwa tofauti na mwaka juzi,nachokiona ni kujihadaa wenyewe kwani mwisho wa siku tutakuwa na wasomi wengi wenye vyeti vizuri vya form 4 na 6 lakini ambao hawawezi ku compete kwneye labour market.Unakuta mtu ana A au B ya English lakini muambie aandike sentensi ya Kiigereza hawezi,au form 4 ana A ya Mathematics mpe swali la hesabu la form 2 hawezi kulijibu.Hayo ndiyo matokeo makubwa sasa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…